Mtihani wa Kiswahili Kidato cha Nne 2022 1

Mti mkubwa katika ardhi ya kijani.

Endapo Unahitaji Kufanya Mtihani Huu ili Usahihishwe, Wasiliana na Mwalimu Hapa

Muda: Saa 3

Maelekezo

1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na mbili (12).

2. Jibu maswali yote katika sehemu A na B na maswali matatu kutoka sehemu C.

3. Sehemu A ina alama 15, sehemu B alama 40 na sehemu C alama 45.

4. Zingatia maelekezo ya kila sehemu na ya kila swali.

5. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihani.

Sehemu A (Alama 15)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1.   Chagua herufi ya jibu sahihi katika Vipengele (i) hadi (x), kisha andika herufi ya jibu hilo kwenye kijitabu chako cha kujibia.

i.        Ipi ni seti sahihi ya vipera vya fasihi simulizi?

A. hadithi, semi na mizungu  B. hadithi, semi na vitendawili       C. hadithi, semi na mafumbo   D. mafumbo, ngomezi na bembea E. Hadithi, semi na ushairi

ii.        Dhima kuu ya rejesta katika lugha ni ipi?

A. kutangaza lugha duniani kote    B. Kutambulisha watumiaji wa lugha ya Kiswahili        C. Kuongeza maneno mengi katika kamusi      D. kuwapa pumziko watumiaji wa lugha E. kukuza utamaduni wa lugha ya Kiswahili

iii.        Bainisha sentensi yenye muundo wa nomino, kitenzi na nomino:

A. Chakula kimeliwa shuleni. B. Baba amelala darasani. C. wamepigwa kwa sababu ya ujinga wao. D. mtoto anapika ugali. E. Kila kitabu na nabii wake.

iv.        Njia ipi ya uhifadhi wa kazi za fasihi simulizi haipokei mabadiliko ya haraka kati ya hizi?

A. Kichwa B. Maandishi C. kompyuta D. kanda za kunasa sauti E. B C na D ni sawa

v.        “Yooo… yooo… leo nimekuja kutoa nyimbo yangu mpya.” Yapi ni masahihisho ya sentensi hii?

A. Nimekuja kutoa wimbo zangu mpya. B. Nimekuja na nyimbo mpya C. Nimekuja kutoa wimbo wangu mpya D. Nimekuja kuachia nyimbo mpya. E. Nimekuja.

vi.        “Wazee, nahamisha majeshi.” Ni ipi dhima ya mazungumzo haya?

A. Kupunguza ukali wa mazungumzo B. kupunguza hadhira C. kupamba lugha D. kusisitiza mazungumzo E. kufikisha ujumbe barabara

vii.        “Mpishi anapika chakula chake polepole.” Kiima cha sentensi hii kimejengwa na aina gani ya neno?

A. kielezi B. kihisishi C. kitenzi D. kivumishi E. nomino

viii.        Idadi ya silabi nane kati na nane mwisho ambazo hutengeneza jumla ya silabi kumi na sita katika ushairi huitwaje?

A. Vina B. Mizani C. Vituo D. Mistari E. Bahari

ix.        Mambo muhimu ya kuzingatiwa katika uandishi wa kadi ya mwaliko ni yapi kati ya haya?

A. Jina la mwalikaji na jina la ndugu wa mwalikwa B. Mahali pa kukutana na kiasi cha mchango C. Cheo cha anayealikwa na cheo cha anayealika D. Siku ya tukio na jina la anayealika E. Majibu kwa wasiofika na namba ya kukusanya michango

x.        Ni kauli ipi iliyotumika katika uundaji wa neno ‘piga’?

A. kutendama B. kutendesha C. kutendeana D. kutenda E. kutendwa

2.   Oanisha maana za dhana za uundaji wa maneno katika orodha A na dhana husika katika orodha B, kisha andika herufi ya jibu sahihi katika kijitabu chako cha kujibia.

Orodha A

Orodha B

i. bibo

ii. pikipiki

iii. mwananchi

iv. msomi

v. lima

A kutohoa

B miambatano

C mpangilio tofauti wa mofimu

D kufananisha sauti, umbo au sura

E kufupisha maneno

F Urudufishaji

G kuambisha

Sehemu B (Alama 40)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

3.   Tunga sentensi moja kwa kila njeo iliyobainishwa katika vipengele hapo chini:

i. Wakati uliopo mtimilifu

ii. Wakati uliopita

iii. Wakati ujao

iv. wakati uliopo unaoendelea

4.   Kwa kutumia hoja nne, fafanua mambo manne yanayohatarisha kutoweka kwa lugha ya Kiswahili.

5.   Taja mambo manne yanayosababisha utata katika sentensi.

6.   Eleza mambo manne yanayopatikana katika kamusi.

7.   Soma beti zifuatazo kisha jibu maswali yanayofuata:

Tanzania, Tanzania,
Nakupenda kwa moyo wote,
Nchi yangu Tanzania,
Jina lako ni tamu sana.

Nilalapo nakuota wewe,
Niamkapo ni heri mama we,
Tanzania Tanzania,
Nakupenda kwa moyo wote.

a. Taja faida mbili za wimbo huu kwa jamii ya Tanzania.

b. Unadhani ni nani anastahili kuimba wimbo huu? Toa sababu ya jibu lako.

c. Toa mfano wa takriri moja iliyotumika.

d. Unadhani hili ni aina gani ya shairi? Toa sababu moja.

8. Andika barua kwa mtendaji wa kata ya Kishapu S.L.P 123, kuomba kazi ya muda mfupi ya kuhesabu watu-SENSA. Jina lako liwe Jiwe Sanane wa S.L.P 256 Kasulu Kigoma. Barua yako ipitie kwa balozi wa mtaa unaoishi.

Sehemu C (Alama 45)

Jibu maswali matatu kutoka katika sehemu hii.

9. Baada ya kuhitimu elimu ya sekondari, umeitwa kwenye usaili wa nafasi ya kazi katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu cha Dar es Salaam. Katika uthaili umetakiwa kuthibitisha iwapo mhakiki wa kazi za fasihi ana umuhimu wowote katika jamii. Kwa kutumia hoja tano na mifano ya kazi mbalimbali za kifasihi, thibitisha hoja hiyo ili kukidhi haja ya usaili wako.

10. Chagua mashairi matatu kwa kila diwani kutoka katika diwani mbili ulizosoma kisha onyesha jinsi washairi walivyo wakosoaji wa jamii ya leo.

11. Waandishi wa riwaya za Watoto wa Mama Ntilie na Joka la Mdimu wameonyesha kuwa umasikini ni miongoni mwa matatizo yanayozikabili jamii nyingi. Kwa kutumia mifano, eleza mambo matatu yaliyopendekezwa na waandishi kwa kila riwaya yenye lengo la kuzuia umasikini katika jamii.

12. Eleza jinsi uteuzi wa wahusika ulivyoibua dhana ya gonjwa la UKIMWI kwa kutoa hoja tatu kwa kila kitabu kutoka katika tamthiliya mbili ulizosoma.

Endapo Unahitaji Majibu ya Mtihani Huu, Gusa Hapa Kuwasiliana Nami.

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne