Uhakiki wa Wimbo Nipeni Maua Yangu wa Roma Mkatoliki

Roma Mkatoliki ni mwanamuziki machachari anayefanya mziki wa kufokafoka maarufu kama ‘Hiphop.’ kibao cha Mr President kilimtambulisha vyema. Katika wimbo huo, msanii huyu anamsema waziwazi rais kuwa kashindwa kutimiza ahadi yake ya maisha bora kwa kila Mtanzania. Baada ya kibao hicho, alijipatia umaarufu mkubwa na alitoa vibao vingine vikali na kama kawaida aliendelea kusema mambo mazito bila kificho. Roma Mkatoliki hakuishia kuwasema wanasiasa tu, aliwasema hata wachungaji katika wimbo wake wa Pastor . Roma siyo malaika, kuna wakati anakosea. Katika wimbo uitwao Tanzania anasikika akisema, “Kimbilio la waliofeli ni ualimu na upolisi” (Roma, 2008). Hapo msanii alikosea pengine ni kwa kukosa taarifa muhimu juu ya sekta nyeti ya ualimu na ile ya upolisi. Kuna hatari ya kubeba kila kinachosemwa na watu na kukitangaza zaidi na Roma hajaiepuka hatari hii. Mwalimu Julius Nyerere aliyeleta uhuru wa Tanzania hakufeli, Mwalimu Mahatma Gandhi aliyewapatia uhuru India hakufeli, Mwalimu Nelso