Kitaalamu Zaidi, Tunaweza Kukuandikia Barua ya Maombi ya Kazi na CV Uitwe Katika Usaili na Upate Kazi. Barua Tsh. 5,000/= na CV Tsh. 9,000/=. Gusa Hapa Kuwasiliana Nasi. CV au wasifu ni kitu cha lazima kwa yeyote anayeomba kazi. Watu wengi wanaokosa kazi, tatizo huwa siyo wao, bali tatizo huwa ni CV zao. Kumekuwa na makosa mengi katika uandishi wa CV jambo ambalo limesababisha watafuta kazi wengi kushindwa kuitwa kwenye usaili. Makala hii itakueleza namna sahihi ya kuandika CV, utaitwa katika ‘interview’ nyingi endapo utaandika CV sahihi. Tena nakukumbusha, kila taaluma ina aina yake ya CV, CV ya rubani haifanani na CV ya injinia. Vivyo hivyo, CV ya mpishi haifananani na CV ya Mwalimu. Pia nakukumbusha usome jinsi ya kuandika barua ya maombi ya kazi , kwani CV huenda pamoja na barua ya maombi ya kazi. Hatua ya kwanza nitaonesha mfano wa CV kwa lugha ya Kiswahili na hatua ya pili nitaonesha mfano wa CV kwa lugha ya Kiingereza halafu utachagua mwenyewe utumie lugha gani katika kua
Kitaalamu Zaidi, Tunaweza Kukuandikia Barua ya Maombi ya Kazi na CV Uitwe Katika Usaili na Upate Kazi. Barua Tsh. 5,000/= na CV Tsh. 9,000/=. Gusa Hapa Kuwasiliana Nasi. Umewekeza katika elimu yako, una kila sifa ya kupata kazi fulani lakini hupati kazi hiyo, inawezekana kabisa sababu mojawapo inayokufanya usipate kazi unayoitaka ni kutokujua kuandika barua ya maombi ya kazi au unapoandika, unaandika katika namna mbaya inayofanya waajiri wakupuuze. Kwa muda mrefu nimekuwa nikiulizwa na wanafunzi na wasomaji wa mtandao wangu kuhusu jinsi ya kuandika barua ya maombi ya kazi kwa kiswahili, na wengine huuliza kuhusu jinsi ya kuandika barua ya maombi ya kazi kwa kiingereza. Waombaji wengi huuliza kuhusu maombi ya kazi ya udereva, hotelini, kazi za polisi, ualimu, afya utendaji wa kijiji na kazi chungu nzima ambazo haziwezi kutosha hapa zikiandikwa. Kazi zote siku hizi zinahitaji kuandika barua, hata kama unataka kujitolea, lazima utaandika barua! Isivyo bahati ni kuwa, hata mtandaoni
Risala ni hotuba fupi iliyokatika maandishi na ambayo husomwa mbele ya mgeni rasmi ikielezea kuhusu mafanikio, changamoto na maombi ya kundi fulani. Muundo wa Risala - Utangulizi. Katika kipengele hiki, cheo cha kiongozi (mgeni rasmi) hutajwa. Pia kundi linalowakilishwa. - Kiini. Mafanikio ya kundi, changamoto za kundi, mapendekezo na ushauri. - Hitimisho. Kipengele hiki hukaa shukrani. Sasa hebu tazama mfano huu wa risala: Swali; Jifanye wewe ni mwanafunzi wa kidato cha nne na umechaguliwa kuandaa risala itakayosomwa mbele ya mgeni rasmi siku ya mahafali yako ya kumaliza kidato cha nne. Andika risala utakayoisoma siku hiyo. RISALA YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE KWA MGENI RASMI Ndugu mgeni rasmi, waalimu, wazazi, wanafunzi wenzetu, wageni waalikwa mabibi na mabwana. Ndugu mgeni rasmi, tunayofuraha kukualika leo hii katika sherehe yetu ya mahafari haya ya kidato cha nne ili usherehekee pamoja nasi na zaidi uweze kusikia mafanikio y