Jinsi ya Kuongeza Kujiamini
Kushindwa
kujiamini ni sababu ya watu wengi kushindwa kupata mafanikio. Inawezekana hukufanya
ile biashara ambayo sasa imemtajirisha fulani kwa sababu wewe hukujiamini
ulipokuwa na wazo hilo. Unaweza kukosa mengi kwa kushindwa kwako kujiamini. Endapo
unataka kuongeza uwezo wa kujiamini, fanya mambo haya:
1.
Acha
uongo
Unashusha
heshima yako pale unaposema uongo. Siku zote zungumza ukweli hata kama hauna
faida kwako.
2.
Kuwa
makini na ahadi zako
Kama
ukisema utafanya jambo fulani, lifanye jambo hilo. Unatakiwa kuwa mtumwa wa
maneno yako. Kujiamini kunakuja pale unapoaminika, je unaweza kumuamini mtu
anayekudanganya? Bila shaka hapana. Timiza ahadi zako, itaongeza uwezo wa
kujiamini.
3.
Kuwa
na watu wanaojiamini
Ukizungukwa
na panya, na wewe utakuwa panya. Siku zote zungukwa na watu wanaojiamini, nawe
utajiamini.
4.
Badili
fikra zako
Je
fikra zako zinakujenga au zinakubomoa? Kama zinakubomoa, badilisha fikra zako. Fikria
mambo mazuri na si mabaya.
5.
Weza
kitu fulani
Ukiweza
utajiamini. Ongeza uwezo wa kufanya kitu fulani. Inaweza kuwa: kufundisha,
kupaka rangi,kutengeneza vitanda na mambo mengine mengi. Yote haya kama
huyawezi kwa ufasaha, ni lazima uwe na hofu. Ukiyaweza, utajiamini.
6.
Fanya
mambo yanayokutisha
Safiri.
Hutubia. Jifunze kucheza muziki. Fanya mambo yanayokutisha.
Kwa kuzingatia
mambo hayo, natumaini uwezo wako wa kujiamini utaongezeka na kukupeleka katika
mafanikio ya kweli ambayo kwa muda mrefu umeyakosa kwa sababu ya kukosa kujiamini.