Sababu Wanafunzi wa Kike Kutofanya Vizuri kama wa Kiume

Mwalimu na wanafunzi wawili

Wanafunzi wa kiume na wale wa kike hawana tofauti katika akili zao. Ukweli ni kwamba, wanafunzi wa kike hufanya vizuri zaidi wawapo katika madarasa ya chini, na huendelea kushuka uwezo wao wa kufanya vizuri kadri wanavyozidi kuongeza madarasa. Akili ya mwanamume na mwanamke zote zipo sawa. Lakini kumekuwa na utofauti mkubwa wa ufaulu wa wanafunzi wa kike na wale wa kiume. Lakini wapo wasichana ambao pamoja na yote, bado wanafaulu vizuri kuliko wale wa kiume, hapa tutaeleza, kwa nini wanafunzi wa kiume hufaulu zaidi ukilinganisha na wale wa kike.

1.   Hofu ya kufanikiwa

Wasichana hutengenezewa hofu ya kufanikiwa tangu wakiwa watoto. Kutokana na tamaduni zetu, wasichana huona kama ni kosa kupigania mafanikio, hata wanapofanikiwa, hufananishwa na wale wa kiume.

Mwanafunzi wangu mmoja aitwaye Helena aliwahi kunisimulia mkasa wake ulionisisimua vilivyo. Anasema akiwa darasa la kwanza, alikuwa akifanya vizuri darasani na kushika nafasi ya kwanza. Watu wengi walimsifu kwa kuwashinda wanafunzi wenzake wa kiume. Watu haohao waliomsifia, waliwacheka na kuwadhihaki wanafunzi wa kiume wa darasa lake kwa kushindwa na msichana.

Alipofika darasa la tatu, walimu walikuwa wakiingia darasani na kuwasema vibaya wanafunzi wa kiume. Walikuwa wakiwahoji kwa nini wanakubali kushindwa na mwanamke. Helena hakujisikia vizuri, aliona kama hakuwa na haki ya kufanya vizuri kuliko wanafunzi wa kiume.

Mambo hayakuishia hapo, walimu walianza kuwaadhibu kwa viboko wanafunzi wa kiume kila walipozidiwa naye. Hali hii ilimtengenezea hali ya chuki Helena na wanafunzi wa kiume. Wapo baadhi ya wanafunzi watukutu ambao walithubutu kumfuata na kumuonya kuwa endapo ataongoza tena, wakichapwa viboko nao watamshikisha adabu. Kuona hivyo, Helena aliamua kuanza kujiferisha makusudi katika mitihani. Wakati alipofanya vizuri maneno mengi yalisemwa kumuelekea, alipofanya vibaya na darasa kuongozwa na mwanafunzi wa kiume, walimu walipongeza kwa kusema, wanaume wa darasa wameamka!

2.   Matabaka ya ushindani

Yapo matabaka ya ushindani yanayotofautisha jinsia. Huu ni utaratibu ambao hutenganisha wanafunzi wa kiume na wale wa kike. Utasikia wataalamu wa elimu wakisema, aliyeongoza upande wa wasichana ni fulani bin fulani. Jambo hili ni baya na linamfanya msichana ahisi kama yeye hapaswi kushindana na mwanamume.

Yapo mengi, mengi tena mengi, mengine unayoyafahamu, ongeza.

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Vichekesho vya Kuchekesha na Kuvunja Mbavu 1