SMS 20 za Vichekesho Zinazochekesha Sana
Tumekukusanyia mkusanyiko wa vichekesho vinavyochekesha sana. Vichekesho hivi, vitakufanya ufurahi muda wote, ni vizuri zaidi, uki’share’ na wenzako. 1. Huu mwezi mwenye nyumba aje atoe nyumba yake kwenye vitu vyangu, sina kodi. 2. Nimetoa vyombo nje nifanye usafi, kurudi naambiwa gari la taka limebeba. 3. Kwa jinsi maisha yalivyo magumu siku hizi unajikuta wewe ndiyo unamuamsha jogoo. 4. Chakula chenyewe unakipata kwa mateso halafu bado unakiwekea pilipili, una tatizo gani mkuu? 5. Mtu anakuja kuniomba elfu 20 kweli! Unaniombaje nusu ya utajiri wangu? 6. Daktari: Bia inatanua moyo. Walevi: imeshindwa kutanua chupa itatanua moyo? 7. Nimeota nakula tambi, kuamka sizioni "earphone" zangu. 8. Taja faida kwa nini unaishi peke yako. Hakuna wa kuniuliza kwa nini pazia nafutia sahani. 9. Leo mwizi kapigwa mpaka kasema, "mawe yanauma, nipigeni makofi.” 10. Hasira mnatoa wapi wakuu, fikiria mtu anaua kipepeo. 11. Bongo movie imen...