RIWAYA: MCHEZO WA JOGOO (sehemu ya nne)

Akakanyaga mafuta na kuongeza kasi ili gari lifike nyumbani mapema. Kona ya kwanza ilikatwa, ya pili, ya tatu alikuwa nyuma ya geti kubwa jeusi. Akapiga honi, kijana wa getini akafungua, gari likaingia. Wakati wote huo, Chekeche alikuwa amelala, mpini wake ukiwa umesimama wima kama msumari.
Suzi aliegesha gari akamuamsha mzee, mzee akashtuka, alipogundua mpini wake ulisimama, akajipinda kuficha aibu lakini alichelewa, mkono wa Suzi ulikwisha fika ukatambaa kunako nyeti.

          “Mzee unaonesha una hamu, naomba nikate kiu yako kama hutojali!”
Ama kweli mbuzi alifia kwa muuza supu, kwa mzee Chekeche wala haikuhitaji kumuomba, yeye mpini wake uliingia kila shimo, Chekeche ndiye aliyeshikilia rekodi ya mtu mwenye umri mdogo zaidi kufumaniwa na mke wa mtu Duniani, miaka 68 iliyopita mzee huyu aliwahi kufumaniwa na mke wa baba yake mdogo, wakati huo Chekeche alikuwa na umri wa miaka mitano tu! Watu wote hawakuamini, lakini ilitokea.

Shughuli ilikwisha anza ndani ya gari, Chekeche alikuwa anachekecha kisawasawa, makelele mengi yalipigwa na Suzi, ni muda mrefu ulipita hajapata kitu hicho. Gari nalo liliitika kwa kunesanesa.

          “sema jina langu!” chekeche alimrisha akiendelea kusugua.
          “chekeche… chekeche… chekeche… chekec…h…e”
          “sijasikia…” chekeche aliyeathiriwa na ngono za kimagharibi alizungumza tena.

          “cheke… chek…chekech…Chekekekekekecheeee.” Suzi alijbu akiwa kalegea kwelikweli, kwa mara ya kwanza katika maisha yake alifikishwa kileleni, alisikia utamu uliopitiliza… wanaume wote aliowahi kukutana nao hawakuwahi kumfikisha, walimwacha akiwa na hamu yake, lakini shababi barobaro wa miaka sabini na mitatu, mheshimiwa sana mzinzi mtiifu Mzee Chekeche Chekecheo, aliweka rekodi.


Suzi alikuwa hoi taabani akajinasua kutoka juu ya chekeche na kukaa katika kiti, alipotazama mbele, hakuamini alichokiona. Alimuona mumewe aliyevaa suti nyeusi akiwa kasimama imara, kashikilia bastola kwa mikono yake miwili, amelilenga lile gari dogo walilokuwamo, kavimba kwa hasira kama nungunungu na machozi kiasi yakimsongasonga.

Itaendelea jumapili...


Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne