Matumizi ya Kiambishi ‘kwa’ | Matumizi ya Mofimu
Kiambishi
‘kwa’ kina matumizi mengi, yafuatayo ni baadhi tu ya matumizi hayo:
1.
Kuonesha
umiliki wa mahali
Tazama
mifano:
Shangazi
amekwenda kwa mjomba.
Musa
amelala kwa baba.
Simba
amepeleka maji kwa sungura.
Ongeza
mifano Zaidi.
2.
Kueleza
sababu
Mifano:
Umepigwa
kwa kuiba kuku.
Umehukumiwa
jela miaka mitano kwa kutukana watu.
Amekufa
kwa kujinyonga.
Jaribu
kuweka mifano yako mingine.
3.
Kuonesha
sehemu ya kitu kizima
Mifano:
Amepata
tano kwa mia moja.
Musa
ana akili sana, katika mtihani amepata sabini na tano kwa mia.
Yahaya
ana jitahidi, amepata saba kwa tisa.
Endapo
umeelewa dhima hii, weka mifano zaidi.
4.
Kuonesha
muda uliochukuliwa na tendo fulani
Mifano:
Tulimsubiri
kwa saa tisa.
Walishauriana
kwa saa saba.
Walikesha
kwa siku mbili wakila nyama na kucheza mziki.
Ongeza
mifano mitatu zaidi.
5.
Kulinganisha
Mifano:
Timu
ya taifa ilishinda mbili kwa moja.
Simba
ilifungwa tano kwa nne.
Timu
ile haina kitu, imefungwa tatu kwa sifuri.
Fanya
mazoezi ya kuongeza mifano zaidi ili utambue kama umeielewa dhima hii.
6.
Kuelezea
kifaa kinachotumika
Shabani
ni tajiri kwelikweli, analima kwa jembe la dhahabu.
Anavuna
karanga kwa koleo.
Jimotoli
anachota maji kwa ndoo.
Fanya
mazoezi ya kuongeza matumizi mengine, kisha mshirikishe mtu mwenye ujuzi
akusahihishe.
7.
Kueleza
jinsi, namna au mbinu
Anna
alipata pesa kwa kuuza vitenge.
Ntobi
alikimbia kwa nguvu.
Manege
anacheza kwa madaha.
Katika
dhima hiyo, fikiria mifano mingine zaidi ili kupima uelewa wako.
Hayo
ndiyo matumizi ya kiambishi ‘kwa’. Katika lugha ya Kiswahili, vipo viambishi
vingi na kila kiambishi kimekuwa na matumizi yake.
Wanafunzi
wengi hukumbwa na changamoto ya kushindwa kutambua matumizi ya viambishi na
kujikuta wakitoa majibu ya kubuni, inashauriwa kuwa, ili utambue matumizi ya
kiambishi fulani, basi kifanyie mazoezi kiambishi hicho kwa kukiweka katika
sentensi tofauti, ni uhakika wangu kuwa, utaweza kuyaona matumizi ya kiambishi
chochote. Hakuna sababu ya kushindwa.