Posts

Showing posts from April, 2017

SAFARI YA KUUSAKA MWEZI (sehemu ya nane)

Image
Looh! Sikuamini, niliiona Mapandagila 214 ikiwa imeegeshwa mbali kidogo, niliruka kwa furaha nikamkumbatia Chokusi, akanikwaruza ubavuni kwa vile vyuma vyake, sikuhisi maumivu. Lakini tena nikakumbuka jambo, nikauliza.             “Lakini nilipodondoka iliharibika kabisa… nitawezaje kupaa tena?”             “Niliitengeneza… kwa sasa iko vizuri na itakufikisha salama huko uendako.” Nilimkumbatia tena kwa furaha, lakini kabla sijamwachia, akanipiga mweleka, wote tukalala chini.             “Askari wanakuja na makombora, wamekwishagundua kuwa umetoroka, tambaa mpaka katika ndege yako, usinyanyue kichwa wala kugeuka nyuma, kwa heri. Chokusi alirudi katika shimo haraka, mimi nilitambaa kama nyoka kuelekea ilipokuwa Mapandagila 214, nikayasikia makombora mazito yakirushwa, nikakaza mwendo. Kombora ...

MSIMLAUMU ANTHONY JOSHUA, AMEFANYA KAZI NILIYOMTUMA

Image
Haina ubishi tena kuwa Anthony Joshua ndiye mfalme wa ndondi katika zama zetu. Laiti kama angeishi katika zama za akina Mohammed Alli, George Foreman, na Joe Frazier historia ingebadilika kidogo. Kizazi cha akina Tyson, Evander na Lenox Lewis hakimuwezi, mwakilishi wao Klitchko kapigwa vilivyo. Pambano lake la leo, limefunika pambano la wale vijana wa uzito wa manyoya, Mayweather na mwenzake Pacquiao… ngumi zimepigwa mpaka kivumbi kikatimuka. Kabla pambano halijaanza, nilipata kumtumia ujumbe kijana wangu Anthony Joshua uliosomeka, “its not over untill its over”, Joshua hakusita kuujibu kwa kusema, “Next Stop The Ring.” Kisha akazima data. Pambano la Klitchko na Joshua lilipoanza, round ya kwanza mpaka ya tano, Joshua alishambulia sana kwa mapigo yote ya kifundi. Watu walimshangilia kama kawaida, huku mimi nikitafuta namna nzuri ya yeye kushinda. Ilipofika Round ya sita, Joshua alionekana kuchoka kidogo hii ni kwa sababu kwa round tano mfululizo alikuwa akirusha makonde, basi ...

Taaluma ya Semiotiki Katika Mazingira Halisi

Image
Eleza kwa mifano muafaka kutoka katika mazingira halisi juu ya taaluma ya semiotiki. Semiotiki imefasiliwa na wataalamu mbalimbali, na hizi ni maana zilizotolewa na baadhi ya wataalamu hao. Kwa kuanza na mtaalamu Massamba (2004), yeye anasema kuwa, semiotiki ni taaluma ya kisayansi inayojishughulisha na uchunguzi na uchanganuzi wa mifumo ya ishara mbalimbali ikiwa inazingatia zaidi uhusiano baina ya kiwakilishi na kitajwa. Pia mtaalamu Ferdinand de Saussure kama alivyonukuliwa na Morris (1971) amefasili semiotiki ni uhusiano kati ya alama na kitu, jambo au hali ya kitu inavyowakilishwa, akaendelea alama ni kiashiria na kitu ni kiashiriwa. Hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya kiashiria na kiashiriwa. Charles (1934), alishughulikia dhana ya semiotiki kwa kuunda tanzu tatu ambazo ni sintaksia, Pragmatiki na semantiki.Sintaksia ni taaluma ya uhusiano kati ya ishara na vitu/ vielezo jinsi vinavyotumika, pragmatiki ni taaluma ya uhusiano kati ya mfumo wa ishara na mtumiaji wake na...

VICHEKESHO VILIVYOTUFIKIA WIKI HII

HPUPIL: Exami~Nation. (TEACHER ) TEACHER: One day our country will be corruption free. What tense is that? PUPIL: Future Impossible Tense. (TEACHER ) TEACHER: What do we call a small lizard in English? PUPIL: Lizzy baby. (TEACHER ) TEACHER: Juma is climbing a tree to pick some mangoes. (Rewrite beginning with mangoes) PUPIL: Mangoes, Juma is coming to pick you. (TEACHER ) TEACHER: What do we call a male duck in English? PUPIL: Mr daka. (TEACHER PUPIL: Would you punish me for something I did not do? TEACHER: No! Of course not! PUPIL: Good, I asked because I did not do my homework. (TEACHER ) Hii ni kazi ngumu kweli Mahusiano ya kimarekani: Siku ya 1= mahusiano Siku ya 2= unakumbatia Siku ya 3= unakumbatia tena Siku ya 4= busu Siku ya 5= denda Siku ya 6= mapenzi ********* Mahusiano ya kibongo: Siku ya 1= unatongoza Siku ya 2= unatongoza tena Siku ya 3= unatongoza tena Siku ya 4= anakubalii Siku ya 5= mahusiano S...

TATHMINI YA WAGOMBEA NAFASI YA URAIS-DARUSO (UDSM)

Anaandika Makoba Daud Japokuwa Wagombea wote wamepitishwa na kamati ya wapiga ramli, tena wagombea hawana mvuto kuanzia sera mpaka majina yao, hatuwezi kususa kabisa kuutazama uchaguzi na mwenendo wa kampeni zao. RICHARD Anatilia mkazo suala la kusoma mapato na matumizi ya DARUSO. Pia anahoji uhalali wa kulipa nauli katika mabasi ya CRDB. Amekopa hoja ya Charles William ya kuwalipa posho ma CR. CHANGAMOTO Wakati wa uzinduzi wa kampeni, hakupata kusikilizwa na watu wengi japo alijieleza vizuri. Kuna mpinzani wake alicheza mchezo mchafu wa kuwatoa watu nje ili kupunguza upinzani. Pia Hatajwi sana katika mitandao ya kijamii. *Siku hii ya mwisho, anaonekana kuanza kukubalika na watu wengi. Hivyo ashone suti nyeusi, huenda akawa raisi. EMANNUEL Anataka kuirudisha DARUSO kwa wana DARUSO. Anadai yeye sio kiongozi wa kujikombakomba na kujipendekeza. Amekopa hoja ya Shamira Mshangama inayotaka Dean afanye kazi ya kushauri wanafunzi na si vinginevyo. ...

SAFARI YA KUUSAKA MWEZI (sehemu ya saba).

Image
Nilikaa ndani ya chumba kile mpaka nilipopitiwa na usingizi, nikiwa usingizini niliota jinsi watu wa nchi yangu walivyokuwa wakiteseka, kabla ndoto haijaisha niliamshwa na binti waziri, mkononi akanipatia mikate miwili iliyotengenezwa kwa ufuta, nikagundua upembe ndio ulileta chakula hicho. Nilikula mikate ile mpaka nikaimaliza, wakati nikiendelea kuusikilizia utamu wa mkate, binti waziri alinishika mkono kisha akasema nami taratibu.             “Hakuna aliyewahi kukataa agizo la mfalme, kesho asubuhi utaondoka kwenda kuvichukua vitabu vya mafanikio… usiogope, utasindikizwa na askari kadhaa.”             “Siwezi kwenda, watu wangu wanateseka.” Nilibisha, binti akatoka ndani na kuufunga mlango. Nikabaki katika chumba nikiwa mpweke. Nikiwa ndani ya chumba kile, niliwaza mengi, kubwa zaidi nilifikiri namna ya kutoroka ili niendelee na safari yangu. Ulin...

Vita ya Bwana Makani na Utamu Korea itakavyokuwa

Kwanza hakuna anayeombea mpambano huu utokee, kwani vita hivi vitakuwa na madhara kwa dunia nzima. Makala haya yanalengo la kuchochea amani. Wengi wetu tunaomba yaendelee kuwa ni maneno kama siku zote! Ila kama wataamua kupigana basi pambano litakuwa hivi. Bwana Makani atarusha kombora kali kwa kutumia kifaru cha aina yake kitwacho ‘Karl Great’. Kombola hilo lisilo na macho litaipiga ‘Utamu Korea’, Kimung’unya mzee wa kiduku kitengo mawe, ataliamsha dude, kwa kutupa kombora hatari linalotembea katika kifaru ambacho hupita katika reli yake, sio kingine ni ‘Schwerer Gustav and Dora’. Hapo sasa vita vitakuwa vimenoga, wanajeshi wa pande zote kutokana na uzito wa makombora hayo hawatatumia silaha ndogo, watabeba ‘RPG-71’ silaha hii kwa urefu wake inaitwa (Ruchnoy Protivotankovyy Granatomyot), sisi wataalamu wa mambo haya huwa tunaiita ‘ant – armor’ yaani huwa inasambaza chochote. Ikikohoa hii haina kusema ‘gari lile la fulani huwa halipitishi risasi wala mabomu’, hii huwa inabomoa tu...

RIWAYA YA TAHARUKI (mwanzo mpaka mwisho)

Image
RIWAYA – TAHARUKI MTUNZI – DAUD MAKOBA 0754 89 53 21 SURA YA KWANZA Mako, mwosha magari maarufu mtaani Sakubimbi, alishughulika kama kawaida yake. Leo alionekana kuchoka zaidi, pengine tenda ya kuosha Fuso, ilimnyong’onyeza vilivyo. Mwanaume huyu alikuwa na mwili wa wastani tu, kakamavu aliyezifikia kilo 61 kwenye uzani. Wakati akiendelea kuosha Fuso ile, jua liliendelea kuipiga ngozi yake, naye hakuisha kushika nywele, kipilipili kilichokoza, ngumu zimerundikana na kutengeneza kitu kama mkutano wa nzi, labda hazikuliona chanuo kwa muda! Fuso sasa ilitakata haswaa, Mako akatembea mpaka alipo mwajiri wake, akachukua fedha na kuzielekeza kibindoni, kabla hazijafika akastushwa na sauti yenye kitetemeshi cha kuigiza, “Uko chini ya ulinzi, toa fedha uishi…” Mako akabinua bichwa ili apate kumtazama aliyetema maneno hayo,macho yake yakagongana na sura ya mtoto mdogo, umri miaka saba, kavaa sare za shule na begi dogo kalipachika mgongoni, kisha akambeba kindakindaki. Kwa ambae...