Kitaalamu Zaidi, Tunaweza Kukuandikia Barua ya Maombi ya Kazi na CV Uitwe Katika Usaili na Upate Kazi. Barua Tsh. 5,000/= na CV Tsh. 9,000/=. Gusa Hapa Kuwasiliana Nasi. CV au wasifu ni kitu cha lazima kwa yeyote anayeomba kazi. Watu wengi wanaokosa kazi, tatizo huwa siyo wao, bali tatizo huwa ni CV zao. Kumekuwa na makosa mengi katika uandishi wa CV jambo ambalo limesababisha watafuta kazi wengi kushindwa kuitwa kwenye usaili. Makala hii itakueleza namna sahihi ya kuandika CV, utaitwa katika ‘interview’ nyingi endapo utaandika CV sahihi. Tena nakukumbusha, kila taaluma ina aina yake ya CV, CV ya rubani haifanani na CV ya injinia. Vivyo hivyo, CV ya mpishi haifananani na CV ya Mwalimu. Pia nakukumbusha usome jinsi ya kuandika barua ya maombi ya kazi , kwani CV huenda pamoja na barua ya maombi ya kazi. CV Bora ni Ipi? Ukurasa Mmoja au Kurasa mbili hadi tatu? CV bora ni ile yenye kurasa mbili hadi tatu. Watu wengi wanapojifunza namna ya kuandika CV, wamekuwa wakiona CV zenye ukurasa...
TAMTHILIYA; KILIO CHETU MWANDISHI; MEDICAL AID FOUNDATION MCHAPISHAJI; TANZANIA PUBLISHING HOUSE MWAKA; 1995 JINA LA MHAKIKI; Mwalimu Daud Makoba Kilio chetu ni tamthiliya inayovunja ukimya uliotawala miongoni mwa jamii katika kutatua matatizo makubwa ambayo chimbuko lake ni mahusiano ya kijinsia. Katika tamthiliya hii vijana wanatoa sauti ya jitimai iliyojaa sononeko na shutuma dhidi ya wazazi, walezi na viongozi ambao wanafumbia macho suala hili nyeti. Ndiyo maana tamthiliya hii inasisitiza sana haja ya kuwapa vijana elimu juu ya mahusiano ya kijinsia badala ya hofu na vitisho ambavyo vimedhihirika kupitia hali halisi ya kuwa vimeshindwa. FANI MUUNDO Tamthiliya hii imetumia muundo wa moja kwa moja. Inaanza kwa kutuonesha wazazi wakibishana juu ya kutoa elimu ya jinsia na mahusiano. Mwisho Joti mtoto ambaye hakupatiwa elimu hiyo anampa mimba mtoto mwenzake Suzi. Baadae Joti anakufa kwa UKIMWI. Pia tamthiliya hii imegawanywa katika sehemu sita. sehemu y...
1. Kukosa hela ni vibaya sana, unaweza kukutana na ng’ombe ukahisi wanakusema. 2. Kama huna gari , huna nyumba, huna simu na huna hela, tofauti yako na kenge ni mkia. 3. Siyo kila anayeamka saa sita mchana ni tajiri, wengine wanapunguza saa za kuteseka. 4. Mtu mmoja aliota anaendesha gari, ikakwama kwenye matope, akaanza kuisukuma. Alipoamka, akajikuta yupo na kitanda jikoni. 5. Maisha ni ya ajabu sana, unakuta mtu hajaoa lakini chumba anachoishi kuna panya wana familia zao na yeye ndiyo anawalisha. 6. Ukiwa ugenini usinyamaze sana. Wenyeji wanaweza wakadhani unafikiria kuwaua. 7. Kila mtu anauogopa usiku. Kichaa mmoja alisikika akisema, “Usiku umeingia waniroge tena.” 8. Pombe mbaya, nimekutana na mlevi anatafuta wanawake wembamba atengeneze fagio. 9. Niliwahi kupanda basi, dereva analalamika njia nzima, “Nimefanya kazi miaka mingi, mafanikio hakuna. Sasa leo mwisho.” Abiria wakaanza kuomba kushuka mmojammoja. 10. Mchana hupati hela, usiku hupati usingizi. Kwa kifu...