Tumekukusanyia mkusanyiko wa vichekesho vinavyochekesha sana. Vichekesho hivi, vitakufanya ufurahi muda wote, ni vizuri zaidi, uki’share’ na wenzako. 1. Huu mwezi mwenye nyumba aje atoe nyumba yake kwenye vitu vyangu, sina kodi. 2. Nimetoa vyombo nje nifanye usafi, kurudi naambiwa gari la taka limebeba. 3. Kwa jinsi maisha yalivyo magumu siku hizi unajikuta wewe ndiyo unamuamsha jogoo. 4. Chakula chenyewe unakipata kwa mateso halafu bado unakiwekea pilipili, una tatizo gani mkuu? 5. Mtu anakuja kuniomba elfu 20 kweli! Unaniombaje nusu ya utajiri wangu? 6. Daktari: Bia inatanua moyo. Walevi: imeshindwa kutanua chupa itatanua moyo? 7. Nimeota nakula tambi, kuamka sizioni "earphone" zangu. 8. Taja faida kwa nini unaishi peke yako. Hakuna wa kuniuliza kwa nini pazia nafutia sahani. 9. Leo mwizi kapigwa mpaka kasema, "mawe yanauma, nipigeni makofi.” 10. Hasira mnatoa wapi wakuu, fikiria mtu anaua kipepeo. 11. Bongo movie imen...
1. Kukosa hela ni vibaya sana, unaweza kukutana na ng’ombe ukahisi wanakusema. 2. Kama huna gari , huna nyumba, huna simu na huna hela, tofauti yako na kenge ni mkia. 3. Siyo kila anayeamka saa sita mchana ni tajiri, wengine wanapunguza saa za kuteseka. 4. Mtu mmoja aliota anaendesha gari, ikakwama kwenye matope, akaanza kuisukuma. Alipoamka, akajikuta yupo na kitanda jikoni. 5. Maisha ni ya ajabu sana, unakuta mtu hajaoa lakini chumba anachoishi kuna panya wana familia zao na yeye ndiyo anawalisha. 6. Ukiwa ugenini usinyamaze sana. Wenyeji wanaweza wakadhani unafikiria kuwaua. 7. Kila mtu anauogopa usiku. Kichaa mmoja alisikika akisema, “Usiku umeingia waniroge tena.” 8. Pombe mbaya, nimekutana na mlevi anatafuta wanawake wembamba atengeneze fagio. 9. Niliwahi kupanda basi, dereva analalamika njia nzima, “Nimefanya kazi miaka mingi, mafanikio hakuna. Sasa leo mwisho.” Abiria wakaanza kuomba kushuka mmojammoja. 10. Mchana hupati hela, usiku hupati usingizi. Kwa kifupi h...
JINA LA KITABU: NGOSWE PENZI KITOVU CHA UZEMBE MWANDISHI: EDWIN SEMZABA Mhakiki: Mwalimu Makoba Utangulizi Afisa aliyetumwa kuhesabu watu-Ngoswe, anashindwa kuifanya kazi yake na kuanzisha ajenda nyingine ya mapenzi. Anapanga kutoroka na binti Mazoea aliyekwisha kuposwa tayari, Mazoea naye kusikia atakwenda kuishi mjini anakubaliana na mpango huo. Wanapotoroka, Ngoswe anasahau mkoba wenye takwimu za watu waliokwisha kuhesabiwa, Mzee Ngengemkeni Mitomingi ambaye ndiye baba yake na Mazoea, anazichoma moto takwimu hizo na kumsababishia hasara kubwa Ngoswe. J ina la Kitabu Jina la kitabu “Ngoswe penzi kitovu cha uzembe” ni jina ambalo limesawiri vyema yaliyomo ndani ya kitabu hicho, kwani Ngoswe ndio jina la mhusika mkuu anayebeba dhamira kuu ya tamthiliya. Pia penzi limeonekana kuwa ni kitovu cha uzembe kwani ndio yaliyopelekea kuteketezwa kwa karatasi za takwimu za sensa. Hivyo jina la kitabu si tu kwamba limesawiri yaliyomo katika kitabu bali pia katika jamii. Maudhui...