Posts

Maswali 100 Kujiandaa na Usaili Tume ya Utumishi wa Mahakama

Image
Vijana wenye sifa mbalimbali huitwa katika Usaili wa Tume ya Utumishi wa Mahakama kila mwaka. Wote hawa wanasumbuliwa na swali moja, maswali ya usaili wa mchujo Tume ya Utumishi wa Mahakama yanatokaje? Kabla hujajibu swali la kwanza, linaibuka swali la pili, maswali haya yanatoka kwa lugha gani? Swali la pili ni jepesi kuliko swali la kwanza. Maswali yanaweza kutoka katika lugha yoyote kati ya Kiswahili au Kiingereza. Hata hivyo, unapojiandaa, ni vyema kutumia lugha ya Kiingereza. Swali la kwanza halina jibu moja. Maswali ya Tume ya Utumishi wa Mahakama yanatoka katika maeneo mengi na hubadilika mara kwa mara! Hata hivyo, tumekubaliana kwamba, maswali mengi huulizwa kuhusu: Uelewa wa mambo mbalimbali yanayotokea katika jamii. Mambo haya ni mambo yanayomhusu kila Mtanzania. Unaweza kuulizwa swali linalohusu mazingira yako na shughuli za kila siku. Maswali kuhusu taaluma yako. Upo uwezekano wa kukutana na baadhi ya maswali ambayo yanahusu taaluma uliyosomea. Mtindo huu haupendelewi san...

Uhakiki wa Riwaya ya Ua la Faraja

Image
Wasiliana na Mwalimu ili Kujiunga Darasa la Uhakiki wa Vitabu vyote vya Fasihi Mtaala Mpya kwa Kugusa Hapa Mwandishi: W.E. Mkufya Mwaka: 2004 Mhakiki: Mwalimu Makoba Utangulizi Profesa Madumla akiizungumzia riwaya ya Ua la Faraja alisikika akisema, “Mkufya anajua kuitumia lugha ya Kiswahili vilivyo… ni fundi wa ujenzi wa taharuki.” Huwa sipendi kubishana na Profesa Madumla, lakini katika hili alidanganya. Haifahamiki kwa nini Madumla alidanganya, ila moja kati ya hoja hizi huenda ikawa kweli: pengine hakukisoma kitabu , na kama alikisoma, huenda kuna manufaa fulani aliyapata, kama hakuna kabisa manufaa yoyote, basi Madumla uzee umeanza kumwingia! Mkufya ni Mwanasayansi aliyeivamia sanaa, sanaa ikamgaragaza vilivyo, Ua la Faraja ni Riwaya ndefu kama andiko la tafiti za Kisayansi, ina kurasa 423! Ni kama riwaya yake mwenyewe ilikuwa ikimdhihaki na kumweleza, “Sanaa ina wenyewe!” Riwaya hii imekosa ujenzi wa taharuki, kila tukio linalofuata linatabirika na matukio mengine wala hayakupasw...