Vichekesho vya Kuchekesha na Kuvunja Mbavu 2
1. Chomoa hela kidogo kwenye ada ya mwanao kisha kunywa bia. Elimu haina mwisho.
2. Mtu unamdai halafu
anakujibu kwa kiingereza.
3. Kuna mwizi amekamatwa
hapa amepewa kipigo. Anaulizwa ataje mwenzake anaanza kuniangalia mimi,
nimempiga bonge la kofi.
4. kukosa hela vibaya sana,
hata ndoto unazoota zinakuwa hazikuheshimu. Mimi kweli ni wa kuota nakimbizwa
na Kinyonga!
5. Nilikuwa siamini kama
kila kitu kinawezekana hapa Duniani mpaka siku nilipoota nakimbizwa na konokono.
6. Usikate tamaa kwa sababu
kakuambia ana mtu wake. Watu hufariki.
7. Mjomba katoka kijijini,
nipo naye katika mgahawa, naagiza chipsi kavu kwa ajili yake na mimi, chipsi
zinaletwa. Baada ya kula mara tatu mjomba anavunja ukimya.
“Mjomba,” mjomba ananiita.
“Naam,” naitika nikila
chipsi zangu.
“Uliagiza chipsi kavu?”
“Ndiyo.”
“Sasa kwa nini zina mafuta
mafuta?
Nilitumia dakika tisini
kumuelewesha.
8. Nilialikwa na jamaa kula
chakula cha mchana nyumbani kwake. Nilipofika nikakutana na watu wengine
waliokuwa nao wamealikwa. Tulipoanza kula, jamaa akachukua simu yake, akapiga ‘video
call’ kwa rafiki yake, ‘video call’ ilipopokelewa akasema,
“Unaona kaka, ni kawaida
yangu kabisa kula na masikini… unawaona!”
Nilitafakari nisuse chakula
au niendelee. Nikaamua niendelee tu kwa sababu kama kudhalilika tayari
nimeshadharirika.
9. Niliachwa na mpenzi kwa
sababu ya ajabu sana. Alikuja kunitembelea kisha akaniomba nimpeleke sehemu
ambayo hajawahi kupelekwa. Basi nikampeleka kumtembeza makaburini. Tuliporudi akasema
hawezi kuwa na mahusiano na mchawi, akaniacha.
10. mwaka mmoja nilivamiwa
na chatu mkubwa nyumbani kwangu. Nikawapigia simu watu wa maliasili kuwa, waje
kumchukua ndani ya dakika arobaini na tano, wasipofanya hivyo wasije. Walichelewa
kuja, wakakuta mimi na familia yangu tunakula mishkaki ya chatu.
11. Alikuwa mfupi,
nikampenda hadi akarefuka, lakini bado aliniacha mpuuzi yule.
12. Bidii uliyonayo katika
kupigania mahusiano yako yasife, ukiiweka kwenye kazi unakuwa bilionea.
13. Walisema mapenzi
hayachagui umri, cheo wala kabila, lakini hawakusema hayachagui sheria, hivyo
tukikukamata una mahusiano na mwanafunzi tunakufunga.
14. Nguvu unazotumia kupigania mahusiano yako yasife, ukizihamishia kwenye kilimo unalisha Afrika nzima.