Tumekukusanyia mkusanyiko wa vichekesho vinavyochekesha sana. Vichekesho hivi, vitakufanya ufurahi muda wote, ni vizuri zaidi, uki’share’ na wenzako. 1. Huu mwezi mwenye nyumba aje atoe nyumba yake kwenye vitu vyangu, sina kodi. 2. Nimetoa vyombo nje nifanye usafi, kurudi naambiwa gari la taka limebeba. 3. Kwa jinsi maisha yalivyo magumu siku hizi unajikuta wewe ndiyo unamuamsha jogoo. 4. Chakula chenyewe unakipata kwa mateso halafu bado unakiwekea pilipili, una tatizo gani mkuu? 5. Mtu anakuja kuniomba elfu 20 kweli! Unaniombaje nusu ya utajiri wangu? 6. Daktari: Bia inatanua moyo. Walevi: imeshindwa kutanua chupa itatanua moyo? 7. Nimeota nakula tambi, kuamka sizioni "earphone" zangu. 8. Taja faida kwa nini unaishi peke yako. Hakuna wa kuniuliza kwa nini pazia nafutia sahani. 9. Leo mwizi kapigwa mpaka kasema, "mawe yanauma, nipigeni makofi.” 10. Hasira mnatoa wapi wakuu, fikiria mtu anaua kipepeo. 11. Bongo movie imen...
TAMTHILIYA; KILIO CHETU MWANDISHI; MEDICAL AID FOUNDATION MCHAPISHAJI; TANZANIA PUBLISHING HOUSE MWAKA; 1995 JINA LA MHAKIKI; Mwalimu Makoba Kilio chetu ni tamthiliya inayovunja ukimya uliotawala miongoni mwa jamii katika kutatua matatizo makubwa ambayo chimbuko lake ni mahusiano ya kijinsia. Katika tamthiliya hii vijana wanatoa sauti ya jitimai iliyojaa sononeko na shutuma dhidi ya wazazi, walezi na viongozi ambao wanafumbia macho suala hili nyeti. Ndiyo maana tamthiliya hii inasisitiza sana haja ya kuwapa vijana elimu juu ya mahusiano ya kijinsia badala ya hofu na vitisho ambavyo vimedhihirika kupitia hali halisi ya kuwa vimeshindwa. Fani Muundo Tamthiliya hii imetumia muundo wa moja kwa moja. Inaanza kwa kutuonesha wazazi wakibishana juu ya kutoa elimu ya jinsia na mahusiano. Mwisho Joti mtoto ambaye hakupatiwa elimu hiyo anampa mimba mtoto mwenzake Suzi. Baadae Joti anakufa kwa UKIMWI. Pia tamthiliya hii imegawanywa katika sehemu sita. sehemu ya kwanza....
1. Kukosa hela ni vibaya sana, unaweza kukutana na ng’ombe ukahisi wanakusema. 2. Kama huna gari , huna nyumba, huna simu na huna hela, tofauti yako na kenge ni mkia. 3. Siyo kila anayeamka saa sita mchana ni tajiri, wengine wanapunguza saa za kuteseka. 4. Mtu mmoja aliota anaendesha gari, ikakwama kwenye matope, akaanza kuisukuma. Alipoamka, akajikuta yupo na kitanda jikoni. 5. Maisha ni ya ajabu sana, unakuta mtu hajaoa lakini chumba anachoishi kuna panya wana familia zao na yeye ndiyo anawalisha. 6. Ukiwa ugenini usinyamaze sana. Wenyeji wanaweza wakadhani unafikiria kuwaua. 7. Kila mtu anauogopa usiku. Kichaa mmoja alisikika akisema, “Usiku umeingia waniroge tena.” 8. Pombe mbaya, nimekutana na mlevi anatafuta wanawake wembamba atengeneze fagio. 9. Niliwahi kupanda basi, dereva analalamika njia nzima, “Nimefanya kazi miaka mingi, mafanikio hakuna. Sasa leo mwisho.” Abiria wakaanza kuomba kushuka mmojammoja. 10. Mchana hupati hela, usiku hupati usingizi. Kwa kifupi h...