Mtihani wa Kiswahili QT 1

Ndege wanapaa
Soma habari ifuatayo kisha jibu maswali.
Ilikuwa usiku wa manane niliposikia kelele za watu nje ya nyumba yetu ya nyasi. Niliamka haraka kisha nami nikaelekea nje ili nikapate kujua kilichokuwa kikiendelea. Huko nje nilikuta watu wote wamesimama wakipiga kelele huku wakiwa wameangalia juu.
Mwizi! Mwizi! Mwizi!”
Nami nilitazama juu ili nione kilichowaliza, Loooh! Nilikiona kijitu kichafu kimevaa koti jeusi toka sayari ya mbali kikiwa kimeubeba mwezi wetu kikikimbia nao kuelekea mbali huko juu angani. Kabla sijashusha uso wangu chini giza kuu liliingia hata hatukuweza kuonana.
Vijana wa usalama wa nchi, waliwasha mienge ya moto hapo tuliweza kuonana tena, wote tulikuwa na masikitiko makubwa. Nilimuona mama na kaka yangu Mowasha wakilia kwa huzuni.
Maswali
a.   Kipi kiliibwa hata watu wakapiga kelele za kuita mwizi
b.   Kwa nini Mowasha alilia kwa huzuni?
c.   Unadhani tukio linalozungumziwa kitabuni linaweza kutokea katika maisha halisi? Kwa nini?
d.   Fupisha habari uliyosoma kwa maneno yasiyopungua 30 na yasiyozidi 40.

Sehemu B

2.   Toa tofauti mbili zilizopo kati ya sentense na kishazi
3.   Orodhesha aina nne za nomino

Sehemu C

4.   Andika barua ya kiofisi ukimuomba ruhusa mkuu wako wa shule akuruhusu kwenda nyumbani kwa sababu unaumwa.

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne