Usipofanya Mambo Haya Utajifungua kwa Upasuaji

sababu za kujifungua kwa upasuaji
Idadi ya wanawake wanaojifungua kwa njia ya upasuaji imekuwa ikongezeka siku hadi siku. Njia hii huchukuliwa kama maamuzi ya mwisho ya kuhakikisha mama anajifungua salama. Ipo hatari kubwa kujifungua kwa njia ya upasuaji, wote, mama na mtoto hukumbwa na hatari hii.
Tafiti zilizofanyika hivi karibuni zimeeleza sababu mojawapo inayopelekea wanawake kujifungua kwa upasuaji ni uzito kupita kiasi. Uzito kupita kiasi mara nyingi ni matokeo ya mitindo ya maisha ya mwanamke mwenyewe. Mitindo hii ni pamoja na kuepuka kufanya mazoezi na kushindwa kabisa kujizuia ulaji wa vyakula vyenye wingi wa mafuta na sukari.

Nini Kifanyike Kumwepusha Mwanamke Kujifungua kwa Njia ya Upasuaji?

Jambo kubwa la msingi ni kuhakikisha mwanamke hana uzito kupita kiasi. Njia mojawapo inayotumika kupima kama una uzito kupita kiasi ni kipimo cha BMI. Endapo utakutwa na uzito kupita kiasi, basi ni vyema ukaanza mazoezi mapema ili kukwepusha na madhara yatakayokupata hapo baadaye.
Njia sahihi ya kupunguza uzito ni mazoezi ya viungo kama kukimbia, kuruka kamba na mazoezi mengine mepesi. Kufanya mazoezi kwa angalau dakika 30 kwa siku kunatosha kabisa kukufanya mwenye afya njema.
Baada ya kuanza ratiba ya ufanyaji wa mazoezi, jambo linalofuata ni kuepuka ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi na sukari. Hapo utajihakikishia kuwa na mwili bora na imara.
Pia, ili kumwepusha mama mjamzito kujifungua kwa njia ya upasuaji ni kuhakikisha anahudhuria ‘kliniki’ ili aweze kupewa msaada wa kiafya na endapo atakutwa na dalili zozote za hatari aweze kusaidiwa.
Hata hivyo kumeibuka imani potofu kwa baadhi ya wanawake kulazimisha wajifungue kwa njia ya upasuaji hata pale wanapokuwa hawana tatizo lolote. Sababu kubwa inayopelekea hali hii, ni kudhani kuwa endapo watajifungua kwa njia ya kawaida, viungo vyao vya uzazi vitaongezeka ukubwa na kuwafanya wapoteze mvuto katika tendo la ndoa. Imani hii ni finyu na haipaswi kuaminika kwani haina ukweli wowote zaidi ya kumuumiza mwanamke mwenyewe.

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne