1. Kukosa hela ni vibaya sana, unaweza kukutana na ng’ombe ukahisi wanakusema. 2. Kama huna gari , huna nyumba, huna simu na huna hela, tofauti yako na kenge ni mkia. 3. Siyo kila anayeamka saa sita mchana ni tajiri, wengine wanapunguza saa za kuteseka. 4. Mtu mmoja aliota anaendesha gari, ikakwama kwenye matope, akaanza kuisukuma. Alipoamka, akajikuta yupo na kitanda jikoni. 5. Maisha ni ya ajabu sana, unakuta mtu hajaoa lakini chumba anachoishi kuna panya wana familia zao na yeye ndiyo anawalisha. 6. Ukiwa ugenini usinyamaze sana. Wenyeji wanaweza wakadhani unafikiria kuwaua. 7. Kila mtu anauogopa usiku. Kichaa mmoja alisikika akisema, “Usiku umeingia waniroge tena.” 8. Pombe mbaya, nimekutana na mlevi anatafuta wanawake wembamba atengeneze fagio. 9. Niliwahi kupanda basi, dereva analalamika njia nzima, “Nimefanya kazi miaka mingi, mafanikio hakuna. Sasa leo mwisho.” Abiria wakaanza kuomba kushuka mmojammoja. 10. Mchana hupati hela, usiku hupati usingizi. Kwa kifupi h...
Katika maandalizi ya mitihani ya usaili walimu, yapo maswali ambayo ni lazima yatoke. Mojawapo ni maswali kuhusu saikolojia ya elimu, ‘ Education Pyschology ’ (EP). maswali mengi yanayotoka yanajikita katika wanasaikolojia 10, hivyo, ukiwafahamu wao na mambo waliyofanya, unakuwa na nafasi nzuri zaidi ya kufanya vizuri katika mitihani yako kiasi cha kufanikiwa kufika usaili wa pili, ‘oral interview’. 1. Jean Piaget Theory of cognitive development Piaget identified four major stages of cognitive development: Sensorimotor stage (0–2 years) Infants learn through senses and actions Preoperational stage (2–7 years) They begin to imagine and use symbolic thinking Dramatic play Teachers should make space for play Concrete operational stage (7–11 years) Children understand logical operations They understand transformations (e.g., adding or subtracting) Thinking is based on concrete objects and events Formal operational stage (11 years and above) Children are able to reason abstractly They can ...
Tumekukusanyia mkusanyiko wa vichekesho vinavyochekesha sana. Vichekesho hivi, vitakufanya ufurahi muda wote, ni vizuri zaidi, uki’share’ na wenzako. 1. Huu mwezi mwenye nyumba aje atoe nyumba yake kwenye vitu vyangu, sina kodi. 2. Nimetoa vyombo nje nifanye usafi, kurudi naambiwa gari la taka limebeba. 3. Kwa jinsi maisha yalivyo magumu siku hizi unajikuta wewe ndiyo unamuamsha jogoo. 4. Chakula chenyewe unakipata kwa mateso halafu bado unakiwekea pilipili, una tatizo gani mkuu? 5. Mtu anakuja kuniomba elfu 20 kweli! Unaniombaje nusu ya utajiri wangu? 6. Daktari: Bia inatanua moyo. Walevi: imeshindwa kutanua chupa itatanua moyo? 7. Nimeota nakula tambi, kuamka sizioni "earphone" zangu. 8. Taja faida kwa nini unaishi peke yako. Hakuna wa kuniuliza kwa nini pazia nafutia sahani. 9. Leo mwizi kapigwa mpaka kasema, "mawe yanauma, nipigeni makofi.” 10. Hasira mnatoa wapi wakuu, fikiria mtu anaua kipepeo. 11. Bongo movie imen...