Swali: Onesha kwa mifano ya kutosha onesha namna uradidi unavyojitokeza katika lugha ya Kiswahili. Ili kutimiza mahitaji ya kila siku ya wanadamu, wanahitaji kuwasiliana, hata hivyo ipo changamoto ya msamiati. Changamoto hiyo ni kukosekana kwa msamiati unaohitajika ili kutaja kila dhana. Kutokana na upungufu wa msamiati unaohitajika kutaja kila dhana, watumiaji wa lugha hutumia mbinu mbalimbali za kuboresha msamiati uliopo ili ubebe dhana za ziada. Miongoni mwa mbinu zitumiwazo ni uradidi. Uradidi ni dhana inayojitokeza katika lugha nyingi kwa lengo la kuboresha msamiati uliopo ubebe dhana za ziada. Katika lugha ya Kiswahili, tukiacha dhima nyingi nyingine kama zile zilizobainishwa na Ashton (1944:316-318), uradidi unaweza kutumika katika mosi: kuimarisha au kudhoofisha maana, pili, kuongeza na kupunguza msisitizo wa dhana inayozungumziwa. Kwa hiyo, wakati mwingine mtumiaji wa lugha ya Kiswahili hulazimika kutumia mbinu ya uradidi ili kuwasilisha dhana ambayo ama haina msamiati un...
Tumekukusanyia mkusanyiko wa vichekesho vinavyochekesha sana. Vichekesho hivi, vitakufanya ufurahi muda wote, ni vizuri zaidi, uki’share’ na wenzako. 1. Huu mwezi mwenye nyumba aje atoe nyumba yake kwenye vitu vyangu, sina kodi. 2. Nimetoa vyombo nje nifanye usafi, kurudi naambiwa gari la taka limebeba. 3. Kwa jinsi maisha yalivyo magumu siku hizi unajikuta wewe ndiyo unamuamsha jogoo. 4. Chakula chenyewe unakipata kwa mateso halafu bado unakiwekea pilipili, una tatizo gani mkuu? 5. Mtu anakuja kuniomba elfu 20 kweli! Unaniombaje nusu ya utajiri wangu? 6. Daktari: Bia inatanua moyo. Walevi: imeshindwa kutanua chupa itatanua moyo? 7. Nimeota nakula tambi, kuamka sizioni "earphone" zangu. 8. Taja faida kwa nini unaishi peke yako. Hakuna wa kuniuliza kwa nini pazia nafutia sahani. 9. Leo mwizi kapigwa mpaka kasema, "mawe yanauma, nipigeni makofi.” 10. Hasira mnatoa wapi wakuu, fikiria mtu anaua kipepeo. 11. Bongo movie imen...
1. Kukosa hela ni vibaya sana, unaweza kukutana na ng’ombe ukahisi wanakusema. 2. Kama huna gari , huna nyumba, huna simu na huna hela, tofauti yako na kenge ni mkia. 3. Siyo kila anayeamka saa sita mchana ni tajiri, wengine wanapunguza saa za kuteseka. 4. Mtu mmoja aliota anaendesha gari, ikakwama kwenye matope, akaanza kuisukuma. Alipoamka, akajikuta yupo na kitanda jikoni. 5. Maisha ni ya ajabu sana, unakuta mtu hajaoa lakini chumba anachoishi kuna panya wana familia zao na yeye ndiyo anawalisha. 6. Ukiwa ugenini usinyamaze sana. Wenyeji wanaweza wakadhani unafikiria kuwaua. 7. Kila mtu anauogopa usiku. Kichaa mmoja alisikika akisema, “Usiku umeingia waniroge tena.” 8. Pombe mbaya, nimekutana na mlevi anatafuta wanawake wembamba atengeneze fagio. 9. Niliwahi kupanda basi, dereva analalamika njia nzima, “Nimefanya kazi miaka mingi, mafanikio hakuna. Sasa leo mwisho.” Abiria wakaanza kuomba kushuka mmojammoja. 10. Mchana hupati hela, usiku hupati usingizi. Kwa kifupi h...