Ufahamu na Ufupisho | Kiswahili Kidato cha Tano na Sita

Ufahamu ni kujua au kulielewa jambo hatimaye kuweza kulifafanua. Mtu anaweza akaona, akasoma, ama akasikia jambo na akaelewa au asielewe. Akielewa atakuwa na uwezo wa kufafanua au kutoa taarifa zinazohusiana na habari hiyo. Ufahamu wa kusikiliza na ufupisho Ufahamu wa kusikiliza ni ule ambao mhusika anapata taarifa hiyo kwa kusikiliza habari hiyo. inawezekana kupata habari hiyo kwa kusimuliwa au kusomewa. Ili kupata habari inayosikilizwa au inayosomwa, msikilizaji azingatie mambo haya: - Kuwa makini kwa kila kinachosimuliwa au kinachosomwa. - Kuhusisha mambo muhimu na habari isimuliwavyo. - Kujua matamshi ya mzungumzaji. - Kubainisha mawazo makuu. Kujibu maswali kutokana na habari uliyoisikiliza Mbinu za kujibu maswali kutokana na habari ya ufahamu wa kusikiliza ni: - Kusikiliza kila swali kwa makini. - Kutafakari kila swali, yaani kutafuta maana ya swali kwa kulihusisha na matini aliyosimuliwa. - Kujibu kila swali kwa