Uhakiki wa Riwaya ya Ua la Faraja
Wasiliana na Mwalimu ili Kujiunga Darasa la Uhakiki wa Vitabu vyote vya Fasihi Mtaala Mpya kwa Kugusa Hapa Mwandishi: W.E. Mkufya Mwaka: 2004 Mhakiki: Mwalimu Makoba Utangulizi Profesa Madumla akiizungumzia riwaya ya Ua la Faraja alisikika akisema, “Mkufya anajua kuitumia lugha ya Kiswahili vilivyo… ni fundi wa ujenzi wa taharuki.” Huwa sipendi kubishana na Profesa Madumla, lakini katika hili alidanganya. Haifahamiki kwa nini Madumla alidanganya, ila moja kati ya hoja hizi huenda ikawa kweli: pengine hakukisoma kitabu , na kama alikisoma, huenda kuna manufaa fulani aliyapata, kama hakuna kabisa manufaa yoyote, basi Madumla uzee umeanza kumwingia! Mkufya ni Mwanasayansi aliyeivamia sanaa, sanaa ikamgaragaza vilivyo, Ua la Faraja ni Riwaya ndefu kama andiko la tafiti za Kisayansi, ina kurasa 423! Ni kama riwaya yake mwenyewe ilikuwa ikimdhihaki na kumweleza, “Sanaa ina wenyewe!” Riwaya hii imekosa ujenzi wa taharuki, kila tukio linalofuata linatabirika na matukio mengine wala hayakupasw...