Posts

Showing posts with the label sekondarinavyuo

Jinsi ya Kuandika Tangazo| O level na Advance

Image
Matangazo ya gazetini huandikwa kwa lengo la kutangaza biashara. Kwa kuwa magazeti yana wasomaji lukuki, hivyo njia hii hudhaniwa kuwa miongoni mwa njia rahisi zaidi za kuwafikia watu wengi ambao hapo baadaye hugeuka wanunuzi wa bidhaa inayotangazwa. Uandishi mzuri zaidi wa matangazo ndiyo utakaofanya bidhaa yako inunuliwe. Uandishi mbovu hugeuka kero kwa watu. Mambo Muhimu ya Kuzingatia 1.    Kichwa cha habari. Kiandikwe kwa herufi kubwa. 2.    Taja aina ya biashara. 3.    Taja bidhaa unazouza na bei zake. 4.    Taja mahali inapopatikana bidhaa yako. 5.    Taja mawasiliano yako. Mawasiliano yanaweza kuwa ya simu, barua n.k. hata hivyo, simu ni  bora zaidi,  kwa sababu mawasiliano yake ni ya haraka. Mfano wa Kwanza MASOMO KWA WANAFUNZI WOTE Kituo cha Mwalimu Makoba kinatoa huduma ya kufundisha wanafunzi wanaorudia mitihani na walio shuleni kwa masomo ya sayansi, sanaa na biashara. Gharama zetu ni shil...

Uhakiki wa Riwaya ya Usiku Utakapokwisha

Image
RIWAYA: USIKU UTAKAPOKWISHA MWANDISHI: MBUNDA MSOKILE MWAKA: 1990 WACHAPISHAJI: DUP MHAKIKI: DAUD MAKOBA (MWALIMU MAKOBA) Utangulizi Usiku Utakapokwisha ni riwaya inayojadili matatizo mbalimbali yanayoikumba jamii ya Mtanzania. Ukosefu wa ajira unafanya vijana watatu, Chioko, Gonza na Nelli wasifikie ndoto zao za mafanikio. Kitabu hiki japo kinajadili mambo kadha wa kadha, lakini kimejikita sana katika matatizo ya kiuchumi. Maudhui Dhamira Rushwa Viongozi wako msitari wa mbele katika kutoa na kupokea rushwa. Chioko anashindwa kupata ajira kwa sababu hakuwa na rushwa. Umasikini Familia nyingi zinaishi katika lindi zito la umasikini. Mwandishi anaonyesha jinsi ambavyo umasikini umelitawala tabaka la chini. kwa mfano, familia moja inakufa Buguruni kwa kukosa chakula. Mapenzi Mwandishi amejadili mapenzi ya kweli na mapenzi ya uongo. Mapenzi ya kweli yameonekana kwa Chioko. Kijana huyu anampenda kwa dhati mpenzi wake Nelli. Hata anaposhauliwa na rafiki ...