Uhakiki wa Riwaya ya Vuta N’kuvute
MWANDISHI: SHAFI ADAM SHAFI WACHAPISHAJI: MKUKI NA NYOTA MWAKA: 1999 MHAKIKI: MWALIMU MAKOBA Utangulizi Vuta n’kuvute ni riwaya inayozungumzia mvutano uliopo baina ya wakoloni na watawaliwa vilevile inaonyesha msuguano na mvutano uliopo kati ya wazazi na watoto katika suala la mapenzi. Maudhui DHAMIRA UKOMBOZI Mwandishi anaonyesha aina mbalimbali za ukombozi unaohitajika katika jamii. Mfano: ukombozi wa kiutamaduni. Hapa anapinga mila zinazomkandamiza mwanamke. Kwa mfano, Yasmini kulazimishwa kuolewa na Raza, ni unyanyasaji usiokubalika. Pia, ukombozi wa kisiasa. Mwandishi anaonyesha jinsi ambavyo Zanzibar ilitawaliwa na Waingereza. Wahusika Denge na wenzake wanapambana vilivyo kuhakikisha uhuru wa Zanzibar unapatikana. Ukiachilia mbali aina hizo mbili za ukombozi, mwandishi pia amejadili ukombozi wa kiuchumi na fikra. Mapenzi Mwandishi anajadili mapenzi ya kweli na yale ya uongo. Katika mapenzi ya kweli, Mwajuma, Denge na kundi lake wanamapenzi ya kweli k...