Jaribio la Kiswahili| Kidato cha Kwanza | past paper
MUDA: SAA 01:00
MAELEKEZO
1.
Mtihani
huu una sehemu A na B.
2.
Jibu
maswali yote.
3.
Simu
za mkononi na vifaa vingine vinavyohusiana navyo haviruhusiwi ndani ya chumba
cha mtihani.
SEHEMU A
1. Andika
kweli kwa kauli ya kweli na si kweli kwa kauli ambayo si ya kweli.
i.
Nomino ni aina ya neno ambayo hutoa taarifa
kuhusu kitenzi.
ii.
Wataalamu wa isimu ya lugha wanabishana
kuhusu idadi ya aina za maneno, wapo wanaosema kuna aina nane, saba na tisa.
iii.
Kitenzi hakina maana yoyote inayoeleweka.
iv.
Kielezi huelezea kuhusu kitenzi
kilivyotendeka.
v.
Vihisishi ni aina ya maneno ambayo hugusa
vionjo vya moyo.
SEHEMU B
2. Andika
hadithi kuhusu kisa kisemacho JEURI ILIMPONZA CHURA.
TAMATI
Mwalimu
Makoba