Tabia Nzuri Zinazosaidia Kukamilisha Mipango Mbalimbali

Plan board.
Mipango lazima ikamilike. Lakini inawezekana mipango yako haikamiliki kwa sababu umekosa tabia hizi ninazokufundisha leo:

     1.   Amka muda unaofanana kila siku

Wikendi, sikukuu na siku ya kuzaliwa zikiwemo. Bila kujali umelala saa ngapi leo, amka muda uleule siku zote. Kama unaamka saa 12 asubuhi, basi iwe hivyo kila siku. Kama unaamka saa mbili asubuhi, iwe hivyo.

     2.   Soma vitabu

Vitabu vitakufanya ujifunze mambo mbalimbali. Maarifa mengi yamefichwa vitabuni, usiache kuyapata.

     3.   Tafakari siku yako

Fikiria siku iliyopita umefanya nini, pia fikiria siku ya leo utafanya nini na siku ya kesho utafanya kitu gani. Weka mipango ya siku ijayo na ikumbuke siku iliyopita.

     4.   Orodhesha mambo ya kufanya kwa siku husika

Orodhesha mambo unayotakiwa kufanya katika siku husika. Kama siku hiyo umepanga kuangalia filamu, kuchat na marafiki, kusoma kitabu na kwenda kufanya mazoezi andika. Ukiandika itakusaidia kufanya kazi kwa utulivu bila kutafakari ni kitu gani kingefuata baada ya kazi uliyonayo kukamilika.

     5.   Zungumza na mtu anayekuzidi katika kitu fulani

Mara mojamoja, jaribu kukaa na watu wanaokuzidi katika mambo fulani. Kama ni mwanafunzi, kaa na wanafunzi wenzako wanaofanya vizuri zaidi. Kama ni mfanyabiashara, kaa na mtu anayefanya biashara vizuri kukuzidi, muhimu kuwa na mtu ambaye ni bora katika jambo fulani. Kuwa naye kutakufanya ujifunze vitu vingi kutoka kwake.

     6.   Cheka angalau mara moja kwa siku

Tazama video za kuchekesha, tazama vituko vya mtandaoni, na unapokuwa peke yako, kuwa kama mtoto. Jitahidi ucheke mara nyingi uwezavyo kwa siku, lakini kama mara nyingi haiwezekani, basi cheka angalau mara moja. Nakukumbusha kuwa, ni rahisi kucheka kuliko kulia!

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne