Posts

Uhakiki wa Wimbo Nipeni Maua Yangu wa Roma Mkatoliki

Image
Roma Mkatoliki  ni mwanamuziki machachari anayefanya mziki wa kufokafoka  maarufu kama ‘Hiphop.’ kibao cha Mr President  kilimtambulisha vyema. Katika wimbo huo, msanii huyu anamsema waziwazi rais kuwa kashindwa kutimiza ahadi yake ya maisha bora kwa kila Mtanzania. Baada ya kibao hicho, alijipatia umaarufu mkubwa na alitoa vibao vingine vikali na kama kawaida aliendelea kusema mambo mazito bila kificho. Roma Mkatoliki hakuishia kuwasema wanasiasa tu, aliwasema hata wachungaji katika wimbo wake wa Pastor . Roma siyo malaika, kuna wakati anakosea. Katika wimbo uitwao Tanzania  anasikika akisema, “Kimbilio la waliofeli ni ualimu na upolisi” (Roma, 2008). Hapo msanii alikosea pengine ni kwa kukosa taarifa muhimu juu ya sekta nyeti ya ualimu na ile ya upolisi. Kuna hatari ya kubeba kila kinachosemwa na watu na kukitangaza zaidi na Roma hajaiepuka hatari hii. Mwalimu Julius Nyerere  aliyeleta uhuru wa Tanzania hakufeli, Mwalimu Mahatma Gandhi aliyewapatia uhuru India hakufeli, Mwalimu Nelso

Uhusiano wa Dhana ya Masharti Ukweli na Dhana ya Uchopezi

Image
Swali Masharti ukweli ina uhusiano wa karibu na dhana ya uchopezi. Jadili dai hili kwa mifano Dhahiri ya sentensi za Kiswahili. Resani (2014) anadai kuwa kanuni ya masharti ukweli (ameitaja kama kanuni ya sifa ya thamani ya ukweli) ni yale ambayo unafahamu siyo ya kweli. Akifafanua zaidi kuhusu kanuni ya thamani ya ukweli, mwandishi anasema: Usiseme yale ambayo unafahamu siyo ya kweli. Pili usiseme yale ambayo huna ithibati nayo au uhakika wa kutosha. Mfano kama wewe si msemaji wa umoja au kikundi fulani usiseme mambo yanayokihusu kikundi hicho kwenye midia au kwa wanahabari. (Resani, 2014:77) Tunaweza kusema kwamba Nadharia ya masharti ukweli husisitiza dhana ya ukweli katika ujasiri wa maana, hivi kwamba maana sharti iwe ya kweli na ukweli huo ubainishwe bayana. Nadharia hii iliasisiwa na wanamantiki na wanafalsafa, kisha ikafafanuliwa na wanaisimu. Mfano (a) Ukweli wa kihistoria i/ Tanganyika ilipata uhuru wake mwaka 1961. ii/ Rais wa kwanza wa Tanzania kufa akiwa madarakani

Mawasiliano | Kiswahili Kidato cha Kwanza

Image
Mawasiliano ni kitendo cha kupashana habari. Inaweza kuwa kwa mdomo baina ya mtu na mtu, simu, barua au njia yoyote itakayosaidia kutoa habari sehemu fulani kuipeleka mahali pengine. Tunasema mawasiliano yamekamilika pale yanapoleta maana iliyokusudiwa. Jamii inayoishi watu, huwasiliana. Chombo kinachotumiwa kwa mawasiliano baina ya mtu na mtu kinaitwa lugha. Lugha ni mfumo wa sauti za nasibu zilizokubaliwa na watu ili zitumike kwa mawasiliano. Lugha hujumuisha: sauti, silabi, neno na sentensi. Unapowasiliana kwa kutumia lugha ya Kiswahili ni muhimu kuzingatia: kiimbo, mkazo, matamshi na lafudhi sahihi. Dhima ya lugha katika mawasiliano 1. Kupashana habari Watu hupashana habari mbalimbali kwa kutumia lugha. Habari za furaha na huzuni zote hutolewa kwa kutumia lugha. Taarifa ya habari katika redio na runinga ni mfano wa namna lugha inavyotumika kama chombo cha kupashana habari. 2. Kutambulisha mtumiaji wa lugha Kwa kusikia watu wakiwa wanazungumza, tunapata kuwafahamu watu hao ni wa ja

Vitu Vinavyokuibia Muda Wako na kufanya Kazi Zisikamilike

Image
Matumizi sahihi ya muda yatakufanya upate amani mahali pa kazi, uongeze ufanisi na uzalishaji. Hata hivyo, vipo vitu ambavyo vinakuibia muda wako na kukufanya uone siku haitoshi ilhali saa ni nyingi. Unapenda kuvifahamu vitu vinavyokuibia muda wako? Soma taratibu. 1.  Simu Simu ni mwizi wa kwanza wa muda. Wakati wa kazi, unaweza kupigiwa simu ukapokea na kuongea kwa zaidi ya dakika ishirini. Utajibu meseji kadhaa, utaingia katika mitandao ya kijamii kutazama habari mbalimbali, ukija kukaa sawa ili ukamilishe kazi, muda umekwisha! 2.  Kelele Wapo watu wanaofanya kazi katika mazingira yenye kelele nyingi. Kelele hupunguza ufanisi kwani mtu hushindwa kufikiri haraka ili kukamilisha jambo. Fikiria mtu anayefanya kazi katika mazingira ya kelele, anaamua kutafuta sehemu yenye utulivu ili atume au asikilize taarifa fulani muhimu, hatua zote hizi zinapoteza muda. 3.  Vikao Vikao vya ofisi navyo ni sehemu ya wezi wa muda. Vikao vingi huwa havina jambo la maana zaidi ya kukumbushana mambo yaley

English Language Examination Form Four 2022 1

Image
Instructions 1. This paper consist of sections A, B and C with a total of twelve questions. 2. Answer all questions in section A and B and three questions from section C. 3. Section A carries fifteen marks, section B forty marks and section C carries forty five marks. 4. Cellular phones and any unauthorized materials are not allowed in the examination room. 5. Write your examination number on every page of your answer booklet(s). Section A (15 Marks) Answer all questions in this section. 1. For each of the items (i) to (x), choose the most correct answer from among the given alternatives and write its letter beside the item number in the answer booklets(s) provided. i. What type is this conditional sentence, “If he calls me, I will answer.” A. Conditional sentence type two B. Conditional sentence type three C. Conditional sentence type one D. Conditional sentence type four E. Conditional sentence type five ii. What is the question tag of this statement, “She was my friend”? A. wasn’t s