Jinsi ya Kuomba Mkopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu

Sarafu ikitumbukia ndani ya kibubu

Bodi ya mikopo ya elimu ya juu (HESLB) hujihusisha na utoaji mikopo kwa wanafunzi wanaotaka kusoma elmu ya juu lakini pengine hawana uwezo wa kumudu gharama hizo hivyo kuhitaji kukopeshwa. Taasisi hii ilianza kufanya kazi mnamo mwaka 2005.

Kwa mujibu wa chapisho la bodi ya mikopo, haya ni maelekezo ya kuzingatia kwa waombaji wote:

Mambo ya kuzingatia kwa waombaji mkopo

Kabla ya kuomba mkopo, hakikisha umesoma maelekezo ya kuomba mkopo.

Namba ya kidato cha nne inayotumika kuomba mkopo, iendane na namba ya kidato cha nne iliyotumika kuomba chuo.

Wanafunzi waliorudia mitihani yao, waorodheshe namba zao zote za mitihani.

Hakikisha kwamba, nyaraka zote unazoambatanisha katika maombi ya mkopo, ziwe zimethibitishwa (verified) na mamlaka husika zinazotambulika.

Hakikisha kwamba, cheti cha kuzaliwa na kifo vithibitishwe na RITA, kwa upande wa Zanzibar, vithibitishwe na ZCSRA.

Vyeti vya kuzaliwa vya wanafunzi waliozaliwa nje ya nchi na vyeti vya vifo kwa wazazi wa Tanzania waliofariki nje ya nchi, vithibitishwe katika barozi za nchi hizo zinazopatikana nchini Tanzania.

Hakikisha kwamba, fomu yako ya maombi imejazwa kwa ukamilifu na imesainiwa kabla ya kutumwa.

Hifadhi nakala baada ya kutuma maombi.

Waombaji wafahamu tarehe ya mwisho ya kutuma maombi.

Tunasisitiza tena kwa mara nyingine kuwa, kabla ya kuomba mkopo, mwanafunzi asome maelekezo yote, japo ni marefu, jitahidi usome yote kwa ukamilifu.

Soma: Jinsi ya Kuomba Chuo

Kwa wanafunzi wanaohitaji usaidizi wa kuombewa mkopo, tunatoa huduma hiyo kwa punguzo la bei. Gharama yetu ni Tsh. 50,000/= tu, mgawanyo wa malipo ni, Tsh. 30,000/= itatumika kama malipo kwa bodi ya mikopo, na Tsh. 20,000/= itatumika kama gharama ya kufanyiwa maombi, Gusa Hapa kuwasiliana na Mwalimu na kuanza kufanyiwa maombi yako.

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne