‘SHARE’ MAKALA ZETU KWENYE MITANDAO YA KIJAMII TUKULIPE!


Usiishie kupata ‘like’ nyingi zisizokunufaisha kwa lolote, zigeuze ‘like’ zako kuwa pesa.
Unawezaje kulipwa kupitia ‘like’ zako?
Unaweza kulipwa pale unapo ‘share’ chochote kutoka blogu ya mwalimumakoba.blogspot.com. kwa kila ‘like’ 200 utalipwa shilingi 2,000 (elfu mbili). Hivyo kwa kila ‘like’ moja utakayopata, ikiwemo ‘like’ yako, utalipwa shilingi 10. Hata hivyo, pungufu ya ‘like’ 200 haitalipwa chochote.
Jinsi ya ku ‘share’ makala zetu
Hatua ya kwanza. Ingia katika blog ya mwalimumakoba.blogspot.com. Chagua makala yoyote utakayoipenda, inaweza kuwa riwaya, notsi za darasani, vichekesho au chochote utakachoona kinafaa.
Hatua ya pili. Ifungue habari hiyo kisha shuka mpaka chini utaona ‘button’ ya ku ‘share’, ‘share’ habari uliyoichagua katika mtandao wa ‘facebook’. Endapo utashindwa ku ‘share’ kwa njia hiyo, tumia njia hii. Chagua makala unayoitaka, kama unatumia simu, kandamiza kwa muda kichwa cha makala, yatakuja maneno, bofya kwenye ‘copy link address’ kisha nenda moja kwa moja kwenye ukurasa wako wa ‘facebook’ kisha ‘post’. Kama unatumia kompyuta, ‘right click’ kichwa cha makala uliyoichagua, yatatokea maneno, chagua, ‘copy link address’ kisha nenda moja kwa moja mpaka katika ukurasa wako wa facebook, ‘paste’ ‘link’ hiyo tayari kwa kui ‘post’.
NINI KINAFUATA BAADA YA HAPO?
Hesabu ‘like’ zinavyomiminika katika habari uliyo ‘share’. Zikifika ‘like’ 200, ‘screen shot’, kisha picha uliyoi ‘screenshot’ itume kwa njia ya WatsApp  kwenda namba 0754 89 53 21. Baada ya masaa mawili ya kuhakiki kama ulichokituma ni sahihi utatumiwa pesa yako katika namba iliyotumika kutuma ile ‘screenshot’.
NINI FAIDA YETU KWA KUFANYA YOTE HAYA?
Faida yetu ni kupata watu wengi wanaoisoma blogu yetu. Kwa kuwa katika blogu hii tunaandika makala zinazowasaidia watu wote wakiwemo wanafunzi, wapenzi wa riwaya, wasoma vichekesho, wapenda siasa, wapenzi wa lugha adhimu ya Kiswahili na watu wa namna zote zisizoweza kuelezeka, basi ni furaha yetu kuona kile tunachoandika kinawafikia watu hawa na si kuishia kuandika bila kupata wasomaji.
NAWEZA KUWA TAJIRI KWA KU ‘SHARE’ MAKALA ZENU?
Hapana. Huwezi kuwa tajiri kwa ku ‘share’ makala zetu. Hatukuahidi kuwa bilionea kupitia mfumo huu, ila tunakuahidi kukupatia pesa itakayotunisha pochi yako na kukutatulia matatizo madogomadogo ya kiuchumi.
NATAKIWA KUANZA LINI?
Ooooh… ulitakiwa kuanza jana! Hata hivyo bado hujachelewa, ANZA SASA!

Nasubiri ‘screenshot’ yako yenye idadi ya like 200.

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Uhakiki wa Riwaya ya Watoto wa Maman’tilie