RIWAYA: MCHEZO WA JOGOO (sehemu ya pili)

Wanaume sita walioshiba misuli walikuwa ndani. Mumewe Mayasa alikuwa miongoni mwao, huyu ndiye aliyekuwa na hasira kuliko wote. Mzee Chekeche aliweza kuwatambua watu wawili, mumewe Mayasa na Bwana Mashiri. Siku tatu tu zilizopita mzee Chekeche alifumaniwa na mke wa Mashiri. Mashiri akamwacha mzee aondoke lakini akavunja ndoa, Mashiri naye alionekana kushiba hasira.
          “Mume wangu nisamehe…” alijitetea Mayasa.
          “Nikusamehe kitu gani, mwanamke huna aibu unazini mchana kweupe bila kuogopa tena na hiki kizee kilichochoka.”
          “Tafadhali kijana nitake radhi, sijachoka mie…” alilalama mzee Chekeche. Mumewe Mayasa akapata hasira akamsogelea mzee na kumpiga kofi moja zito la uso, mzee akamsukuma, akakimbia kuliko mlango, huko akakutana na wanaume watano, wakajaribu kumdhibiti, akawa mbishi, wakampiga ngumi nyingi lakini hatimaye kulingana na uzoefu wa uzinifu wa mzee huyu alifanikiwa kuufikia mlango akiwa amepigwa haswa, mlango wenyewe ulikwisha jeruhiwa hakupata shida, punde tu alikuwa nje, akakimbia kwa mwendo wa farasi akiwa haamini kama kaponyoka kwenye fumanizi lile.
Mzee Chekeche akiwa na kaptura yake nyepesi, hana shati kifua kiko wazi alikimbia mpaka nje, watu walishangaa lakini hakujali, aliitoka Nyambizi guest house, akaibukia katika barabara ya Mtaka shari, kabla hajaivuka gari dogo lililokuwa kasi likataka kumgonga lakini dada aliyeliendesha alimudu kuzifunga breki na kulifanya liserereke na kuacha harufu ya matairi.
“We mzee mchawi nini?” alihoji dada.
          “Binti yangu nisaidie nipe ‘lift’ kuna watu wabaya wanaiwinda roho yangu… nisaidie nitakusimulia.
Binti hakuwa mtu wa hiyana wala maswali mengimengi, aliufungua mlango wa mbele wa gari lake, mzee Chekeche akaingia na kukaa pembezoni mwa dereva. Kwa vile mzee hakuwa na shati binti alifunga madirisha yaliyokuwa na uwezo wa kuzuia watu wa nje kuwaona waliokuwa ndani. Japokuwa kioo cha mbele kiliweza kuonesha, binti hakujali… akazikanyaga pedali gari likatembea tena.
Itaendelea Jumapili...


Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Vichekesho vya Kuchekesha na Kuvunja Mbavu 1