WALICHOAMUA ‘WHATSAPP’ KUHUSU KUFUTA MESEJI ULIYOTUMA KWA BAHATI MBAYA

‘WHATSAPP’ KUHUSU KUFUTA MESEJI ULIYOTUMA KWA BAHATI MBAYA

Hakuna jambo linalokosesha amani kama kushindwa kuifuta meseji uliyoituma ‘WhatsApp’ ili watu wengine wasiweze kuiona. Kushindwa kufuta meseji baada ya kutuma kumewahi kusababisha maafa na mifadhaiko mikubwa sana. Mara nyingi hutokea ukadhani ujumbe  ambao unaweza kuwa wa masihara au mapenzi unatuma kwa mtu fulani lakini kwa bahati mbaya ujumbe huo ukaingia katika kundi la watu unaoheshimiana nao sana. Aibu hii imewatesa wengi na sasa ‘WhatsApp’ wameonyesha kuguswa na jambo hili na wameamua kulitafutia ufumbuzi.
Mvujishaji wa taarifa za ‘WhatsApp,’ WABentaInfo, ametaarifu kuwa, mtandao  huo kwa sasa unafanyia kazi mfumo mpya utakao wezesha kufuta ujumbe ulioutuma kwa bahati mbaya. Tayari majaribio yameanza kufanyika katika mifumo ya Android na iOS. Imezidi kuarifiwa mfumo huo unafanya kazi kwa ufanisi mkubwa.
Mitandao mingine ya Telegram, WeChat na Viber, imetumia mfumo huu kwa muda mrefu huku watumiaji wa 'WhatsApp' nao wakiomba wawekewe ‘delete for everyone.’

Huenda mfumo huu mpya ukaanza kufanya kazi mwaka huu au mwakani. Endapo utatumika, bila shaka utapokelewa vyema!

POVU LA MWALIMU MAKOBA KWA WASANII WANAO VAA HOVYO...

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne