Mchango wa Tipu, Bloomfield, Krapf Katika Kueneza Kiswahili

Vitabu
Swali lote linasema, “Onesha mchango wa watu wafuatao katika kukuza na kueneza kiswahili nchini: Tippu Tipu, D.k Ludwig krapf, Broomfield na Askofu Edward steer.”

Watu wengi wamesaidia katika kukua na kuenea kwa Kiswahili nchini Tanzania. Leo tutajadili mchango wa TippuTipu, Krapf, Broomfield na Askofu Edward Steer.

Mchango wa Tippu Tipu katika kueneza Kiswahili

Jina halisi la bwana huyu ni Hamad bin Muhammad bin Juma bin Rajab el Murjeb. Alikuwa mwarabu mfanyabiashara wa watumwa.

Tippu Tipu alisaidia kukua na kuenea kwa Kiswahili kwa sababu, alitumia Kiswahili katika biashara zake. Hivyo, kote alikopita, alieneza lugha ya Kiswahili na ikafahamika kwa watu wengi Zaidi.

Mchango wa D.k Ludwig Krapf katika kueneza Kiswahili

Krapf alisaidia kukua na kuenea kwa Kiswahili kwa sababu alitunga kamusi ya kwanza ya lugha ya Kiswahili. Kamusi hii ilisaidia kuuweka msamiati wa lugha ya Kiswahili katika kitabu kimoja.

Mchango wa Broomfield katika kueneza  Kiswahili

Mtaalamu Broomfield naye hayuko nyuma katika kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili kwani yeye alijihusisha katika usanifishaji wa lugha ya Kiswahili.

Mchango wa Askofu Edward Steere katika kukuza na kueneza Kiswahili

Askofu Edward Steere alitafsiri biblia katika lugha ya Kiswahili. Pia aliandika vitabu vingi vya sarufi ya Kiswahili, miongoni mwavyo ni kile kinachoitwa, ‘A Handbook of the Swahili Language as Spoken at Zanzibar.’

Lugha ya Kiswahili imefika hapo ilipo kwa sababu ya mchango wa watu wengi ambao hawakuchoka katika kuipeleka mbele lugha hii. Wengine walikuza na kukieneza Kiswahili kwa maslahi yao binafsi, na wengine walikuza lugha ya Kiswahili kwa mapenzi yao katika lugha hii. Ni jukumu la watumiaji wote wa lugha ya Kiswahili, kuhakikisha wanaikuza lugha yao na kufika mbali Zaidi.

Mpaka hivi sasa, Kiswahili kinazidi kujizolea umaarufu ikiwemo kutumika katika mikutano mikubwa ya kimataifa, kuimbwa na wanamuziki wengi wa kimataifa, kuandikwa vitabu vingi, kuwa na mitandao mingi inayotumia lugha ya Kiswahili na kingine ni kutumika katika matangazo ya redio nyingi za kimataifa.

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne