Kilichotokea Katika Kaburi la Mume wa Zari Kinasikitisha
Hamu ya utajiri na imani potofu ni miongoni mwa mambo
ambayo yanazidi kuichafua dunia kila uchwao. Huko Uganda, kaburi la aliyekuwa
mume wa mwanadada Zari, bwana Ivan Ssemwanga limefukuliwa na wahalifu
wasiojulikana.
Watu wengi wanaamini mwili wa Ivan ulizikwa ukiwa na
pesa nyingi kitu ambacho huenda kikawa kimechochea ufukuaji huo. Jambo jingine
linalotajwa na mashuhuda wa tukio hilo ni imani za kishirikina ambapo huenda
waganga waliwatuma watu hao fuvu la Ivan.
Mara baada ya Ivan kuzikwa, waliwekwa walinzi ili
kuzuia tukio kama hili. Hata hivyo, inasemekana walinzi hao waliacha kulinda
baada ya kutofautiana katika gharama za malipo.
Kaburi la Ivan likiwa limefukuliwa. |