JAZA UJAZWE! UPEMBA MWINGI NA TAFSIRI ZA KIMOMBASA

picha ikionyesha watu wakipiga soga 'chat'
Lugha ya Kiswahili ina maneno lukuki ambayo kama hutakuwa makini katika uchaguzi utaibua sintafahamu na mishangao kwa watu! Hata kabla ya ‘jaza ujazwe,’ neno ‘tigo’ peke yake lina maana nyingine mbali na maana yake!
Ama hakika, muhusika wa kitengo cha matangazo kutoka kampuni ya ‘tigo’ atakuwa amefanikiwa sana kuitangaza biashara na ofa hii mpya ya kampuni yake. Lakini mbali na faida hiyo, kuna ukakasi mkubwa ambao umetanda miongoni mwa watu hasa wanaotambaa na maana ya ziada. Wengi hususani wanaume, wanaona neno hili si zuri kutumika na linawadharirisha.
Makampuni ya simu yamekuwa na tabia ya kuigana kila inapotokea kampuni mojawapo ikaja na ubunifu wa kuvutia. Lakini katika hili makampuni pinzani bado yako kimya, hakuna aliyejibu mashambulizi haya. Kinacholeta ugumu ni kupata maneno yasiyo na ukakasi. Jekejeke litatokea endapo makampuni mengine yatakuja na misemo hii: CHOMEKA UCHOMEKWE, TIA UTIWE, WEKA UWEKWE, NYONYA UNYONYWE, GEUZA UGEUZWE, LAINISHA ULAINISHWE na mengine mengi ya aina hiyo.
Ukiangalia kwa undani maneno haya hayana maana mbaya, ila kwa kuwa maana katika lugha huwa ni zaidi ya ile maana ya msingi, ukakasi kama huu ni lazima kutokea.
Lugha kuwa na utata na kuibua maana nyingi ni kiashiria kwamba imekua. Hili ni pigo kwa wanaodhani bado tunapaswa kuendelea kufundisha maarifa kwa lugha ya kiingereza. Kwa miaka dahari na dahari, kiswahili kimekuwa na msamiati wa kutosha. Nafunga pazia hapa, kama umependa waraka huu wa dharura, basi MINYA UMINYWE!

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne