Vichekesho 10 Vinavyochekesha Mpaka Mbavu Ziume

Kama unataka kuwa mwenye afya bora, basi hakikisha unacheka , siku inayopita ikiwa na vicheko ndani yake ni siku bora mno.Kucheka ni jambo muhimu katika maisha. Kucheka huongeza kinga katika mwili wako, husaidia mwili kutoa homoni ya furaha aina ya ‘endorphins’, kucheka hulinda moyo, husaidia katika mmeng’enyo wa chakula, hupunguza hasira na kucheka kunaweza kuongeza hata siku zako za kuishi. Leo tunakuletea vichekesho 10, ambavyo ni lazima vikufanye ucheke, ufurahi na uwe mwenye afya bora. 1. Nilikuwa na mjomba yangu, yeye alikuwa akiniambia nisiogope kitu kwa sababu ni askari . Siku moja nilikamatwa, nikampigia simu kumuita, alipofika, nikamwambia awaambie askari wenzake waniachie. Mjomba akanijibu kwa sauti ya upole, “Mjomba sina uwezo, mimi siyo askari polisi, mimi ni askari wa jeshi la wokovu kanisani kwetu, labda nikufanyie maombi.” 2. Mlio kwenye mahusiano, mkiambiwa ‘take care’ na wapenzi wenu huwa mnajibuje? Msaada tafadhali. 3. Nimeshuhudia mjomba akianguka k...