Posts

Showing posts with the label solvingkiswahiliadvance

Dhima Tano za Mofimu KI Katika Lugha ya Kiswahili

Image
Siku zote ambazo nilisimamia mitihani ya taifa, nilisimamia wanafunzi waliokuwa shule. Sikuwahi kusimamia wanafunzi wa kujitegemea mpaka ilipowadia mwaka fulani ambapo nilipangwa kwenda kusimamia mtihani wa taifa katika shule fulani ndani ya jiji la Dar es Salaam. Muda ulipowadia, nilifika katika kituo changu, baada ya kufuata taratibu zote, nilisimama pembezoni ya mti ili niweze kuwaona wanafunzi waliokuwa wakifika shuleni hapo tayari kufanya mtihani. Alipita binti mmoja mrembo sana ambaye naye alikuwa miongoni mwa wale wanaofanya mtihani, kwa sababu ya urembo wake, nilikosa nguvu za kusimama na isingekuwa kuushikilia ule mti, ningedondoka! Hata hivyo, nilikaa katika hali ya kuhisi kizunguzungu kwa muda wa dakika tano, hali ilipokuwa shwari, nikaelekea darasani ambako ndipo mtihani ulikuwa ukifanyika. Niliingia darasani, mimi na mwenzangu mmoja tuliyekuwa tunasimamia pamoja, tulitimiza taratibu zote na mtihani ulianza. Katika chumba hiki cha mtihani, yule binti mrembo sana, alik...

Njia Nne Zitumikazo Kuunda Misimu ya Lugha ya Kiswahili

Image
Niliketi katika kiti kirefu nikinywa kinywaji ambacho siwezi kukitaja. Katika kiota nilichokuwamo, mhudumu alikaa mbele yangu sehemu iitwayo ‘kaunta’ nasi tulitenganishwa na dirisha kubwa lililokuwa na nondo pana. “Mwanaidi ongeza kinywaji,” nilisema kwa sauti kali, nilijiamini kwa sababu katika kiota hiki, tulikuwa wawili tu, mimi na Mwanaidi. Kiota cha Mwanaidi hakina wateja wengi na leo nilikuwa peke yangu. Aliongeza kinywaji kama nilivyotaka, kisha akabadili wimbo na kuweka dansa moja matata. Nilitaka kuinuka ili nisakate dansa, lakini nikajizuia baada ya kukumbuka kuwa mimi ni mwalimu, tena siyo mwalimu wa kawaida, ni mwalimu wa walimu na wanafunzi. Basi nikakaa tuli nikitikisa kichwa na mabega. Lakini ghafla tukavamiwa na watu watatu. Watu hawa walivaa sare za jeshi la polisi. Bila shaka, walikuwa polisi. “Kwa nini unafungua biashara yako mpaka saa saba usiku tena ukipiga mziki kwa sauti ya juu?” aliuliza askari aliyekuwa na mbavu nene kuliko wenzake. Mwanaidi hakuwa na c...

Swali la Ufahamu na Ufupisho Kuhusu Mtu Aliye Muungwana

Image
1.    Soma kwa umakini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu kwa usahihi maswali yanayofuata. Wazo la watu wengi juu ya muungwana ni kuwa mtanashati au labda kuwa mtu arifu mwenye cheo kwa watu. Lakini nguo nzuri hazimtukuzi mtu wala hazimfanyi kuwa muungwana. Fasihi ya hili ni kuwamba, nguo ni kama ngozi ya mtu au mnyama; au hasa ni duni sana kuliko ngozi au manyoya. Ngozi ya simba haiwezi kumfanya punda kuwa simba. Uungwana wa kufanywa na mshoni ni mzaha; si uungwana wa kweli. Neno muungwana lina maana kubwa zaidi kuliko nguo nzuri au adabu nzuri na elimu nzuri. Kwa hakika twatumia vibaya neno hili kwa mtu yeyote aendaye kwa miguu miwili. Kwanza muungwana hawezi kumuudhi au kumdhuru mtu kwa maneno au matendo yake, hata kwa kumtazama. Ana moyo wa uvumilivu na anaweza kusikiliza kwa makini maoni ya watu wengine bila ya kujaribu kuwalazimisha wakubali maoni yake. Ni mkarimu, mnyofu na amini katika taiba yake kwa wengine. Hapendi kujionyesha alivyo tajiri a alivyoelimik...