Vita ya Bwana Makani na Utamu Korea itakavyokuwa
Kwanza hakuna anayeombea mpambano huu utokee, kwani vita hivi vitakuwa
na madhara kwa dunia nzima. Makala haya yanalengo la kuchochea amani. Wengi wetu
tunaomba yaendelee kuwa ni maneno kama siku zote! Ila kama wataamua kupigana
basi pambano litakuwa hivi.
Bwana Makani atarusha kombora kali kwa kutumia kifaru cha aina yake
kitwacho ‘Karl Great’. Kombola hilo lisilo na macho litaipiga ‘Utamu Korea’,
Kimung’unya mzee wa kiduku kitengo mawe, ataliamsha dude, kwa kutupa kombora
hatari linalotembea katika kifaru ambacho hupita katika reli yake, sio kingine
ni ‘Schwerer Gustav and Dora’.
Hapo sasa vita vitakuwa vimenoga, wanajeshi wa pande zote kutokana na
uzito wa makombora hayo hawatatumia silaha ndogo, watabeba ‘RPG-71’ silaha hii
kwa urefu wake inaitwa (Ruchnoy Protivotankovyy Granatomyot), sisi wataalamu wa
mambo haya huwa tunaiita ‘ant – armor’ yaani huwa inasambaza chochote. Ikikohoa
hii haina kusema ‘gari lile la fulani huwa halipitishi risasi wala mabomu’, hii
huwa inabomoa tu.
Kama kawaida Utamu Korea atatishia kutumia kombora la nyuklia ‘B53’,
kitisho hiki kitasababisha Bwana Makani ashambulie haraka kwa kutumia dhana ya
hatari sana iitwayo ‘MOAB/GBU-43/B Massive Ordinance Air Blast’… mimi huwa naiita
‘fukufuku zamisha’ kwani ikiachiwa inauwezo wa kuharibu majiji tisa kwa kipimo
cha radius ya 137.61 m.
Vita vikifikia hapo, Utamu Korea atajibu kwa kumrusha ‘king of bombs’ Tsar
Bomba. Hatua hii itafungulia matumizi ya nyukilia kwa pande zote mbili. Madhara
yake yatakuwa ni makubwa sana kuwahi kushuhudiwa na dunia hii.
Wito wangu, lazima tuombe kila mtu kwa dua yake – BALAA HILI LISITOKEE.