Mitindo Rahisi Tisa ya Maisha kwa Wanafunzi
Kwa
mwanafunzi, siyo rahisi kupata mitindo ya maisha iliyosahihi kwa afya ya mwili
na akili. Hapa nimekuwekea mitindo sahihi itakayokufanya uwe na afya bora
wakati ukifurahia masomo yako.
1.
Usile
kupita kiasi
Hata
kama hukula chakula cha mchana, haina maana ule kupita kiasi ili kulipa chakula
ambacho hukula. Kula kwa kiasi ni jambo jema na kula kupita kiasi ni hatari kwa
afya yako.
2.
Kula
mboga za majani
Kula
viazi, mahindi, mboga na vyakula vyenye protini kama samaki na maharage.
3.
Usinywe
pombe
Unywaji
wa pombe kupita kiasi hauwezi kukufanya mwenye afya. Pia epuka kula vyakula
vyenye sukari kupita kiasi, vyakula hivi ni chanzo cha maradhi na husababisha
unenepe.
4.
Weka
malengo
Unapofanya
jambo bila kuweka malengo, huwezi kuwa na ari ya kufanya jambo hilo. Weka
malengo katika kila jambo unalofanya, kwa mfano kama unafanya mazoezi, weka
malengo, malengo ya kufanya mazoezi yanaweza kuwa: kupunguza unene, kuwa na
afya, kuondoa hofu au malengo mengine.
5.
Fanya
mazoezi mara kwa mara
Mazoezi
yanatufanya wenye afya. Hata mimi hufanya mazoezi, kwa sababu ya kazi nyingi,
ratiba yangu ya mazoezi ni rahisi. Unaweza kufuata ratiba yangu? Jumapili huwa
nakimbia kiasi cha kilometa 8. Jumatatu sifanyi mazoezi. Jumanne asubuhi pale
ninapoamka hupiga pushapu ishirini, huruka kamba mara 200 na hufanya mazoezi ya
kukata tumbo. Jumatano na alhamisi sifanyi mazoezi, Ijumaa nafanya mazoezi yale
niliyofanya Jumanne. Jumamosi sifanyi mazoezi kisha jumapili nafanya zoezi lile
nililokwambia, kukimbia kilomita 8.
6.
Fanya
jambo moja kwa wakati
Ni
bora kufanya jambo moja ukalikamilisha kisha ukafanya jambo jingine. Ukifanya
mambo mengi kwa wakati mmoja, kuna hatari ya kufanya makosa mengi na kushindwa
kuyamaliza mambo hayo. Kama unasoma, tumia muda huo kusoma na siyo kuchat na
marafiki.
7.
Tumia
mbinu sahihi kupambana na msongo wa mawazo
Huwezi
kuuzuia msongo wa mawazo, hofu na mawazo mabaya. Hata hivyo, unaweza kupambana
na vitu hivi hata visiweze kukusumbua. Njia mojawapo ni kujumuika na marafiki,
kuzungumza na mtu na tiba nyingine ni kufanya kazi yoyote.
8.
Usiache
kulala
Wanafunzi
wengi hudhani kukesha wakisoma ndiyo kupata maarifa. Unakosea sana kama
unafanya hivi. Miili yetu huhitaji kupumzika kwa kupata usingizi. Hivyo,
hakikisha unalala na kamwe usikeshe ukisoma.
9.
Kitanda
chako kiwe sehemu ya kulala pekee
Usifanye jambo lolote kitandani isipokuwa kulala. Usisome
kitandani wala kutumia simu yako, ukifanya hivyo, utafanya kitanda chako kiwe
sehemu mpya ya msongo wa mawazo.