Fasihi ya Watoto na Vijana | KF 203
Fasihi ni Sanaa ambayo hutumia lugha kuwasilisha ujumbe uliokusudiwa.
Fasihi ya watoto na vijana
ni aina ya sanaa ambayo inatumia lugha kufikisha ujumbe kwa watoto na vijana.
Mtoto ni nani?
Linaweza kutafsiriwa kwa
kutumia vigezo mbalimbali vya kimuktadha:
Kiimani
Kibaiolojia na Kiumri
Wafura (2011) amegawanya
watu katika makundi manne:
i. 0-17 watoto
ii. 18-34 vijana
iii. 35-52 utu uzima
iv. 53 na kuendelea, wazee
Mamlaka za kiserikali na
mashirika mbalimbali yanamtambua mtoto kuwa mtu yeyote ambaye ana umri wa chini
ya miaka 18.
Kuna watoto wadogo na
watoto wakubwa (vijaluka). Vijaluka ni watoto wakubwa ambao wako katika umri wa
kujitambua.
Mtazamo mwingine kuhusu
fasihi ya watoto:
Wamitila (2008) anasema
suala la ufafanuzi wa fasihi ya watoto linaweza kueleweka kwa kutumia mitazamo
miwili:
i. Kuwalenga watoto kama
hadhira.
ii. Ni ile ambayo maudhui
na dhamira zilizopo zinawarejelea watoto.
Mtazamo mwingine:
Ni aina ya sanaa ambayo
watumizi wake ni watoto.
Ili kuweza kutambua fasihi
ya watoto, zipo nduni (sifa) mbalimbali.
i. matumizi ya picha,
vielelezo na michoro.
Lengo la kutumia hivyo ni:
-
Picha yaweza tumika kama simulizi hata kama
mtoto hajaweza kusoma.
-
Wahusika wake wakuu, nguli au shujaa lazima
wawe watoto. Hata hivyo, hii haimzuii mwandishi kutumia wahusika watu wazima.
-
Hutumia lugha rahisi.
-
Huwa na visa vichache.
-
Hujengwa katika msuko sahili wa matukio.
Muundo mwepesi.
-
Hutumia sana fantasia. Fantasia ni matumizi
ya mambo ambayo hayapo katika ulimwengu wa kawaida.
Kwa nini mwandishi hutumia fantasia?
-
Huburudisha
-
Humjengea mtoto au hadhira taswira
mbalimbali.
-
Huhusisha milango mingi ya fahamu. Mtunzi
hutumia viungo vya mwili, picha na maelezo yanayomwezesha kuhisi harufu fulani
na vitu fulani ambavyo humjengea picha kichwani mwake. Watoto hupenda kusikia,
kuona, kunusa na kugusa badala ya maneno matupu.
-
Maisha ya wahusika huanzia na kuishia
nyumbani. Sababu ni kuwa, mtoto hana uwezo wa kujitegemea hivyo wahusika lazima
waishie nyumbani hata kama akiondoka lazima atarudi. Mfano, kitabu cha Bahati
na Mwewe.
-
Mambo mema ndiyo matarajio. Lengo ni
kuwajengea watoto mtazamo chanya.
-
Hutumia mbinu ya kurudiarudia. Mfano,
marudio ya sentensi au neno. Lengo ni kuwawezesha walengwa waelewe
kinachowasilishwa.
-
Kazi za watoto hujikita katika motifu ya
safari na motifu ya msako. Motifu ni kipengele kinachojirudiarudia ambacho
huweza kuwa cha kijamii au kimaudhui, kinachotokea katika kazi za fasihi. Mfano,
motifu ya majambazi matatu, saba n.k
Vitabu vingi vina motifu
ya Bibi Kizee Mchawi.
Motifu ya safari na msako.
Msako wa kitu
kilichopotea.
-
Fasihi ya watoto inajali saikolojia ya
mtoto. Inazingatia mtoto anapenda nini na hapendi nini?
Dhima
ya fasihi ya watoto na vijana
i. Kuburudisha, Hii ni
dhima kuu, mtoto anaweza kuburudika kwa kuangalia picha, jinsi lugha
inavyotumika kumfuatilia mhusika fulani n.k
ii. Kumuondoa mtoto katika
hali aliyonayo mpaka katika hali bora zaidi. Usomaji wa hadithi husaidia mtoto
kuongeza ufahamu.
iii. Kuchachawisha ubunifu
(kuhamasisha). Kazi nyingi za fasihi zinamfanya mtoto aweze kufikiria kuhusu
mazingira fulani.
iv. Humsaidia mtoto
kujielewa na kuwaelewa wengine.
v. kupata uzoefu na
kuelewa umbo la lugha.
vi. husaidia katika
kujifunza masomo na mada mbalimbali.
Aina za fasihi
Fasihi simulizi za watoto
na fasihi andishi za watoto.
Bunilizi (fiction), si
bunilizi (nonfiction)
Bunilizi ni ubunifu.
Kazi zinazopatikana katika
bunilizi ni:
Ngano, visasili, visakale,
visafuli, hadithi fupi, novela, riwaya, tamthiliya, ushairi, semi, michezo ya
watoto…
Visasili hueleza sababu ya
matukio fulani, mfano, kwa nini sungura ana mkia mfupi.
Novela haina uchangamani
wa visa na matukio kama riwaya.
Aina za bunilizi
Zinatokana na kuangalia
bunilizi imetawaliwa na nini, imetokana na nini, ikoje?
i. Bunilizi ya kifantasia
hii imetawaliwa na mambo
ya ajabu ajabu. Mamboya njozi. Mara nyingi hutawaliwa na wanyama, huwa katika
ulimwengu dhahania, hutawaliwa na nguvu za ajabu, vikaragosi…
ii. Bunilizi ya kisayansi
(saifa)
Ni kazi ya sanaa ambayo
imetungwa kwa kuegemea kwenye sayansi yaani matukio ambayo yanaweza
kuthibitishwa kisayansi.
iii. Bunilizi ya
kihistoria
Hii imeegemea katika mambo
ambayo yamekwishatokea.
iv. Bunilizi ya kihalisia
Katika bunilizi hii, kuna
mhusika wa kweli ambao wanapatikana katika ulimwengu halisi.
Si bunilizi
Ni kazi ya sanaa ambayo
mambo au matukio ya kweli hutawala zaidi kuliko iliyo katika bunilizi.
Si bunilizi huwa na
taarifa za watu za kweli katika dunia halisi. Hulenga kutoa taarifa au
kuonyesha.
Aina zake:
Tawasifu
Kumbukumbu
Hadithi
Ni masimulizi au kisa
kinachohusu suala fulani kwa muhtasari na mara nyingi huwa na mhusika mmoja
aliyejitokeza sana ingawa hakuzwi kwa mapana yake kama ilivyo katika riwaya.
Matei (2011) anaeleza
hadithi kama masimulizi yanayowasilishwa kwa lugha ya kinathari kuhusu watu,
matukio na mahali mbalimbali.
Hadithi huwa haina upana
wa kimaudhui au uchangamano wa visa au matukio kama ilivyo katika riwaya.
Katika hadithi, huwa kuna
fanani na hadhira, pia, huweza kuwa ya ukweli au kubuni lakini ikiwa na maadili
fulani.
Sifa zinazobainisha hadithi
I.
Haitumii wahusika wengi.
II.
Inahusu jambo moja kubwa lililowekwa katika
utamaduni wa hadhira husika.
III.
Ni masimulizi ya kubuni.
IV.
Haina uchangamano wa visa au inatakiwa iwe
na muundo sahili.
V.
Inaeleza matukio kwa mpangilio wa moja kwa
moja. Kuanzia tukio la mwanzo au la mwisho.
VI.
Huwa na mgogoro au tukio la kuelezea.
Riwaya
Wataalamu mbalimbali
wanajadili kwa kutumia vigezo na sifa tofautitofauti. Mphahlele (1976) riwaya
ni masimulizi ya kinathari yenye maneno kati ya 35,000 mpaka 75,000. Riwaya
fupi inaanzia maneno 35,000 mpaka 50,000 na ndefu inafika mpaka maneno 75,000.
Mhando na balisidya (1976)
wanakubaliana na Mpahlele kuhusiana na kigezo cha urefu.
Senkoro (2011) tukitumia
kigezo cha urefu tutapata riwaya chache sana katika fasihi ya Kiswahili.
Senkoro anasema, riwaya ni
kisa mchangamano ambacho huweza kuchambuliwa na kupimwa mapana na marefu,
kifani na kimaudhui.
Riwaya ni kisa au
mkusanyiko wa visa.
Riwaya ni hadithi ndefu ya
kubuni yenye visa vingi, wahusika wengi na inayoangalia mambo muhimu katika
jamii.
Vipengele muhimu katika kueleza maana ya riwaya:
Uchangamano wa visa. Huwa na wahusika wengi na dhamira nyingi.
ii. Kufungamana na wakati. Ili kuweza kueleza na kufafanua.
iii. Mawanda mapana.
iv. Mpangilio, msuko wa matukio. Msuko changamano wa matukio.
Hivyo, suala la urefu si kigezo muhimu katika kufafanua riwaya.
Ngano
Senkoro (1982) ngano ni
hadithi za kimapokeo zitumiazo wahusika kama wanyama, miti na watu ili kuelezea
au kuonya watu kuhusu maisha.
Wamitila (2004) anasema
ngano ni hadithi za kimapokeo ambazo hutumia wahusika wa aina mbalimbali kama
miti, majitu, watu ili kuweza kusimulia tukio au kisa fulani chenye mafunzo.
Matei (2011) anasema ngano
ni hadithi za kimapokeo ambazo hutumia wahusika kama vitu, mizimu, uchawi…
Hurafa ni aina ya ngano
ambayo wahusika wake ni wanyama lakini hutumika kuwakilisha tabia za
kibinadamu.
Hekaya ni aina ya ngano
ambayo wahusika wake ni binadamu ili kuwakilisha tabia fulani.
Sifa za ngano
i.
Huanza na muundo maalumu au fomula maalumu.
Mfano, hadithi hadithi… paukwa…
ii.
Huwa na kimalizio maalumu. Miisho ya
kifomula. Mfano, wakaishi raha msitarehe.
iii.
Husimuliwa kwa njia ya kinathari tena kwa
mdomo.
iv.
Huwa na funzo fulani kulingana na maadili
ya jamii.
v.
Huwa na muingiliano na tanzu zingine kama
nyimbo.
vi.
Wahusika wake mara nyingi ni bapa.
vii.
Mandhari hayapewi nafasi kubwa na wakati
mwingine hayaoneshwi.
viii.
Dhamira za kingano zinahusu mapambano kati
ya wema na ubaya.
ix.
Muundo wake ni sahili.
x.
Zinahusu kufichua hadhira iliyofichika.
xi.
Kuwa na ujirudiaji.
Tamthiliya
Ni andiko ambalo lengo
lake ni kwa ajili ya maonyesho.
Ushairi
Ni utungo ambao unaonyesha
jinsi wazo, hali, kitu au tukio fulani kwa kutumia lugha ya mkato, mpangilio
maalumu wa maneno yenye kugusa moyo.
Shairi ni utungo ambao
unagawanyika katika beti.
Nyimbo
Utungo wenye mahadhi ya
sauti ya kupanda na kushuka. Kuna aina nyingi za nyimbo:
Tendi ni aina ya wimbo
inayohusu mashujaa.
Fasihi ya watoto kwa ujumla
Nadharia:
Fasihi chimbuko lake ni
Mungu (Plato).
Udhaifu
Inachanganya imani na
taaluma. Huwezi kuthibitisha kisayansi.
Sihiri
Nguvu ama uwezo wa
kimiujiza.
Mwigo wa uigaji
Wananadharia hii wanaamini
kwamba, mambo yote yaliyopo katika dunia hii yanaigwa toka kwa Mungu.
Nadharia ya kiyakinifu
Waasisi ni Karl Max na
Engels.
Mwanadamu ni zao la
maumbile ambayo yalitokana na mabadiliko. Waamini kuwa, mwanadamu alianza kama
sokwe.
Fasihi ya Watoto
Ilitokana na simulizi au
hadithi ambazo zilikuwa zikitolewa katika jamii kwa njia yam domo kutoka kizazi
kimoja hadi kingine.
Simulizi hizo zilikuwa na
lengo la kuburudisha jamii.
Tunaweza kugawa fasihi ya
watoto katika vipindi vifuatavyo:
Zama
za mwanzo 400
Hakukuwa na fasihi ya
mtoto kama ilivyo sasa. Kulikuwa na fasihi ya jumla.
Zama
za kati 476-1400
Kulikuwa na simulizi za
kidini, hususani simulizi za kibiblia. Mfano, kulikuwa na habari za mtoto Yesu
na zilihusu sala mbalimbali. zilikuwa zinahusu zaidi maadili. Hakukuwa na
michoro. Simulizi hizi zilikuwa na mchanganyiko wa fantasia na uhalisi.
Kipindi
cha elimu na maarifa 1400-1700
Dhana ya utoto ilianza
kuwaingia watu.
Uhamasishaji wa elimu.
Vitabu vilianza
kuchapishwa.
Kitabu cha kwanza cha
watoto cha picha kilichapishwa na kilitungwa na John Comenius.
Vitabu vingine viliendelea
kutungwa.
Watoto walikuwa angalau
wengi, hata hivyo hawakupewa taswira ya utoto.
1700-1830
Dhana ya utoto ilianza
kuchukuliwa kwa upekee.
Vitabu vingi vya watoto
vilianza kuchapishwa.
John Newberry aliweza
kutunga kitabu kidogo zaidi ambacho kingeweza hata kuwekwe mfukoni.
Wazazi walikuwa wanasomea
watoto vitabu.
1830-1900
Kazi za watoto za
kifantasia zenye ubunifu wa kisasa. Vitabu hivi vilihusu: maadili, kufundisha,
kuburudisha n.k
Lakini pia, kulitokea
hadithi za kweli.
Kuanzia karne ya 20
Hapa ndipo tunapata kazi
zenye ubunifu wa hali ya juu zinazowahusu watoto. Hii yote ni kutokana na watu
kupata elimu.
Fasihi ya watoto nchini Tanzania
Hii inajumuisha kazi za
riwaya, hadithi, ushairi ambazo zinaandikwa. Fasihi andishi ya watoto ni change
kwa sababu haikupewa kipaumbele. Kazi nyingi ziliwahusu watu wazima.
Mulokozi anasema fasihi
andishi ni changa kuliko fasihi simulizi kwa
kuwa uandishi hutugemea fasihi simulizi na ili iwepo ni lazima kuwe na
maandishi. Vilevile fasihi andishi ya watoto ilichelewa zaidi.
Hadithi fupi zilizoonekana
za kwanza zilionekana zilianza kuchapwa miaka ya 1960.
Kupatikana kwa vitabu vya
watoto kuliwezeshwa na mradi wa vitabu vya watoto.
Mulokozi alitunga Ngome ya
Mianzi na Moto wa Mianzi.
Watu mbalimbali
walihamasika kutunga fasihi ya watoto.
Mradi huendesha mashindano
ya usomaji na uandishi.
Kitabu cha kazi ya kwanza
lazima kiwe na picha nyingi zaidi kuliko ngazi ya pili na tatu.
Hivi sasa Tanzania ina
vitabu vingi vya fasihi ya watoto.
Maendeleo ya fasihi ya watoto nchini Tanzania
Fasihi ya watoto si
kongwe. Kabla ya mwambao wa pwani kuingiliwa na wageni, fasihi ya Kiswahili
ilikuwa ni ya kusimuliwa. Maendeleo ya fasihi hususani ya Kiswahili ni suala
lisilojadilika bila kuangalia historia ya Tanzania.
Kipindi kabla ya uvamizi
kulikuwa na simulizi tu. Kipindi cha ujamaa jamii ilikuwa na itikadi ya umoja
na ushirikiano. Hivyo fasihi ilikuwa ya wote. Fasihi haikutofautiana kati ya
ile ya watoto na watu wazima.
Baada ya wageni, mambo
yalianza kubadilika. Mfano kuingia kwa waarabu walioleta hati ya kiarabu na
uislamu.
Fasihi ilikuwa
inafundishwa kupitia mafundisho ya mtume. Hati ya kiarabu ilisaidia katika
fasihi.
Kipindi cha Waarabu
kilikuwa na shujaa wa kijadi maarufu mfano Fumo Lyongo.
Mulokozi 1996.
Tungo mbalimbali
zilitungwa ikiwemo Tumsifu Yangu.
Baada ya Waarabu walikuja
Wareno. Walisaidia kueneza Kiswahili. Walipofika kulitokea mgogoro kati ya
wenyeji na Wareno. Waarabu walisaidiana na wenyeji kupambana na Wareno.
Kipindi hiki kazi
zilitungwa kuonyesha hali ya kuwapinga Wareno, mfano: Mzungu Migeli, Portuguese
Afala. Bado fasihi ili dumisha watoto.
Kipindi cha Waarabu baada
ya kuondoka kwa Wareno. Tenzi mbalimbali ziliibuka. Mfano, utenzi wa
Mwanakupona.
Kipindi cha wageni kutoka
magharibi walileta hati ya Kirumi na dini ya Kikristo.
Kuletwa kwa hati za kirumi
zilisaidia baadhi ya simulizi kuwekwa
katika maandishi, kazi zikaanza kutafsiriwa mfano: Machimbo ya Mfalme Selemani,
Hekaya za Abunuwasi.
Mzungu alionekana bora
kuliko mwenyeji.
Kipindi hiki kulianzishwa shirika la Uchapishaji K.A.M 1948...
Notes Hazijafika Mwisho, Gusa Hapa Kupata Notes Zote kwa Tsh. 2,000/= Tu.