Uhakiki wa Diwani ya Malenga Wapya
Mwandishi: Taasisi ya Kiswahili, Zanzibar Wachapishaji: Oxford University Press MWAKA: 2001 Mhakiki: Mwalimu Makoba Kuhusu Malenga Wapya Malenga wapya ni diwani ambayo inaangazia yale yanayotokea katika jamii. Inaangazia mambo mbalimbali yanayohusu siasa, mapenzi , uchumi, jamii na mengine mengi. Maudhui Vipengele mbalimbali vya maudhui vinajadiliwa, miongoni mwavyo ni: Dhamira Malenga hawa wapya wanaibua dhamira mbalimbali kama zinavyojadiliwa: Uongozi mbaya Katika shairi la PAYUKA, mshairi anasema, “Kupayuka kwenu huko, Mbona tu kokoriko, Sioni linalokuwa.” Mshairi analalamika waziwazi juu ya uongozi mbaya. Viongozi kazi yao ni kupayuka majukwaani, lakini wanapokuw...