Mfano wa Barua ya Maombi ya Kazi TAKUKURU Ajira Mpya
TAKUKURU wametangaza nafasi za kazi kwa vijana wenye sifa mbalimbali. Nafasi mpya za kazi zilizotangawa na TAKUKURU zinayahusu makundi mawili: Kundi la kwanza, Muombaji awe na angalau elimu ya shahada ya kwanza iliyotolewa na chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika moja ya fani zifuatazo: Uhasibu, Usanifu Majengo, Usimamizi wa Biashara, Usanifu wa Majengo, Ukadiriji wa Majengo (Quantity Surveying), Uhandisi wa Usindikaji wa Kemikali, Maendeleo ya Jamii, Sayansi ya Kompyuta/TEHAMA, Uhandisi wa Ujenzi, Uchumi na Mipango, Uhandisi wa Umeme. Lishe na Sayansi ya Chakula, Usimamizi wa Rasilimali Watu, Usimamizi na Tathmini ya Ardhi, Sheria, Uhandisi wa Mitambo, Uhandisi wa Mafuta na Gesi, Ununuzi na Ugavi, Usimamizi wa Miradi, Ushauri Nasaha, Utawala wa Umma, Mahusiano ya Umma/Mawasiliano ya Umma, Usimamizi wa Kumbukumbu, Sayansi ya Michezo/Elimu ya Viungo, Takwimu, na Uhandisi wa Maji. Kundi la pili: ulinzi, ufundi wa magari, ujuzi wa udereva, h...