Posts

Showing posts from May, 2018

Uhakiki wa Tamthiliya ya Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe

Image
JINA LA KITABU: NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE MWANDISHI: EDWIN SEMZABA Mhakiki: Mwalimu Makoba Utangulizi Afisa aliyetumwa kuhesabu watu-Ngoswe, anashindwa kuifanya kazi yake na kuanzisha ajenda nyingine ya mapenzi. Anapanga kutoroka na binti Mazoea aliyekwisha kuposwa tayari, Mazoea naye kusikia atakwenda kuishi mjini anakubaliana na mpango huo. Wanapotoroka, Ngoswe anasahau mkoba wenye takwimu za watu waliokwisha kuhesabiwa, Mzee Ngengemkeni Mitomingi ambaye ndiye baba yake na Mazoea, anazichoma moto takwimu hizo na kumsababishia hasara kubwa Ngoswe. J ina la Kitabu Jina la kitabu “Ngoswe penzi kitovu cha uzembe” ni jina ambalo limesawiri vyema yaliyomo ndani ya kitabu hicho, kwani Ngoswe ndio jina la mhusika mkuu anayebeba dhamira kuu ya tamthiliya. Pia penzi limeonekana kuwa ni kitovu cha uzembe kwani ndio yaliyopelekea kuteketezwa kwa karatasi za takwimu za sensa. Hivyo jina la kitabu si tu kwamba limesawiri yaliyomo katika kitabu bali pia katika jamii. Maudhui ...

History Examination for Form Four| Pre NECTA| 26 May 18

Image
Endapo Unataka Kufanya Mtihani Huu ili Usahihishwe na Mwalimu Makoba, Zingatia Mambo Haya: 1. Mtu yeyote na kokote aliko anaruhusiwa kufanya mtihani huu. 2. Fanya mtihani huu kwa kutumia aina yoyote ya karatasi. 3. Ukimaliza, piga picha karatasi hizo kisha zitume WhatsApp kwenye namba ya Mwalimu Makoba, 0754 89 53 21. 4. Subiri mtihani wako usahihishwe, Urudishiwe na ufanyiwe masahihisho. 5. Gharama ya mtihani huu ni shilingi 2,000/= (elfu mbili) tu. Namba za malipo ni: M – Pesa 0754 89 53 21 (Daud Mhuli) na Tigo pesa 0653 25 05 66 (Daud Makoba) “Kwa kuwa lengo la mtihani huu ni kutaka kujua uwezo na mapungufu ya mwanafunzi ili aweze kupewa mbinu mbadala za kumsaidia kufaulu mtihani wake wa mwisho, kuangalizia majibu hakuna faida yoyote kwani lengo la mtihani si kubaini nani atakuwa wa kwanza na yupi atakuwa wa mwisho!” Mwalimu Makoba| Mwalimu wa Waalimu na Wanafunzi| Mwalimu wa Ushindi! Sasa fanya mtihani wako... Answer all questions Use 2.30 ...

Vichekesho Haviishi Miaka Yote, Soma Hivi Vipya

Image
Masihara ya Watanzania Tanzania ndio nchi pekee duniani mtoto anauliza akitaka kuwa Rubani afanyaje anaambiwa alale kwenye chandarua chenye dawa... Timbwili la Mke wa Kibongo Tofauti ya Mke wa Kizungu na mke wa Kibongo pale ambapo Mwanaume wake atokapo kuoga. Mke wa Kizungu: Baby you look nice and fresh. Mke wa Kibongo: Naona safari imeiva, Mwanaume hupumziki kama nesi wa zamu. Dalili ya Vyuma Kukaza Mwezi wa 11 mwaka uliopita, kuna mtu alinitumia Tshs 50,000/= akapandishwa cheo kazini. Rafiki yangu wa zamani akanitumia Tshs 75,000/= akashinda bahati nasibu. Mwingine akanitumia Tshs 100,000/= muda si mrefu akaolewa.               Sikwambii unitumie hela ila fikiria baraka walizopata walionitumia hela baada ya hapo fanya maamuzi SAHIHI... Mbaazi na Makopo Kilo ya Mbaazi Tsh 300 na Kilo ya Makopo Tsh 450. Sasa utachagua mwenyewe ulime Mbaazi au uokote Makopo �

English Examination for Form Four| Pre Necta 3

Image
Endapo Unataka Kufanya Mtihani Huu ili Usahihishwe na Mwalimu Makoba, Zingatia Mambo Haya: Mtu yeyote na kokote aliko anaruhusiwa kufanya mtihani huu. Fanya mtihani huu kwa kutumia aina yoyote ya karatasi. Ukimaliza, piga picha karatasi hizo kisha zitume WhatsApp kwenye namba ya Mwalimu Makoba, 0754 89 53 21. Subiri mtihani wako usahihishwe, Urudishiwe na ufanyiwe masahihisho. Gharama ya mtihani huu ni shilingi 2,000 (elfu mbili) tu. Namba za malipo ni: M – Pesa 0754 89 53 21 na Tigo pesa 0653 25 05 66 “Kwa kuwa lengo la mtihani huu ni kutaka kujua uwezo na mapungufu ya mwanafunzi ili aweze kupewa mbinu mbadala za kumsaidia kufaulu mtihani wake wa mwisho, kuangalizia majibu hakuna faida yoyote kwani lengo la mtihani si kubaini nani atakuwa wa kwanza na yupi atakuwa wa mwisho!” Mwalimu Makoba| Mwalimu wa Waalimu na Wanafunzi Sasa fanya mtihani wako... SECTION A (10 Marks) COMPREHENSION AND SUMMARY 1.  Read the passage below carefully and...