Mtihani wa Kiswahili 2 Kidato cha Sita 2020 2 Fomati Mpya


Kitabu kimefunuliwa kurasa.

Maelekezo ya Kufanya Mtihani Ili Usahihishwe na Mwalimu:

1. Mtu yeyote na popote alipo anaruhusiwa kufanya mtihani huu.
2. Fanya mtihani huu kwa kutumia aina yoyote ya karatasi.
3. Ukimaliza, piga picha karatasi hizo kisha zitume WhatsApp kwenye namba ya Mwalimu Makoba, 0754 89 53 21.
4. Subiri mtihani wako usahihishwe, Urudishiwe na ufanyiwe masahihisho.
5. Gharama ya mtihani huu ni shilingi 2,000/= (elfu mbili).
Namba za malipo ni: M – Pesa 0754 89 53 21 (Daud Mhuli) na Tigo pesa 0653 25 05 66 (Daud Mhuli).

Muda: Saa Tatu

Sehemu A (Alama 40)

Jibu maswali yote

    1.   Orodhesha dhima nne za tamthiliya ya Kiswahili tangu kupata uhuru mpaka hivi sasa.

    2.   Jadili kwa ufupi dhima nne za mhakiki wa kazi za fasihi.

   3.   Kwa kutumia mifano, jadili kwa ufupi jinsi uandishi wa riwaya ulivyoisaidia jamii yetu. Toa hoja tano.

    4.   Soma kwa makini habari hii kisha jadili vipengele vya fani vilivyotumika:
“Mako, nirejeshe nyumbani, njia iko wapi?” aliuliza Chimota bila ya salamu. Sikuijua njia ya kurejea nyumbani, nikamtazama nikitabasamu kisha nikamjibu,
“Siijui njia, nilijikuta niko huku kwa ulozi wa babu yako, sifahamu kabisa nilifikaje maeneo haya.” Jibu hili lilikuwa baya kabisa kwa Chimota, alikosa matumaini akakaa chini kwa huzuni. Bila shaka aliyachoka maisha ya mapambano, alichoka kukaa msituni akiwindwa, alitamani kuwa sehemu salama nyumbani kwa babu yake.
Tukiwa tumekaa pale tukitafakari namna ya kurejea nyumbani, tulisikia muungurumo wa kitu kama ndege. Vumbi jingi likatimka. Chimota aliitazama kwa tahadhari, akataka kushambulia, lakini nikamkamata mkono wake kumsihi asubiri kwanza tuone ni nani alikuwa akielea katika chombo hicho.
Chombo kilizidi kushuka chini mpaka kikawa sawa na urefu wangu nikisimama wima, ndani ya Chombo hicho mzee mwenye nywele nyeupe akachungulia, alikuwa Samike. Mimi na Chimota tukatazamana kwa furaha, Chimota alimkumbuka babu yake, hakumsahau!
Amri ilitoka ikitutaka tuingie chomboni, nami nikamshika Chimota, nikamuingiza humo, kisha nikafuata mwenyewe. Sasa tukawa watu watatu ndani ya chombo kilichopaa. Tulitazamana kwa nyuso za furaha isiyo kifani. Naye mzee akatamka, “sasa tunarejea nyumbani.” kisha akakichochea chombo tayari kwa safari.
Lakini kabla chombo hakijachochewa sawasawa, Chimota akamshika mkono babu yake, akanena kwa sauti tulivu, “hatuwezi kurejea nyumbani, mama yupo huku, lazima tumuokoe!”
“Mama yako alikufa, kafikaje huku?” Samike aliuliza. Kabla Chimota hajatoa maelezo, tulimuona msichana akikimbia kuomba msaada, nyuma, alifukuzwa na askari waliopanda fisi. Samike alimtambua msichana yule, alikuwa mtoto wake wa pekee. Chimota alimtambua msichana yule, alikuwa mama yake mzazi. Nami nilimtambua msichana yule, alikuwa mpenzi mpya niliyempata matekani!
Chimota hakutaka mchezo mbele ya binti yake, akarusha kombola kali, askari na fisi wakaanguka chini. Kama ilivyokawaida yao, wachache waliobaki, wakarudi nyumbani!
Tulimchukua binti yule, alipokaa, tukatazamana kwa aibu! Samike akaondoa chombo kwa kasi, mengi aliyokuwa nayo, angeyasema tukifika, hakutaka kuzungumza, alijali usalama wetu. Nami nikawaza, “sasa nimepata mke, mimi si popo tena, mimi ni shujaa Mako!”

Sehemu B (Alama 60)

Jibu maswali matatu. Swali moja lazima litoke katika ushairi.

    5.   “Waandishi wana kazi moja tu, kupiga vita mambo yanayozuia maendeleo ya jamii.” Jadili ukweli wa kauli hii kwa kutumia diwani mbili ulizosoma. Hoja tatu kwa kila diwani.

    6.   Jadili miundo mitatu tofauti ya mashairi kwa kila diwani kati ya diwani mbili ulizosoma.

    7.   Jadili dhamira zenye uhalisia katika riwaya mbili ulizosoma. Tumia hoja tatu kwa kila kitabu.

    8.   Chagua wahusika wawili kutoka kila tamthiliya, kisha eleza wasifu wao. Toa hoja tatu kwa kila kitabu.

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Sifa Bainifu za Irabu ya Kiswahili Sanifu