Swali la Ufahamu na Ufupisho Kuhusu Mtu Aliye Muungwana
1. Soma
kwa umakini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu kwa usahihi maswali
yanayofuata.
Wazo
la watu wengi juu ya muungwana ni
kuwa mtanashati au labda kuwa mtu arifu mwenye
cheo kwa watu. Lakini nguo nzuri hazimtukuzi mtu wala hazimfanyi kuwa
muungwana. Fasihi ya hili ni kuwamba, nguo ni kama ngozi ya mtu au mnyama; au
hasa ni duni sana kuliko ngozi au manyoya. Ngozi ya simba haiwezi kumfanya punda
kuwa simba. Uungwana wa kufanywa na mshoni ni mzaha; si uungwana wa kweli. Neno
muungwana lina maana kubwa zaidi kuliko nguo nzuri au adabu nzuri na elimu
nzuri. Kwa hakika twatumia vibaya neno hili kwa mtu yeyote aendaye kwa miguu
miwili.
Kwanza
muungwana hawezi kumuudhi au kumdhuru mtu kwa maneno au matendo yake, hata kwa
kumtazama. Ana moyo wa uvumilivu na anaweza kusikiliza kwa makini maoni ya watu
wengine bila ya kujaribu kuwalazimisha wakubali maoni yake. Ni mkarimu, mnyofu
na amini katika taiba yake kwa wengine. Hapendi kujionyesha alivyo tajiri a
alivyoelimika. Hana makuu wala unafiki, yu mnyofu kwakila asemalo au atendalo.
Hajitwezi kwa matendo yake wala hadunishi matendo ya watu wengine kwa sababu
hana wivu. Haudhi wala hadhuru mtu yeyote kwa sababu ajua kwamba ushenzi kama o
ni kinyume cha uungwana.
Siku
zote muungwana ni mwema kama baba au mama, mwaminifu kama rafiki na msaidizi
kama ndugu. Hutenda tena na kuendekesha kama raia mwadilifu ajuae kazi au
madaraka yake kwa watu. Huchukuana na watumishi wake kwa mapenzi, huruma na
upole. Hujiheshimu na kuwaheshimu wengine. Hivyo basi uungwana wake hautokana
na malezi ya shule ila hutokana na uungwana wa kweli.
Maswali
a) Andika kichwa cha habari hii.
b) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika habari hii.
i. Muungwana
ii. Arifu
iii. Hajitwezi
iv. Mwadilifu
c) Eleza mawazo makuu mawili ya mwandishi.
d) Kutokana na habari uliyosoma, taja tabia tatu za mtu muungwana.
Majibu
B. i. Muungwana ni mtu mwenye adabu na tabia zinazokubalika katika jamii.
ii. Arifu ni mtu mwenye ujuzi mwingi.
iii. Hajitwezi ni kutokujivunjia heshima.
iv. Mwadilifu ni mtu mwenye maadili mema.
c. Mawazo makuu mawili ya mwandishi ni:
Uungwana, mwandishi anataka watu wawe waungwana na waishi vyema katika jamii.
Wazo la pili ni heshima, mwandishi anashauri heshima iwepo kwa watu wote, wakubwa kwa wadogo.
d. Tabia tatu za mtu muungwana ni:
- Mkarimu.
- Hapendi kujionyesha.
- Siyo mnafiki.
2. Fupisha
habari ulisoma kwa maneno tisini.
Jibu
Maana
ya muungwana ipo tofauti zaidi ya watu wanavyodhani. Mtu hawi muungwana kwa
sababu ya mavazi yake. Kutazama mavazi kumewapoteza watu wengi na kujikuta
mikononi mwa watu wabaya.
Muungwana
hatendi mambo mabaya kama: kujikweza, kusema watu vibaya, kusema uongo, unafiki
wizi na mambo yote yasiyofaa. Kwa muungwana, kutenda mambo yasiyofaa ni mwiko.
Muungwana
ni mwema, rafiki na ndugu. Muungwana hujiheshimu mwenyewe na kuwaheshimu watu
wengine. Uungwana ni matokeo ya malezi anayopata mtu nyumbani na shuleni.