Mtihani wa Kiswahili 2 Kidato cha Sita 2024 NECTA Majibu

Muda: Saa 3 Sehemu A (Alama 40) Jibu maswali yote katika sehemu hii. 1. Wasanii huongozwa na mbinu mbalimbali katika kutunga kazi za fasihi simulizi. Onesha mbinu zinazotumiwa na wasanii katika kutunga igizo kisha tunga igizo fupi linalohusu madhara ya ukeketaji. Taratibu za kutunga maigizo - Kuchagua tukio la kuigizwa Tukio hilo, liwe na mchango chanya katika jamii , ikiwemo kuelimisha. - Kuchagua mahali pa kutendeka kwa jambo Mahali panaweza kuwa: ofisini, shuleni, kijijini barabarani n.k - Kuamua mtindo wa kuwasilisha jambo la kuigizwa Hapa mwandishi anaweza kutumia fumbo, vichekesho n.k - Kupanga hoja kuu zinazojenga maudhui ya igizo Maudhui hujikita katika migogoro au mivutano. Masuluhisho ya migogoro yanatakiwa kupatikana. Mfano, jambazi kuu hukamatwa mwisho wa igizo. - Kuweka mpangilio wa maonyesho Mtunzi atumie mpangilio mzuri ambao utasaidia wasomaji waweze kuelewa kazi yake. - Kubuni wahusika Mwandishi anashauriwa kubuni wahusika wenye sifa tofauti: wanene, weupe, weusi...