Mtihani wa Kiswahili 1 Kidato cha Sita 2021 2

Msichana akitazama kompyuta.

Maelekezo ya Kufanya Mtihani Ili Usahihishwe na Mwalimu:

1. Mtu yeyote na popote alipo anaruhusiwa kufanya mtihani huu.

2. Fanya mtihani huu kwa kutumia aina yoyote ya karatasi.

3. Ukimaliza, piga picha karatasi hizo kisha zitume WhatsApp kwenye namba ya Mwalimu Makoba, 0653 250 566.

4. Subiri mtihani wako usahihishwe, Urudishiwe na ufanyiwe masahihisho.

5. Gharama ya mtihani huu ni shilingi 2,000/= (elfu mbili).

Namba za malipo ni: M – Pesa 0754 895 321 (Daud Mhuli) na Tigo pesa 0653 250 566 (Daud Mhuli).

Pata Majibu ya Mtihani Huu, Gusa Hapa Kuwasiliana Nami.

Muda: Saa 3

Maelekezo

1. karatasi hii ina sehemu A na B zenye jumla ya maswali nane.

2. Jibu maswali yote katika sehemu A na maswali matatu kutoka sehemu B. swali la tano ni la lazima.

3. Sehemu A in alama arobaini na sehemu B ina alama sitini.

4. Zingatia maagizo ya kila sehemu na kila swali.

5. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihani.

6. Andika namba yako ya mtihani au jina katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia.

Sehemu A (Alama 40)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Soma kifungu cha habari kifuatacho kwa makini kisha jibu maswali yanayofuata:

Msiba mkuu wa Watanzania ni ufisadi. Ufisadi unaofanywa na viongozi wao unawaumiza na kuwaacha watupu kabisa. Ama hakika, ufisadi unapofanyika, haki ya wananchi hupotea na baada ya muda hupandishiwa kodi ili kufidia.

Watanzania wanawaza ufisadi unaofanywa na viongozi watawezaje kuuondoa. Pengine suluhisho ni kuchagua viongozi wema, lakini utawezaje kutambua kuwa huyu ni kiongozi mwema na huyu ni mbaya? Ni ngumu.

Pengine suluhisho juu ya ufisadi ni mahakama. Lakini mahakama ya mafisadi ipo lakini ufisadi unaendelea. Basi kumbe suluhisho dhidi ya ufisadi ni serikali kufanya mambo yake kwa uwazi, zikiingia pesa fulani, serikali isema, akipewa bwana fulani serikali isema yaani kila linalotendekea, wananchi wataarifiwe. Hii itasaidia kupunguza ufisadi, siyo kuumaliza.

Dawa kamili ya ufisadi ni uzalendo wa viongozi. Viongozi wakiipenda nchi yao zaidi ya wanavyojipenda wao, ufisadi utakwisha.

Maswali:

a. Toa maana ya maneno yafuatayo:

i. Watupu ii. Kodi iii. Watanzania iv. Kiongozi v. Mahakama vi. Uzalendo

b. Fafanua wazo kuu la mwandishi katika aya ya pili.

c. kwa kutumia aya moja, eleza athari za ufisadi katika jamii.

d. Fupisha habari ifuatayo kwa maneno yasiyopungua mia moja.

Kusoma ndiyo mwanzo wa maarifa yote ulimwenguni. Mtu asiyejua kusoma huhesabika kuwa mjinga. Ajuaye kusoma, huwezi kujipatia maarifa mapya yakamsaidia sana katika maisha yake.

Katika nchi yetu, watu hujifunza kusoma wengine wakiwa shule ya msingi na wengine kabla ya elimu ya msingi. Lakini wapo vichwa ngumu ambao humaliza la saba bila kujua kusoma.

Changamoto ya watu wetu ni kwamba, baada ya kumaliza elimu, hukoma kabisa kusoma. Huona kama wamemalizana na jambo la kusoma, lakini kumbe ukweli ni kwamba, mwanadamu safi ni yule asomaye vitabu kila siku ili kujiongezea maarifa yake. Kusoma ni kama hewa, huwezi kujua umuhimu wake mpaka uikose walau kwa dakika moja.

Huko katika mataifa yaliyoendelea sana kwa teknolojia, watu wake husoma vitabu ili kupata maarifa mbalimbali. Husoma vitabu vya fasihi, wakasoma vitabu vya biashara na hata vitabu vya saikolojia. Sasa wayapatapo maarifa hayo, huijenga nchi yao.

2. Bainisha dhima nne za kielezi katika lugha ya Kiswahili.

3. Kwa kutumia mifano, eleza dhana za kisarufi zifuatazo:

a. Mzizi huru b. Fonolojia c. Viambishi d. Sentensi changamano e. Alomofu

4. Toa maana mbili kwa kila sentensi zifuatazo:

a. Mwalimu wetu wa Kichina alitutembelea jana.

b. Bibi Mwanaheri amewachezea jirani zangu.

c. Mtoto wake alimwibia pikipiki.

d. Wizi wa silaha umeongezeka sana siku hizi.

e. Huyu babu ni mpangaji mzuri.

Sehemu B (Alama 60)

Jibu maswali matatu kutoka sehemu hii. Swali la tano ni la lazima.

5. Endapo utaandika kitabu chako na kikatakiwa kufasiriwa, ni sifa zipi utazizingatia kwa mfasiri utakayemwajiri?

6. Andika insha yenye maneno 300 kuhusu muziki wa Tanzania.

7. Watu husema, “Waingereza walikuwa wabaya, lakini walifanya jema moja la kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili.” Thibitisha kauli ya watu hao kwa kutumia hoja sita.

8. Taasisi ya Taaluma za Kiswahili (TATAKI) iliyopo katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, imefanya mengi katika kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili nchini Tanzania. Toa hoja sita kuthibitisha madai haya.

Pata Majibu ya Mtihani Huu, Gusa Hapa Kuwasiliana Nami.

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne