Mtihani wa Kiswahili QT 1
Soma habari ifuatayo kisha jibu maswali.
Ilikuwa usiku wa manane niliposikia kelele za watu nje
ya nyumba yetu ya nyasi. Niliamka haraka kisha nami nikaelekea nje ili nikapate
kujua kilichokuwa kikiendelea. Huko nje nilikuta watu wote wamesimama wakipiga kelele
huku wakiwa wameangalia juu.
“Mwizi! Mwizi! Mwizi!”
Nami nilitazama juu ili nione kilichowaliza, Loooh!
Nilikiona kijitu kichafu kimevaa koti jeusi toka sayari ya mbali kikiwa
kimeubeba mwezi wetu kikikimbia nao kuelekea mbali huko juu angani. Kabla
sijashusha uso wangu chini giza kuu liliingia hata hatukuweza kuonana.
Vijana wa usalama wa nchi, waliwasha mienge ya moto
hapo tuliweza kuonana tena, wote tulikuwa na masikitiko makubwa. Nilimuona mama
na kaka yangu Mowasha wakilia kwa huzuni.
Maswali
a. Kipi
kiliibwa hata watu wakapiga kelele za kuita mwizi
b. Kwa
nini Mowasha alilia kwa huzuni?
c. Unadhani
tukio linalozungumziwa kitabuni linaweza kutokea katika maisha halisi? Kwa
nini?
d. Fupisha
habari uliyosoma kwa maneno yasiyopungua 30 na yasiyozidi 40.
Sehemu B
2. Toa tofauti mbili zilizopo kati ya sentense na kishazi
3. Orodhesha aina nne za nomino
Sehemu C
4. Andika barua ya kiofisi ukimuomba ruhusa mkuu wako wa shule akuruhusu kwenda nyumbani kwa sababu unaumwa.