ALICHOKIANDIKA MMILIKI WA MTANDAO WA FACEBOOK
Mark Zuckerberg ambaye ni
mmiliki wa mtandao wa facebook na baba wa watoto wawili aliowapata kwa mwenzi
wake Priscilla Chan, amezua gumzo mtandaoni baada ya kuianika barua ambayo
amemwandikia binti yake.
Katika barua hiyo, Mark
amemtaka binti yake awe anatoka nje kucheza ili kuyafurahia maisha ya utoto.
Pia, amemsihi binti yake
afanye mazoezi ya kukimbia kuzunguka sebule na akipenda atoke nje kucheza
atakavyo.
Barua iliendelea kusema
kuwa, utoto upo mara moja tu, hivyo ni busara kuufurahia na kuepuka kuwaza
kupita kiasi.
GUMZO LAIBUKA MITANDAONI
Wake kwa waume wametoa maoni
yao kuhusiana na barua hiyo ya Mark kwa binti yake. Wanaume wameonekana
kucharuka zaidi huku wengi wao wakipanga mikakati ya kumuwinda atakapotoka ili
waweze kuwa wakwe wa bilionea Mark Zuckeberg mmiliki na mwanzilishi wa mtandao
wa kijamii wa facebook.
Unalizungumziaje hili? Shusha comment yako…