Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi Jeshi la Wananchi JWTZ
Jeshi la wananchi Tanzania limetangaza nafasi za kuandikishwa na jeshi hilo kwa vijana wenye baadhi ya sifa hizi: raia wa Tanzania, umri kuanzia miaka 18 mpaka 25 kwa kidato cha nne na sita na miaka isiyozidi 28 kwa wanaotoka vyuoni au elimu ya juu na awe na cheti cha jeshi la kujenga taifa kilichopatikana kwa kujitolea au kwa mujibu wa sheria. kuandika barua inayokubalika , kutakufanya uitwe katika usaili huu wa nafasi hizi ambazo zina waombaji wengi. Unapotuma maombi, anza na barua yako, Weka nakala ya kitambulisho chako cha NIDA ikifuatiwa na nakala ya cheti cha kuzaliwa, na vyeti vya shule, nakala ya cheti cha JKT, karatasi moja iliyoandikwa namba yako ya simu, kichwa cha habari kiwe, NAMBA YA SIMU YA MKONONI, halafu nenda posta kayatume maombi hayo katika anuani yao iliyoandikwa hapo kwenye mfano wa barua ya maombi JWTZ. Huu hapa mfano wa barua ya kuomba kuandikishwa katika Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ): Mtaa wa Kambangwa, S.L.P 1248, KINONDONI, DAR ES SALAAM. 1...