BONDIA MSOMI KUTOKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM, ASEMA YUKO TAYARI KWA PAMBANO
Goodluck Elisaria, bondia machachari wa uzito wa
'featherweight', mwanafunzi wa mwaka wa tatu kutoka ndaki ya COHU
anayekiwakilisha Chuo Kikuu Cha Dar es salaam katika ulimwengu wa ngumi, sasa
amethibitisha rasmi kupanda tena ulingoni kukipiga na mpinzani wake Vasco
Maklin.
Maamuzi haya yanakuja baada ya Saria kupona jeraha
lake alilolipata siku ya tarehe 07/05 mara baada ya kutokea ajali ya kugongana
vichwa akiwa ulingoni hali iliyopelekea pambano hilo lihesabike kama suruhu
'technical draw'.
Bondia huyu ambaye hajawahi kupigwa, kule Congo
alifanya mambo makubwa wakampa jina la 'SariaMundende'. Hapa Tanzania
tunamwita 'SariaZege'.
"Nitampiga Maklin katika raundi ya kwanza, kisha
nitakwenda chuo kufanya test nikiwa ninatabasamu kwa ushindi!" Alisema
SariaZege.
KILA LA KHERI SARIA. WAPIGE!!