Mtihani wa Kiswahili Kidato cha Nne 2023 1

Muda: Saa 3 Maelekezo 1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali 12. 2. Jibu maswali yote katika sehemu A na B na maswali matatu kutoka sehemu C. 3. Sehemu A in alama 15, sehemu B ina alama 40 na sehemu C ina alama 45. 4. Zingatia maelekezo ya kila sehemu na ya kila swali. 5. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihani. 6. Andika namba yako ya mtihani katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia. Sehemu A (Alama 15) Jibu maswali yote katika sehemu hii. 1. Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele (i) hadi (x), kisha andika herufi ya jibu hilo kwenye kijitabu chako cha kujibia. (i) “Kushindana na mtu aliyekuzidi kwa kila hali si busara.” Methali zifuatazo zinashabihisha kauli hii isipokuwa: A Mwenye pesa si mwenzio B Nazi haishindani na jiwe C Chanda chema, huvikwa pete D mwenye nguvu mpishe E Maji yakija kasi yapishe (ii) Bainisha sentensi yenye vielezi zaidi ya kimoja katika sentensi zifuatazo: A vitabu vyangu