Kiswahili Pre Necta 6

Watoto wawili wa mbwa
Muda: Saa 02.30

MAELEKEZO

·        Jibu maswali yote. Swali la tano ni la lazima.
·        Fanya mtihani kwa utulivu. Mtihani huu haupimi uwezo wako wa kupata alama nyingi bali unapima ulipo katika hatua ya ujifunzaji ili tukusaidie kufika unapotakiwa. Ukiangalizia kwa mwenzako au sehemu yoyote ile, utakwamisha juhudi zetu kwako.

SEHEMU A

UFAHAMU
1.   Soma habari ifuatayo kisha jibu maswali.
Mzee Bruda anaye punda wa kiume ambaye anampenda sana. Punda huyu, anamanyoya meusi na meupe yaliyopangiliwa vyema hata humfanya aonekane mtanashati na nadhifu.

Punda wa Bruda hula nyasi peke yake, hupenda nyasi ndefu zilizomea vyema, amalizapo kula, hulala kwa furaha ya shibe.

Watu wengi huenda kumtazama punda wa Bruda. Wazee hutueleza kuwa hawajapata kumuona punda mwenye kuvutia kama yule. Hata hivyo waliomsogelea, aliwapiga mateke wakabaki wakigugumia kwa maumivu.

Kama nilivyosema awali kuwa, Bruda anampenda sana punda wake, punda huyu hajawahi kuadhibiwa kwa makosa yake.

Maswali

A. Kipi kinafaa kuwa kichwa cha habari hii?
B. Ni upi ujumbe wa mwandishi wa habari hii?
C. Unafikiri ni kwa nini punda wa Bruda alivutia sana.
D. Ama hakika anayesemwa na mwandishi si punda bali kajificha tu katika kichaka cha fasihi pengine kwa sababu ya uoga wake. Unadhani ni nani hasa huyu punda wa Bruda?

SEHEMU B

SARUFI
2.   A. Toa maana ya sentensi kisha kwa kutumia mifano, taja aina tatu za sentensi.
B. Changanua sentensi hii kwa njia ya matawi,
Baba analima na mama anapika.

SEHEMU C

UANDISHI
3.   Andika barua ya maombi ya kazi ya ualimu katika shule ya EBENEZA SEKONDARI. Tumia ubunifu wako kutengeneza anuani na majina. Usitumie majina yako halisi.

SEHEMU D

MAENDELEO YA KISWAHILI
4.   Jadili mchango wa sayansi na teknolojia katika kukuza na kueneza kiswahili. Toa hoja sita.
SEHEMU E

Fanya maswali mawili. Swali la tano ni la lazima.

FASIHI KWA UJUMLA

5.   Tunga hadithi fupi kuhusu kisa chochote cha kusisimua.
6.   Kwa kutumia tamthiliya uliyosoma, jadili wahusika wawili kwa kila kitabu huku ukitaja sifa zao.
7.   Waandishi wa riwaya ni WAHENGA. Jadili.
8.   Viongozi wa nchi za kiafrika ni sababu mojawapo ya kukosekana kwa maendeleo. Jadili kauli hii kwa kutumia diwani mbili ulizosoma.




Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne