Mfano wa Barua ya Maombi ya Kazi TAKUKURU Ajira Mpya

Kijana wa kiume ameshikilia barua ya maombi ya kazi takukuru
TAKUKURU  wametangaza nafasi za kazi kwa vijana wenye sifa mbalimbali. Nafasi mpya za kazi zilizotangawa na TAKUKURU zinayahusu makundi mawili: Kundi la kwanza, Muombaji awe na angalau elimu ya shahada ya kwanza iliyotolewa na chuo kinachotambuliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika moja ya fani zifuatazo: Uhasibu, Usanifu Majengo, Usimamizi wa Biashara, Usanifu wa Majengo, Ukadiriji wa Majengo (Quantity Surveying), Uhandisi wa Usindikaji wa Kemikali, Maendeleo ya Jamii, Sayansi ya Kompyuta/TEHAMA, Uhandisi wa Ujenzi, Uchumi na Mipango, Uhandisi wa Umeme. Lishe na Sayansi ya Chakula, Usimamizi wa Rasilimali Watu, Usimamizi na Tathmini ya Ardhi, Sheria, Uhandisi wa Mitambo, Uhandisi wa Mafuta na Gesi, Ununuzi na Ugavi, Usimamizi wa Miradi, Ushauri Nasaha, Utawala wa Umma, Mahusiano ya Umma/Mawasiliano ya Umma, Usimamizi wa Kumbukumbu, Sayansi ya Michezo/Elimu ya Viungo, Takwimu, na Uhandisi wa Maji.

Kundi la pili: ulinzi, ufundi wa magari, ujuzi wa udereva, huduma kwa wateja, msaidizi wa uhasibu, masomo ya ukatibu, fundi wa kompyuta na fundi wa mashine za ofisi.

Katika maombi haya, ni lazima uandike wasifu (CV) inayokubalika tena yenye wadhamini watatu, na ni lazima, uandike barua ya maombi ya kazi.

Hapa tunakupa mfano wa barua ya maombi ya kazi katika nafasi mpya za kazi TAKUKURU. Kwa sababu nafasi hizi ni chache na waombaji ni wengi, wengi watachujwa kwa kukosea kuandika barua pekee, hivyo, utakapoandika barua sahihi kama inayotolewa katika mfano huu, utakuwa katika nafasi nzuri ya kupata kazi hii.

Mtaa wa Kambangwa,
S.L.P 120,
KINONDONI, DAR ES SALAAM.
13/04/2026.

Mkurugenzi Mkuu,
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa,
Mtaa wa Jamhuri,
S.L.P 1291,
1101 DODOMA.

Yah: OMBI LA KAZI YA MCHUNGUZI MSAIDIZI

Mimi ni mwanamume Mtanzania mwenye umri wa miaka 21. Ninaomba Kazi ya Mchunguzi Msaidizi kama ilivyotangazwa na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) siku ya tarehe 11/04/2026 katika tovuti ya TAKUKURU.

Nina ujuzi wa Udereva (Dereva Daraja C), ujuzi huu nimejifunza katika chuo cha VETA Shinyanga na kuhitimu mwaka 2025. leseni yangu ni halali nikiwa na rekodi safi ya udereva pamoja na uzoefu wa mwaka mmoja. Zaidi ya hayo, nina elimu ya kidato cha Nne niliyoipata katika Shule ya Sekondari Kishapu mwaka 2023.

Kutokana na elimu yangu, uwezo wa kufanya kazi nilionao pamoja na kuwa na sifa zinazotakiwa, ninaamini kuwa ninastahili kupata kazi hii. Endapo nitapata kazi ya Mchunguzi Msaidizi, nitafanya kazi kwa bidii na kutimiza majukumu yangu yote. Pia nipo tayari kufanya kazi wilaya yoyote ya Tanzania Bara.

Nipo tayari kwa usaili siku yoyote nitakayohitajika. Vilevile, ninatarajia majibu mazuri kutoka kwako na nimeambatanisha nakala ya vyeti vyangu kwa uthibitisho zaidi.

Wako,

______________

JUNIOR KINYAUNYAU PUSIKATI

Tunaweza Kukuandikia Barua ya Maombi ya Kazi, Wasifu (CV), pamoja na Kukusaidia Kufanya Maombi ya Kazi Hizi Katika Akaunti Yako, Ili Kuwasiliana na Mwalimu, Gusa Hapa

Popular posts from this blog

SMS 20 za Vichekesho Zinazochekesha Sana

Jinsi ya kuandaa Somo na Kuwasilisha Oral Interview Ajira za Walimu

Mbinu 4 na Maswali 50 Kusaidia Ufaulu Oral Interview Ajira za Walimu