Maswali 100 ya Kujiandaa na Usaili Walimu Somo la Kiswahili
Katika mitihani ya usaili walimu , maswali haya ni msaada mkubwa. Kwa kuwa muda wa kusoma kila kitu hautoshi, maswali haya hutumika kama njia nzuri zaidi inayomfanya mwalimu apate kila kitu kwa muda mfupi na kumsaidia awe ‘selected’ kwenda ‘oral interview’ katika mitihani hii yenye ushindani mwingi. 1. Katika kompyuta, ukibonyeza alama ctr+A unapata nini? A. Unafuta maandishi yote yaliyochaguliwa. B. Unachagua (highlight) maandishi au mafaili yote. C. Unahifadhi (save) kazi uliyokuwa unafanya. D. Unafungua faili jipya la kazi. Jibu: B 2. Juma amewasha kompyuta yake, lakini anagundua kwamba, kila akicheza mziki, sauti haisikiki, afanye nini kama suluhisho? A. Kununua spika mpya za kisasa zaidi. B. Kufuta nyimbo zote na kuziweka upya. C. Kukagua kama sauti imewekwa "Mute" au kama kadi ya sauti ina hitilafu. D. Kuzima kompyuta na kutofanya kazi yoyote. Jibu: C 3. Program ya akili mnemba inayohusika na utengenezaji wa picha inayomilikiwa na kampuni ya google inaitwaj...