Mwanamke Uliyekula Pesa Zangu Nakutafuta | Sehemu ya Tano

Mbabe gizani
Baada ya siku tatu bila kupita mitaa yake Asi huko Mwananyamala ndanindani, nilipita tena ili niweze kumuona msichana huyu. Hali ilikua tofauti kuliko siku zote, msichana hakuwepo. Nilitazama kama kweli ni nyumba ileile ambayo tangu nianze kupita sijawahi kumkosa akiwa kakaa kibarazani, ilikuwa nyumba ileile na msichana hakuwepo. Hata hivyo sikuwa na wasiwasi, nilihisi huenda alikuwa na kazi humo ndani.

Nilipita tena siku iliyofuata, msichana hakuwepo. Nikapita siku nyingine, hakuwepo, nikapita tena na tena mpaka chovya chovya ikamaliza buyu la asali, lakini msichana hakuwepo. Hapo nikapatwa na hofu, hofu ya kupotea kwa mwanamke aliyekula pesa zangu. Shilingi halali za Kitanzania elfu kumi na tisa. Pengine hazikuwa zile pesa, kwani ni pesa kidogo sana zisizotosha hata kununua simu ndogo ya Kichina, pengine nilianza kumpenda Asi, binti mdogo aliyekuwa na tabasamu pana, mwepesi kuzoea watu tena aliyechangamka vyema. Basi baada ya pitapita ya siku nyingi bila kumuona, nikaahidi kumtafuta mpaka nimpate.

Soma: Mwanamke Uliyekula Pesa Zangu Nakutafuta |Sehemu ya Sita


Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne