SABABU YA MWIZI KUWAPONGEZA POLISI YAJULIKANA

mwizi na polisi

Leo kumeibuka kituko na gumzo baada ya mwizi mmoja kuwapongeza polisi waliomkamata baada ya kuiba fedha katika duka la simu.
Jamaa huyo anayefahamika kwa jina la Boubacar Diallo na ambaye pia ni mwanafunzi katika chuo cha ufundi cha Mamu huko nchini Guinea amezua gumzo kwa kitendo chake cha kulimwagia sifa jeshi la polisi kwa kumkamata.
Baada ya uchunguzi wa masaa kadhaa, hatimaye sababu iliyomfanya jamaa huyo kumwaga kongole kwa jeshi la polisi tofauti na walivyo wahalifu wengine ikajulikana.



SABABU ZAJULIKANA

Jamaa huyo imefahamika kuwa ni mwizi kupindukia na hajawahi kukamatwa kutokana na kuwa na mbinu mbalimbali za kukwepa mkono wa sheria. Hata hivyo, kitendo cha yeye kukamatwa mapema kuliko alivyotarajia ndiko kumemshitua na kumfanya awapongeze polisi kwa ufanisi mkubwa walioonyesha.

AWAOMBEA MSAADA ASKARI

Akihojiwa na waandishi wa habari, jamaa huyo, alisema polisi wanahitaji vifaa vya kisasa zaidi vitakavyowasaidia kufanya kazi zao kwa ufanisi.

Diallo kwa sasa yuko mikononi mwa polisi na amesema anajuta sana kuwa mwizi. Pia, ameahidi kuacha tabia hiyo.






TAZAMA POVU LA MWALIMU MAKOBA KWA WASANII WAVAA HOVYO

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne