Uhakiki wa Tamthiliya ya Usaliti Mjini
Wasiliana na Mwalimu ili Kujiunga Darasa la Uhakiki wa Vitabu vyote vya Fasihi Mtaala Mpya kwa Kugusa Hapa Mwandishi: Francis Imbuga Mwaka: 1976 Mhakiki: Mwalimu Makoba Simulizi kwa Ufupi Tamthiliya hii inahusu harakati za wanajamii kupigania haki ikiwamo kupambana na uongozi mbaya uliokithiri. Wanafunzi wanafanya maandamano kupinga uongozi mbaya, katika maandamano hayo wanafunzi wengi wanauawa, miongoni mwao ni Adika. Adika ana ndugu yake anayebaki hai, naye anaitwa Jaspa Wendo, mwanafunzi wa chuo kikuu. Mauaji haya yanafanyika kwa sababu ya uongozi mbaya wa Bosi, kiongozi wa Kafira. Bosi ambaye ndiye kiongozi mkuu, anashauriwa na binamu yake aitwaye Mulili. Uongozi wote mbaya, mshauri mkuu ni Mlili. Mwisho tunaona igizo likiandaliwa ili kutoa burudani. Waigizaji wanachaguliwa, miongoni mwao ni Jaspa Wendo. Mwingine ni Mosese, mhadhiri wa chuo kikuu aliyefungwa kwa kupinga maovu ya serikali. Katika igizo hilo, mwigizaji mmoja hakutokea, Bosi anachukua nafasi yake. Wanapopand...