Kitaalamu Zaidi, Tunaweza Kukuandikia Barua ya Maombi ya Kazi na CV Uitwe Katika Usaili na Upate Kazi. Barua Tsh. 5,000/= na CV Tsh. 9,000/=. Gusa Hapa Kuwasiliana Nasi. CV au wasifu ni kitu cha lazima kwa yeyote anayeomba kazi. Watu wengi wanaokosa kazi, tatizo huwa siyo wao, bali tatizo huwa ni CV zao. Kumekuwa na makosa mengi katika uandishi wa CV jambo ambalo limesababisha watafuta kazi wengi kushindwa kuitwa kwenye usaili. Makala hii itakueleza namna sahihi ya kuandika CV, utaitwa katika ‘interview’ nyingi endapo utaandika CV sahihi. Tena nakukumbusha, kila taaluma ina aina yake ya CV, CV ya rubani haifanani na CV ya injinia. Vivyo hivyo, CV ya mpishi haifananani na CV ya Mwalimu. Pia nakukumbusha usome jinsi ya kuandika barua ya maombi ya kazi , kwani CV huenda pamoja na barua ya maombi ya kazi. Hatua ya kwanza nitaonesha mfano wa CV kwa lugha ya Kiswahili na hatua ya pili nitaonesha mfano wa CV kwa lugha ya Kiingereza halafu utachagua mwenyewe utumie lugha gani katika kua
Kitaalamu Zaidi, Tunaweza Kukuandikia Barua ya Maombi ya Kazi na CV Uitwe Katika Usaili na Upate Kazi. Barua Tsh. 5,000/= na CV Tsh. 9,000/=. Gusa Hapa Kuwasiliana Nasi. Umewekeza katika elimu yako, una kila sifa ya kupata kazi fulani lakini hupati kazi hiyo, inawezekana kabisa sababu mojawapo inayokufanya usipate kazi unayoitaka ni kutokujua kuandika barua ya maombi ya kazi au unapoandika, unaandika katika namna mbaya inayofanya waajiri wakupuuze. Kwa muda mrefu nimekuwa nikiulizwa na wanafunzi na wasomaji wa mtandao wangu kuhusu jinsi ya kuandika barua ya maombi ya kazi kwa kiswahili, na wengine huuliza kuhusu jinsi ya kuandika barua ya maombi ya kazi kwa kiingereza. Waombaji wengi huuliza kuhusu maombi ya kazi ya udereva, hotelini, kazi za polisi, ualimu, afya utendaji wa kijiji na kazi chungu nzima ambazo haziwezi kutosha hapa zikiandikwa. Kazi zote siku hizi zinahitaji kuandika barua, hata kama unataka kujitolea, lazima utaandika barua! Isivyo bahati ni kuwa, hata mtandaoni
Fafanua kwa kina huku ukitumia mchoro sifa bainifu za irabu ya Kiswahili sanifu. Irabu ni aina ya vitamkwa ambavyo hutolewa pasi, bila kuwepo kizuizi chochote katika mkondohewa au hewa itokayo mapafuni ikipitia katika chemba ya kinywa au ya pua iwapo irabu hiyo itasilimishwa. Irabu ziko za aina nyingi lakini tutatumia zaidi irabu za lugha ya Kiswahili. Katika kuainisha sifa za irabu ni lazima kuzingatia lugha ambamo irabu hizo zinatumika, kwa sababu kila lugha huchagua idadi ya irabu kadhaa kutoka katika bohari la sauti kwa kuzingatia irabu msingi ambacho ndicho msingi wa irabu za lugha mbalimbali. Kuhusu lugha za Kibantu kuna irabu kuu tano ambazo hutumika karibu katika lugha nyingi za Kibantu na lugha ya Kiswahili ikiwemo kama asemavyo Massamba na wenzake (2004). Irabu hizo huwakilishwa kiimaandishi kama ifuatavyo. Maandishi ya kawaida Maandishi ya kifonetiki a) i [i] mfano katika neno l i a, p i ka b) e [ε] mfano katika neno ch