Baada ya Mugabe, Waziri wa Fedha Zimbabwe Kukiona cha Mtema Kuni
Baada ya jeshi kuchukua mamlaka
na kumkabidhi Mnangagwa kwa kile kilichosababishwa na maamuzi magumu ya
aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Robert Mugabe kumtimua makamu wake na kutaka
kumwachia mamlaka mkewe, purukushani bado zinaendelea.
Aliyekuwa waziri wa fedha wa nchi hiyo, Ignatius Chombo amefikishwa mahakamani akikabiliwa na mashtaka ya ufisadi
na utumiaji mbaya wa mamlaka wakati alipokuwa akishikiria nyadhifa serikalini.
Chombo alikamatwa tangu tarehe 14
Novemba saa chache baada ya Mugabe kuzuiliwa nyumbani kwake.
Kuhusu jeshi kumpora mamlaka
Mugabe, mahakama imesema jambo hilo ni halali.
Tayari Mnangangwa ameapishwa na
hali nchini Zimbabwe inaonekana kuwa shwari.