PROFESA MUHONGO ANAVYOTESWA NA NAMBA 24

Prefesa Muhongo akiwa kakaa bungeni.
January 24, 2015, Profesa huyu mwenye bahati mbaya, alijiuzuru wazifa wake kutokana na sakata la Tegeta Escrow.
May 24, 2017, Muhongo analeta utata. Kwanza naiona barua ya Mheshimiwa Rais ikisema kuwa, uteuzi wake umetenguliwa ama kama wasemavyo watoto wa mjini, barua ile ilibeba tamko la kumtumbua mzito huyu. Lakini baadaye naiona barua ya Profesa Muhongo mwenyewe akitangaza kujiuzuru huku akiwa tayari amekwisha tumbuliwa! Kama sikuchanganya mambo, basi hii ni ajabu. (KICHEKO).
Cha kushangaza ni kwamba katika mara zote alizoondoka madarakani kwa zahama, aliondoka tarehe 24. Kuna nini katika hii tarehe 24?
Kwa imani aliyonayo Muhongo, namba 24 ina maana kubwa. Namba hii ina uhusiano na masuala ya kumtumikia Mungu hususani katika hekalu. Hivyo rafiki yangu Profesa huyu achague kilinge chochote kinachomfaa katika shughuli za utumishi wa Bwana, kama ataamua kulihubiri neno kwa imani ya Kirastafari, Budha, Hindu, Dini ya Afrika ya Jadi n.k, basi afanye hima kabla hajachelewa. Kwa wakristo, hekalu lilihudumiwa na watumishi wa Bwana 24, ambao ni, 1) Jehoiarib; 2) Jedaiah; 3) Harim; 4) Seorim; 5) Malchijah; 6) Mijamin; 7) Hakkoz; 8) Abijah; 9) Jeshua; 10) Shecaniah; 11) Eliashib; 12) Jakim; 13) Huppah; 14) Jeshebeab; 15) Bilgah; 16) Immer; 17) Hezir; 18) Happizzez; 19) Pethahiah; 20) Jehezkel; 21) Jachin; 22) Gamul; 23) Delaiah; 24) Maaziah. Pia kitabu cha Mtakatifu Luka, kina jumla ya sura 24. Namba hii haiko katika siasa. HAIKO.
Profesa Muhongo alidondoka, akajizoazoa! Kadondoka tena, hawezi nyanyuka, labda awe mhubiri.

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Uhakiki wa Riwaya ya Watoto wa Maman’tilie