Masomo Yaliyofundishwa Mtandaoni na Taasisi ya Elimu 12/05
Mathematics-The Number System Quadrilateral
ENGLISH LISTENING SKILLS PROBLEM SOLVING PART A
Masomo mapya yanawekwa katika ukurasa huu kila siku. Kuona masomo yaliyopita, mengi zaidi, ingia katika channel ya Taasisi ya Elimu huko YouTube.
ENGLISH LISTENING SKILLS PROBLEM SOLVING PART A
Masomo mapya yanawekwa katika ukurasa huu kila siku. Kuona masomo yaliyopita, mengi zaidi, ingia katika channel ya Taasisi ya Elimu huko YouTube.
Kufuatia
shule kufungwa nchini kwa sababu ya ugonjwa wa Korona, Taasisi ya elimu imeamua
kutoa masomo kwa njia ya mtandao ili kuweza kuwasaidia wanafunzi wote nchini Tanzania.
Nchini
Tanzania, madarasa yanayotegemea kufanya mtihani mwaka huu ni: darasa la nne,
darasa la saba, kidato cha pili, kidato cha nne na kidato cha sita. Hata hivyo, masomo hayatolewi kwa vidato vinavyofanya mtihani pekee, bali yanatolewa kwa vidato vyote.
Masomo
yanatolewa kwa kutumia televisheni na mtandao. Bila shaka mpango huu utawafaa
sana wanafunzi ambao wako nyumbani kufuatia kufungwa kwa shule.
Wanafunzi wawapo nyumbani, wazingatie ushauri wangu huu:
Kwanza,
wajilinde na ugonjwa wa korona kwa kufuata ushauri wa wataalamu ikiwemo: kunawa
kwa maji tiririka na sabuni, kutumia vitakasa mikono, kuepuka mikusanyiko na
kanuni nyinginezo.
Pili,
wajisomee, mwanafunzi anashauriwa afuate ratiba ileile aliyokuwa nayo shule.
kama ulikuwa unaingia darasani saa mbili asubuhi, basi hapohapo nyumbani anza
kujisomea saa mbili asubuhi. Kama muda wa mapumziko ilikuwa saa nne asubuhi,
nawe pumzika saa nne asubuhi. Kwa kifupi ni kwamba, fuata ratiba ya shule ukiwa
hapohapo nyumbani.
Jambo
la tatu, wanafunzi wasiwe na hofu. Hata kama upo kidato cha mtihani, amini
kwamba, kufungwa kwa shule siyo sababu ya wewe kufanya vibaya katika masomo
yako. Utafanya vizuri, muhimu ni kuutumia vizuri muda huu ukiwa nyumbani.
Kanuni
za kufaulu mitihani yako bado zipo palepale: kanuni ya kwanza ni kufundishwa,
masomo yanafundishwa kwa njia ya mtandao.
Kanuni
ya pili ni kujisomea, tayari nimesisitiza uutumie muda wako vizuri hapo
nyumbani kwa kujisomea.
Kanuni
ya tatu ni kufanya maswali ya mwalimu, katika masomo maswali yanatolewa, hivyo
fanya maswali hayo.
Kanuni
ya nne ni kufanya mitihani ya mwalimu, ipo mitihani mingi online unaweza
ukafanya kadri unavyotaka.
Kanuni
ya tano ni kupitia mitihani iliyopita, ipo mitandao mingi ina mitihani
iliyopita, tembelea mitandao hiyo kujipatia nakala ya mitihani iliyopita.
Kanuni
ya sita ni kusoma notes au vitabu sahihi, natumaini una notes na vitabu sahihi
kama huna tafuta sasa.
Kanuni
ya mwisho ni kuzingatia muda, hii nimeisisitiza mwanzoni kuwa unatakiwa
kuzingatia muda uwapo nyumbani wakati huu. Ratiba ya shule, ihamishie nyumbani.