Posts

Showing posts from May, 2017

JAZA UJAZWE! UPEMBA MWINGI NA TAFSIRI ZA KIMOMBASA

Image
Lugha ya Kiswahili ina maneno lukuki ambayo kama hutakuwa makini katika uchaguzi utaibua sintafahamu na mishangao kwa watu! Hata kabla ya ‘jaza ujazwe,’ neno ‘tigo’ peke yake lina maana nyingine mbali na maana yake! Ama hakika, muhusika wa kitengo cha matangazo kutoka kampuni ya ‘tigo’ atakuwa amefanikiwa sana kuitangaza biashara na ofa hii mpya ya kampuni yake. Lakini mbali na faida hiyo, kuna ukakasi mkubwa ambao umetanda miongoni mwa watu hasa wanaotambaa na maana ya ziada. Wengi hususani wanaume, wanaona neno hili si zuri kutumika na linawadharirisha. Makampuni ya simu yamekuwa na tabia ya kuigana kila inapotokea kampuni mojawapo ikaja na ubunifu wa kuvutia. Lakini katika hili makampuni pinzani bado yako kimya, hakuna aliyejibu mashambulizi haya. Kinacholeta ugumu ni kupata maneno yasiyo na ukakasi. Jekejeke litatokea endapo makampuni mengine yatakuja na misemo hii: CHOMEKA UCHOMEKWE, TIA UTIWE, WEKA UWEKWE, NYONYA UNYONYWE, GEUZA UGEUZWE, LAINISHA ULAINISHWE na mengine mengi y...

RIWAYA| SAFARI YA KUUSAKA MWEZI (sehemu ya 10)

Image
“Jitambulisheni nyie ni akina nani? Sivyo tunawachoma moto.” Alisema mmoja wao aliyeonekana kuwa kiongozi.           “Tumekuja kwa amani,” nilijibu, “sisi ni wanadamu toka sayari ya Dunia, tupelekeni kwa mfalme wenu tuna mazungumzo.”           “Ha! ha! ha! mmeufuata mwezi wenu, hampati kitu, na mkileta habari za kudai mwezi mtarudi bila roho zenu.” Kilijibu kijitu kichafu, nilipokitazama usoni nikagundua ni kilekile kilichoiba mwezi wetu na kuuweka mfukoni, nilistaajabu umbile dogo la kiumbe yule liliwezaje kuubeba mwezi tena kwa kuutia mfukoni! Baada ya mazungumzo walikubali kutupeleka kwa mfalme wao. Walitutaka twende kwa mwendo pole ili tufike asubuhi maana usiku ule mfalme alilala na haikupaswa kumsumbua. Chombo kilitembea taratibu tukiwa tumewekwa katikati ya vile vijitu, hatukuruhusiwa kuongea wala kukohoa. Kwa muda wote huu, msichana Minza hakuonesha dalili yoyote ya kuchoka w...

VICHEKESHO VILIVYOTUFIKIA WIKI HII

Image
😏😏😏😏😏   *YAAN WADADA WA SIKU HIZI BHANA, UNAKUTA YUKO BAFUNI ANAOGA HALAFU NYWELE KAZIACHA CHUMBANI..*. πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚   πŸƒπŸ½πŸƒ XXX  *mzee kanitumia sms "njoo upike ugali mboga tayari" kwa haraka haraka zangu nikajibu OWA badala ya POA*  *saiz nipo nyumbani hapo naona mabegi yangu ya nguo yote yapo nje itakuwa mzee anafanya usafi ndani...* XXX  *_BANK bhana wapuuzi kweli sie tunaweka mamilion yetu tunawaamini ... lakini wao pen ya sh.100 wanaifunga kamba inamaana hawatuamini πŸ˜πŸ˜πŸ˜€πŸ˜ŠπŸ˜†πŸ˜†πŸ˜œ _* XXX  *Maisha Bhana!! Yani We Ukivuta Subira Kuna Mwingine Anavuta Bangi* XXX  I started fearing smoking weed,when I saw my neighbour's son dancing to the sound of my generator. ..When I switched it off he asked me who sang that song ? Because I was afraid he would beat me , I answered " Yamaha featuring Petrol" πŸ˜‚πŸ˜œπŸ˜œ XXX  MKE;(kachukua simu akaanza kuongea kwa hasira),mume wangu uko wapi mpaka mida hii saa 4 za usiku? MUME;Mke ...

PROFESA MUHONGO ANAVYOTESWA NA NAMBA 24

Image
January 24, 2015, Profesa huyu mwenye bahati mbaya, alijiuzuru wazifa wake kutokana na sakata la Tegeta Escrow. May 24, 2017, Muhongo analeta utata. Kwanza naiona barua ya Mheshimiwa Rais ikisema kuwa, uteuzi wake umetenguliwa ama kama wasemavyo watoto wa mjini, barua ile ilibeba tamko la kumtumbua mzito huyu. Lakini baadaye naiona barua ya Profesa Muhongo mwenyewe akitangaza kujiuzuru huku akiwa tayari amekwisha tumbuliwa! Kama sikuchanganya mambo, basi hii ni ajabu. (KICHEKO). Cha kushangaza ni kwamba katika mara zote alizoondoka madarakani kwa zahama, aliondoka tarehe 24. Kuna nini katika hii tarehe 24? Kwa imani aliyonayo Muhongo, namba 24 ina maana kubwa. Namba hii ina uhusiano na masuala ya kumtumikia Mungu hususani katika hekalu. Hivyo rafiki yangu Profesa huyu achague kilinge chochote kinachomfaa katika shughuli za utumishi wa Bwana, kama ataamua kulihubiri neno kwa imani ya Kirastafari, Budha, Hindu, Dini ya Afrika ya Jadi n.k, basi afanye hima kabla hajachelewa. Kwa w...

VICHEKESHO VILIVYOTUFIKIA WIKI HII

Leo tupo kwenye Taxi tunaelekea Mjini Traffic akasimamisha gari letu, akamuuliza Dereva "Mbona plate namba za nyuma na mbele ni tofauti !?. Dereva akamjibu, 'Kwani ww sura yako na makalio yako vinafanana !?. Wote tukaanza kucheka ... Tumepandishwa kwy defender lao nadhani wanatupeleka kupata lunch ! πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ XXX πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€’ IVI KWA MFANO MKEO AKIWA NA KICHWA KIKUBWA KULIKO WW BADO TU UTAITWA KICHWA CHA FAMILIA? 🀣🀣🀣🀣🀣 XXX ......... Jaman Hivi hakuna Mtu yeyote Mwenye *Picha* ya *WAHENGA*   Anitumie Mimi Nawaskiaga Tu Cjawahi kuwaona    πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ XXX   Ile siku nitaona mwanamke akiskuma mkokoteni bila shati.....ndio nitaamini kuwa #what_a_man_can_do_a_woman_can_do_better πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ Wacha niende hivi narudi baadae πŸƒπŸΌπŸƒπŸΌπŸƒπŸΌπŸƒπŸΌ XXX   Mdada:- beby nimefukuzwa kwetu Jamaa:- maskini pole Mdada:- Hapa Hata sijui ntafanyeje Jamaa:- panda Gari za mbagala zinazopitia Tazara ulale kwenye FoleniπŸƒπŸΎπŸƒπŸΎ XXX ...

BONDIA MSOMI KUTOKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM, ASEMA YUKO TAYARI KWA PAMBANO

Image
Goodluck Elisaria, bondia machachari wa uzito wa 'featherweight', mwanafunzi wa mwaka wa tatu kutoka ndaki ya COHU anayekiwakilisha Chuo Kikuu Cha Dar es salaam katika ulimwengu wa ngumi, sasa amethibitisha rasmi kupanda tena ulingoni kukipiga na mpinzani wake Vasco Maklin. Maamuzi haya yanakuja baada ya Saria kupona jeraha lake alilolipata siku ya tarehe 07/05 mara baada ya kutokea ajali ya kugongana vichwa akiwa ulingoni hali iliyopelekea pambano hilo lihesabike kama suruhu 'technical draw'. Bondia huyu ambaye hajawahi kupigwa, kule Congo alifanya mambo makubwa wakampa jina la 'SariaMundende'. Hapa Tanzania tunamwita  'SariaZege'. "Nitampiga Maklin katika raundi ya kwanza, kisha nitakwenda chuo kufanya test nikiwa ninatabasamu kwa ushindi!" Alisema SariaZege.  KILA LA KHERI SARIA. WAPIGE!!

VICHEKESHO VILIVYOTUFIKIA WIKI HII

*Upo ugenini unasikia "HUMU NDANI HATUJAWAHI KUPOTELEWA NA KITU"* πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€” XXX *Leo kuna mtu nimemtolea uvivu ! amenikuta nimetulia akaniuliza mbona nimekunja sura ...nikamwambia nataka kuiweka kwenye bag.* Sipendangi ujinga mimi πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ XXX *_Dogo kampigia simu baba yake:_* *_DOGO:_*_Baba katika zile shilingi laki mbili ulizonipa nikalipe ada nmetumia shilingi elfu 30 kubeti._ *_BABA:_*_Unasema nini we mpumbavu mshenzi mkubwa? Nimekukanya mara ngapi kuhusu kubeti._ *_DOGO:_*_Lakini baba......!_ *_BABA:_*_Lakini baba nini ngoja urudi utaona ntakachokufanya._ *_DOGO:_*_Nilitaka kukwambia kuwa nmeshinda shilingi milioni 3._ *_BABA:_*_Ndio hayo ninayosema wewe ni mpumbavu sana kwanini hukutumia laki nzima kubeti? Si ungepata pesa nyingi zaidi? Ngoja urudi niwataarifu ndugu zako jinsi ulivyo na akili za kuamua haraka mwanangu kipenzi_ XXX *Jana nlienda kununua parachichi la mia tano nkaomba mfuko,mama ayubu akaniambia hatoagi mfuk...