Posts

Showing posts from November, 2017

Sitasahau Nilipolala na Mwanamke Juu ya Kaburi (27)| Riwaya

Image
Nilishtuka nikaamka. Shingo iliuma lakini nilijikaza. Nilikuwa mahali nisipopafahamu, nazo fahamu zikazidi kunirejea taratibu hata nikagundua palikuwa pangoni. “Umetumwa kuja kuniokoa! Lakini nimekudondosha kwa kofi moja tu.” Mtoto alizungumza, bila shaka ni Chimota. “Sijabobea katika ulozi!” nilijibu. “Nani kabobea?” “Wewe, inasemekana ulizaliwa nao.” “Ulishuhudia wakati nazaliwa?” “Hapana. Niliambiwa tu.” “Ujinga ni kukubali kila unachoambiwa!” alinijibu. Nikakaa kimya. Nilizungumza na Chimota mpaka tukazoeana. Nilipomuuliza aliwezaje kuishi pangoni badala ya kuishi katika falme ya Matumbawe, alinijibu kuwa, aliutoroka utawala huo baada ya kugundua walitaka kumtumia katika mambo ya kunyanyasa watu wengine. Pia aligundua siri kuwa, yeye hakuwa mzaliwa wa Matumbawe, bali aliibwa kichawi na kufikishwa huko. Alipogundua nguvu zake za ziada, hakusita kukimbia. Hata hivyo, hakujua hasa ni kwa namna gani angerudi tena nyumbani, ujio wangu mahali pale ulimpa faraja na ...

Roma na Stamina Katika Upumbavu wa Kimkakati| Makala za Mwalimu

Image
Upumbavu wa kimkakati, ni kutumia busara ulizonazo kuupandisha juu upumbavu, ukasikika na kusifiwa kila pahala na kila mtu isipokuwa sisi! Msanii yeyote atakaye kuifanya kazi yake kwa misingi na weledi, hana budi kuwa na falsafa moja inayoeleweka. Roma alianza akiwa na falsafa moja tu, kulisema tabaka lisilopenda kusemwa. Hata hivyo, mwishoni alianza kubadilika na nilishangaa lakini niliamini niliposikia wimbo wake uitwao ‘k’ ajabu ya mwaka ule! Baada ya kutekwa, mambo yamebadilika zaidi! Naona sasa ule msemo wake wa “nawaachaje wanaobaki” unafanya kazi kwa kasi. Akishirikiana na msanii mwenzake-Stamina, ametoa wimbo uitwao ‘Kiba_100’. Wakati lengo la Muziki likiwa kuburudisha, kuelimisha na kuonya, wimbo huu unalengo la peke yake! Kusambaza matusi kwa njia ya kificho. UPUMBAVU! Ni aibu kusikiliza wimbo huu ukiwa na watu wanaokuzidi umri. Ni aibu pia, kuusikiliza pembezoni mwa watu mnaoheshimiana sana. Na itaendelea kuwa aibu kuusikiliza katika kundi la watoto wadogo! Kama ...

Baada ya Mugabe, Waziri wa Fedha Zimbabwe Kukiona cha Mtema Kuni

Image
Baada ya jeshi kuchukua mamlaka na kumkabidhi Mnangagwa kwa kile kilichosababishwa na maamuzi magumu ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Robert Mugabe kumtimua makamu wake na kutaka kumwachia mamlaka mkewe, purukushani bado zinaendelea. Aliyekuwa waziri wa fedha wa nchi hiyo , Ignatius Chombo amefikishwa mahakamani akikabiliwa na mashtaka ya ufisadi na utumiaji mbaya wa mamlaka wakati alipokuwa akishikiria nyadhifa serikalini. Chombo alikamatwa tangu tarehe 14 Novemba saa chache baada ya Mugabe kuzuiliwa nyumbani kwake. Kuhusu jeshi kumpora mamlaka Mugabe, mahakama imesema jambo hilo ni halali. Tayari Mnangangwa ameapishwa na hali nchini Zimbabwe inaonekana kuwa shwari.

Uhusiano wa Fasihi na Tanzu Nyingine za Sanaa

Image
Fasihi ni taaluma inayotumia sanaa maalum ya lugha. Nayo SANAA ni uzuri unaojitokeza katika umbolililosanifiwa, umbo ambalo mtu hulitumia kueleza hisi zinazomgusa kwa kutoakielelezo au vielelezo vyenye dhana maalum. Ukiachilia mbali fasihi, baadhi ya tanzu nyingine za sanaa ni: Ususi, utarizi, sanaa za maonyesho, ufinyanzi, uchoraji na uchongaji. Upo uhusiano wa fasihi na tanzu hizi za sanaa kama inavyoelezwa: Zote ni kazi za sanaa. Kama ufinyanzi, uchoraji na uchongaji ulivyo, yaani uzuri unaojitokeza katika umbo lililosanifiwa, umbo ambalo mtu hulitumia kueleza hisi zinazomgusa kwa kutoa kielelezo au vielelezo vyenye dhana maalum. Fasihi na tanzu nyingine za sanaa hutoa mafunzo fulani. kwa mfano, katika kazi ya fasihi andishi ya WATOTO WA MAMAN’TILIE , tunapata mafunzo kuwa, ulevi si suluhisho la matatizo. Pia, katika sanaa nyingine kama sanaa za maonyesho, kuna mafunzo ambayo watazamaji huyapata. Fasihi na tanzu nyingine za sanaa hutegemea watu. Riwaya, tamthiliya na ushair...

Jaribio la Kiswahili| Kidato cha Kwanza | past paper

Image
MUDA: SAA 01:00 MAELEKEZO 1.    Mtihani huu una sehemu A na B. 2.    Jibu maswali yote. 3.    Simu za mkononi na vifaa vingine vinavyohusiana navyo haviruhusiwi ndani ya chumba cha mtihani. SEHEMU A 1.    Andika kweli kwa kauli ya kweli na si kweli kwa kauli ambayo si ya kweli. i.              Nomino ni aina ya neno ambayo hutoa taarifa kuhusu kitenzi. ii.             Wataalamu wa isimu ya lugha wanabishana kuhusu idadi ya aina za maneno, wapo wanaosema kuna aina nane, saba na tisa. iii.            Kitenzi hakina maana yoyote inayoeleweka. iv.           Kielezi huelezea kuhusu kitenzi kilivyotendeka. v.            Vihisishi ni aina ya maneno ambayo hugusa vionjo v...

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne

Image
Risala ni hotuba fupi iliyokatika maandishi na ambayo husomwa mbele ya mgeni rasmi ikielezea kuhusu mafanikio, changamoto na maombi ya kundi fulani. Muundo wa Risala -       Utangulizi. Katika kipengele hiki, cheo cha kiongozi (mgeni rasmi) hutajwa. Pia kundi linalowakilishwa. -       Kiini. Mafanikio ya kundi, changamoto za kundi, mapendekezo na ushauri. -       Hitimisho. Kipengele hiki hukaa shukrani. Sasa hebu tazama mfano huu wa risala: Swali; Jifanye wewe ni mwanafunzi wa kidato cha nne na umechaguliwa kuandaa risala itakayosomwa mbele ya mgeni rasmi siku ya mahafali yako ya kumaliza kidato cha nne. Andika risala utakayoisoma siku hiyo. RISALA YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE KWA MGENI RASMI Ndugu mgeni rasmi, waalimu, wazazi, wanafunzi wenzetu, wageni waalikwa mabibi na mabwana. Ndugu mgeni rasmi, tunayofuraha kukualika leo hii katika sherehe yetu ya mahafari haya ya kid...

Masai (Mc Kapalalai) wa Siri za Familia Mapenzini na Mwigizaji Recho

Image
NI kweli, si maigizo tena kama wafanyavyo siku zote. Masai (Mc Kapalalai), amezama katika dimbwi zito la mahaba na mwigizaji mwenzake wa Siri za Familia – Recho! Inasemekana kuwa, Masai kwa sasa haambiwi lolote juu ya mwigizaji mwenzake Recho. Hajiwezi na sasa yupo tayari kuchukua jiko. RECHO AGOMA KUJIBU Recho alipoulizwa kuhusu taarifa hizi kama zimesheheni ukweli wowote, alikataa kujibu kwa madai kuwa kwa wakati huo alikuwa na mambo mengi ya kufanya hivyo atafutwe baadaye. Hata alipotafutwa baadaye, hakuwa tayari kutoa ushirikiano. MAJIBU YA MASAI Alipoulizwa kuhusu tetesi hizi, Masai (Mc Kapalalai), alisema kwa sasa hayuko tayari kulizungumzia suala hilo, jambo linaloleta utata na kutufanya tuamini kuwa huenda wawili hao wako mapenzini. Recho na Mc Kapalalai (Masai), ni waigizaji wa tamthiliya ya Siri za Familia. Tamthiliya hii, huzungumzia maisha halisi na purukushani kedekede zinazotokea katika familia zetu. Dalili zote zinaonyesha kuwa, wawili hao ni w...