Nimefanya tafiti kwa kipindi kirefu tangu ajira za ualimu zianze kupatikana kwa usaili. Katika tafiti hizo, nimegundua mengi ambayo nitakuleza ili nawe uweze kutumia ushauri wangu na uweze kufaulu mitihani hii, uwe selected! Vijana wengi wanaoomba ajira sasa wanaelekea kuamini mfumo hauko sawa, wanahisi kuna mchezo wanachezewa! Wanahisi pengine alama zile siyo zao na huenda matokeo yale yanatungwa sehemu. Sikuliacha hivihivi jambo hili, niliamua kuingia katika utafiti mimi mwenyewe, kwa kuwa kigezo ni vyeti na umri na wala hawajali sasa unafanya kazi wapi nilijisajili, nikachaguliwa kufanya masomo mawili, mtihani wa kwanza nilipangwa kufanyia chuo cha Kampala International, na mtihani wa pili nilipangwa kufanyia NIT. Kwa kuwa nilikuwa katika utafiti, nilijibu maswali yale tu ambayo nina uhakika wa asilimia 100 kuwa yalikuwa sahihi, maswali ambayo yalikuwa na utata sikuyajaza. Nilipotoka kwenye mtihani nilitambua kabisa kwamba lazima nipate alama fulani, matokeo yalipotoka, ilikuja ala...
Tumekukusanyia mkusanyiko wa vichekesho vinavyochekesha sana. Vichekesho hivi, vitakufanya ufurahi muda wote, ni vizuri zaidi, uki’share’ na wenzako. 1. Huu mwezi mwenye nyumba aje atoe nyumba yake kwenye vitu vyangu, sina kodi. 2. Nimetoa vyombo nje nifanye usafi, kurudi naambiwa gari la taka limebeba. 3. Kwa jinsi maisha yalivyo magumu siku hizi unajikuta wewe ndiyo unamuamsha jogoo. 4. Chakula chenyewe unakipata kwa mateso halafu bado unakiwekea pilipili, una tatizo gani mkuu? 5. Mtu anakuja kuniomba elfu 20 kweli! Unaniombaje nusu ya utajiri wangu? 6. Daktari: Bia inatanua moyo. Walevi: imeshindwa kutanua chupa itatanua moyo? 7. Nimeota nakula tambi, kuamka sizioni "earphone" zangu. 8. Taja faida kwa nini unaishi peke yako. Hakuna wa kuniuliza kwa nini pazia nafutia sahani. 9. Leo mwizi kapigwa mpaka kasema, "mawe yanauma, nipigeni makofi.” 10. Hasira mnatoa wapi wakuu, fikiria mtu anaua kipepeo. 11. Bongo movie imen...
Kama unaelekea kufanya mtihani wa English au Geography, maswali haya usikubali kuyakosa, na kamwe usiingie katika mtihani wako, bila kuyasoma. Nafahamu unajiuliza kwamba, Geography na English iweje maswali yafanane? Kama umechelewa kujua, mambo yamebadilika japo kwa kushtukiza, maswali sasa yanaangazia hesabu nyepesi, kompyuta, akili mnemba na taaluma ya ualimu! Lakini kabla sijajikita katika maswali, naomba nisimulie mkasa ili kukuondoa hofu ya kuwa ‘not selected’ badala yake uamini jambo moja tu, ‘selected’! Niweke wazi kuwa, nina mahusiano na mwanamke anayefanya kazi Sekretariati ya Ajira . Hata hivyo, kitengo chake wala hakihusiki na mitihani ya usaili walimu. Ninafichua kuwa, mahusiano yangu na yeye yamelegea, tukigombana akinitaka niache hiki ninachokifanya asije akafikiriwa vibaya nikamharibia ugali wake! Siwezi kuacha, ninafanya jambo hili kwa sababu mimi ni mwalimu, sipendi kuona walimu wanateseka kusoma mambo ambayo hayatoki. Kazi yangu ni kuwaambia linatoka jambo hili,...