Historia na Maendeleo ya Fasihi ya Kiswahili
Fasihi ya Kiswahili ni ile
iliyoandikwa kwa lugha ya Kiswahili tu. Iwapo inazungumzia utamaduni wa
Kiswahili au utamaduni mwingine. (Masebo & Nyangwine; 2007).
Historia ya fasihi ya Kiswahili
inajadiliwa kwa kugawanywa katika vipindi vinne:
-
Kabla
ya wageni
-
Wakati
wa waarabu
-
Wakati
wa ukoloni
-
Baada
ya uhuru mpaka hivi sasa
Historia ya Fasihi ya Kiswahili Kabla ya Wageni
Katika kipindi hiki, fasihi
haikuandikwa. Kulikuwa na fasihi simulizi pekee. Fasihi hii ilijumuisha ngano,
methali, vitendawili, nyimbo, mashairi, majigambo n.k.
Fasihi hii ilipambwa na wahusika
wanyama na mizimu, na ilisimuliwa jioni baada ya watu kumaliza kufanya kazi.
Katika kipindi hiki, fasihi
ilitumiwa kama chombo cha kuelimisha jamii na kukemea maovu yote.
Wakati wa Waarabu
Wakati wa waarabu fasihi ya
Kiswahili ilianza kuandikwa kwa hati za kiarabu. Kazi nyingi za Kiarabu
zikafasiliwa na kuwekwa katika Kiswahili. Kwa mfano: hadithi za Alfu Lela
Ulela, Hekaya za Abunuwasi na mashairi yaliyokuwa na urari wa vina na mizani.
Fasihi ya Kiswahili kwa mara ya
kwanza ikapata nafasi ya kuhifadhiwa katika maandishi. Huo ndiyo ukawa mwanzo
wa kuibuka kwa fasihi andishi.
Wakati wa Ukoloni
Katika wakati huu wazungu
walikuja na hati zao za Kilatini. Fasihi ya Kiswahili ikaanza kuandikwa kwa
hati ya Kilatini mpaka hii leo.
Hali hii ilikwenda sambamba na
kuibuka kwa kazi nyingi za fasiri. Safari za Gulliver, Mashimo ya Mfalme
Suleiman na Kisiwa Chenye Hazina ni mfano wa kazi hizo.
Kazi hizo za tafsiri zilijaa propaganda
nyingi ili kuwafanya waafrika wajione wanyonge mbele ya wazungu.
Hazikuzungumzia mambo yoyote yaliyowafaidisha waafrika.
Waandishi wa Kiafrika kama,
Shaaban Robert na Mussa Said Abdallah waliibuliwa na mashindano ya uandishi
yaliyoendeshwa na wakoloni.
Baada ya Uhuru Mpaka Hivi Sasa
Baada ya uhuru vitabu vya awali
viliandikwa kwa lengo la kupongeza kupata uhuru huo.
Mara baada ya uhuru kuwa
umekwisha patikana na hakuna jipya lolote lililoletwa na serikali za Kiafrika,
fasihi ya kichokozi iliyosema na kuuhoji ukweli ikaibuka. Vitabu kama, Rosa
Mistika, Nagona, Mzingile, Fungate ya Uhuru, Wasakatonge, Lina Ubani, n.k ni
mfano wa vitabu ambavyo vinaonyesha
kutokuridhishwa na hali ya mambo hata baada ya uhuru kuwa umepatikana.