MBOWE AELEZA HALI YA TUNDU LISSU KWA SASA
Mbunge wa Hai, Mheshimiwa
Freeman Mbowe ameeleza hali ya kiafya ya
Mbunge Tundu Lissu ambaye alipigwa risasi na watu wasiojulikana siku chache
zilizopita.
Akiandika katika ukurasa wake wa
‘instagram’ amesema, madaktari wanatoa matumaini na ile hali ya kuhofia
kupoteza maisha kwa Lissu imekwisha.
Vilevile, anazungumza na anaweza
kutoa salamu. Kuhusu taarifa za maambukizi ya kifua zilizosambaa, Mbowe
amekanusha na kusema taarifa hizo si za kweli.
Mwisho amewasisitiza watu wote
wazidi kumuombea kila wakati aweze kupona kwa haraka na hatimaye kutoka
hospitali.
Taarifa hiyo imesisitiza watu
wasisikilize taarifa kutoka kwa watu wasiohusika, bali wasikilize taarifa
zinazotoka kwake yeye na timu yake iliyoko Nairobi kwani wao ndiyo wapo karibu
na mgonjwa.
Mbali na hayo, hii leo
kumefanyika tukio la kuwasomea ‘albadri’ watu wote waliohusika na tukio la
kumshambulia Tundu Lissu. Shughuli hiyo imefanyika katika mikoa kadhaa nchini.