Mtihani wa Kiswahili Kidato cha Nne | Pre Necta | Jan 2018
JINSI YA KUUFANYA MTIHANI HUU
Mtu yeyote na kokote aliko anaruhusiwa kufanya mtihani huu.
Fanya mtihani huu kwa kutumia aina yoyote ya karatasi.
Ukimaliza, piga picha karatasi hizo kisha zitume WhatsApp kwenye namba ya Mwalimu Makoba - 0754 89 53 21.
Subiri mtihani wako usahihishwe, Urudishiwe na ufanyiwe masahihisho.
Gharama ya mtihani huu ni shilingi 2,000 (elfu mbili) tu.
Namba za malipo ni: M – Pesa 0754 89 53 21 na Tigo pesa 0653 25 05 66
“Kwa kuwa lengo la mtihani huu ni kutaka kujua uwezo na mapungufu ya mwanafunzi ili aweze kupewa mbinu mbadala za kumsaidia kufaulu mtihani wake wa mwisho, kuangalizia majibu hakuna faida yoyote kwani lengo la mtihani si kubaini nani atakuwa wa kwanza na yupi atakuwa wa mwisho!”
Daud Makoba – Mwalimu Makoba – Mwalimu wa Waalimu.
Unataka kufanya mtihani huu na hujaelewa taratibu zake? Wasiliana na Mwalimu Makoba kwa 0754 89 53 21.
Sasa fanya mtihani wako.
Jibu
maswali yote;
SEHEMU A (alama 10)UFAHAMU
1. Soma
kifungu cha habari ifuatayo kisha jibu maswali kama ilivyoelekezwa.
Dubwana limevamia,
linatafuna watoto, vijana na wazee! Meno yake ya shaba yanalifanya litoboe
mpaka mifupa… wengi wameumizwa na Dubwana
hili, wengi zaidi wanagugumia kwa
maumivu.
Baada ya umasikini na
ujinga, ndipo hufuata Dubwana hili hatari, dude ambalo limepotosha maadili na
kuifanya heshima ya jamii yetu izorote!
Ajabu ya yote, washenga wa
Dubwana ndio haohao wanaojinasibu katika majukwaa ya kanyaga tunese, kuwa
wataliondoa Dubwana na kulitupilia mbali! Uliona wapi pepo akamfukuza pepo?
Yangu macho!!
MASWALI
i. Andika kichwa cha habari hiyo kwa maneno yasiyopungua matano.
ii. Kwa mujibu wa habari uliyosoma unahisi Dubwana ni nini?
iii. Ni watu wa aina gani wanatafunwa na Dubwana hili?
iv. Ni akina nani wanajinasibu kuwa wataliondoa Dubwana?
v. Ni yapi maoni yako kuhusu washenga wa Dubwana?
2. Soma
kifungu cha habari ifuatayo kisha fupisha kwa maneno yasiyozidi ishirini.
Baada ya kuachana na mke
wangu Nyangema, aliniachia mtoto mdogo wa miezi minne tu. Kama ujuavyo mimi ni
mtu wa shughuli hivyo nisingeweza kulea mtoto Yule peke yangu, niliamua
kutafuta dada wa kazi za ndani. Nikampata dada “mashallah”, mwenye guu kama
chaki mwendo wa tembo na macho katikati kama anayesinzia – jina lake aliitwa
Shushu.
Lakini sasa nasikitika
kukuta barua mezani na mtoto wangu
akilia hovyo, barua yenyewe inasema Shushu anakwenda kijijini kwao kugombea
Ubunge! Ajabu kwelikweli ati mfanya kazi wangu wa ndani naye kaamua kujiajiri
katika sekta hii rasmi. Akipita nitakuwa nikimuita mheshimiwa Shushu! Ajabu
kwelikweli!
Sasa tujiandae kuona maji yakipanda mlima!
Shushu mfanya kazi wangu wa
ndani anautaka ubunge!
SEHEMU B Sarufi na Matumizi ya Lugha (alama 25)
3. Katika
kila moja ya sentensi zifuatazo, onesha kosa moja la kisarufi kisha andika
sentensi hiyo kwa usahihi.
a. Kinyonga
kinakimbia.
b. Arusi
ya dada yenu zitakuwa Disemba 2015.
c. Mwaka
huu jua zinachoma sana.
d. Tafadhali
nikope shilingi mia nitakurudishia keshokutwa.
e. Kichumba
hiki kichafu sana.
4. Onyesha
dhima ya kiambishi “ni” kilichopigiwa msitari katika sentensi zifuatazo.
a. Alinisaidia
b. Wajumbe
wapo mkutanoni
c. Wakubalieni
d. Yeye ni mvivu
e. Nina kalamu
SEHEMU C (Alama 10) UTUNGAJI
5. Andika insha yenye maneno mia moja kuhusu mada hii.
“kampeni za uchaguzi mkuu 2015”.
SEHEMU D (alama 10) HISTORIA YA LUGHA
6. “Kiswahili
ni kibantu”. Thibitisha kauli hii kwa kutumia hoja sita.
SEHEMU E (alama 45)
chagua maswali matatu, swali la 10 ni la lazima.
7. “Mwandishi
wa fasihi ni mchunguzi wa jamii ambaye huyaweka wazi maovu mbalimbali”. Jadili
jinsi kazi za washairi wawili kati ya hao walioorodheshwa zilivyosadifu kauli
hii.
8. “Matendo
yasiyo na utu hujadiliwa na wasanii”. Thibitisha kauli hii kwa kutumia riwaya
mbili kati ya hizo zilizoorodheshwa.
9. "Tamthiliya huacha mafunzo makubwa kwa hadhira waitazamapo ikiwa jukwaani." jadili kauli hiyo kwa kutumia tamthiliya mbili ulizosoma.
10. Tunga shairi la kimapokeo lenye beti nne, ukiusifia Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
ORODHA YA VITABU
Ushairi
wasakatonge – M.S Khatibu
mashairi ya chekacheka – T. Mvungi
Malenga
wapya – TAKILUKI
RIWAYA
watoto wa maman’tilie – E. Mbogo
Takadini – B. Hanson
Joka la mdimu – A. Safari
TAMTHILIYA
kilio chetu – Medical Aid foundation
orodha – S. Reynolds
Ngoswe penzi kitovu cha uzembe – E. Semzaba
Ukingoni.
Mwalimu Makoba