MWIZI WA SIMU YANGU

Mwizi! Alipokonya simu yangu, kisha akakimbia... Nami nikaanza kumkimbiza. Tukakimbizana. 

Alipofika mbele kidogo akakunja kona, NIKAKUNJA NAYE. Haikuchukua muda akazama katika kichaka, NIKAZAMA NAYE. Akaibukia katika shamba la mpemba, NIKAIBUKA NAYE. Akaamua kunyoosha njia, NIKANYOOKA NAYE.  

Alipoona hali imekuwa ngumu, akachomoa kisu kidogo cha kuchinjia kuku ili anitishe. Mimi nikachomoa panga kubwa la kuchinjia ng'ombe ili aniogope! Akashusha chini kisu chake, nikashusha chini panga langu, kisha nikamuuliza. 

          "Utarudisha simu yangu au tuendelee kukimbizana kama wapenzi wapya wa kihindi?" Hakuwa na maneno mengi, akanipa simu yangu, nikaipokea nikitabasamu. Mwizi aka'jamba' kwa mshangao!  
NIKAJAMBA NAYE. 



#Makoba. 

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika Risala | Kiswahili Kidato Cha Nne