Uhakiki wa Riwaya ya Mfadhili
Riwaya: Mfadhili Mtunzi: Hussein Issa Tuwa Wachapishaji: Macmillan Mwaka: 2007 Utangulizi Riwaya ya Mfadhili imazungumzia suala la mapenzi. Riwaya hii inajaribu kuchambua kwa kina mapenzi na athari zake. Maudhui Dhamira i. Mapenzi Mwandishi ameainisha aina mbili za mapenzi: Mapenzi ya kweli na mapenzi ya uongo. Mapenzi ya kweli yameonekana kwa Gaddi Bullah na dada yake Bi Hanuna. Walipendana kwa dhati tena waliishi kwa furaha kabla Gaddi hajapatwa na matatizo. Gaddi kwa Junior. Japokuwa Junior hakuwa mtoto wa Gaddi, Gaddi alimpenda kama mtoto wake wa kumzaa. Kwa upande wa mapenzi ya uongo kuna: Dania kwa Gaddi Bullah. Mwanamke huyu hana mapenzi ya kweli. Anamsaliti Gaddi na kuamua kuishi na Jerry. Jerry kwa Dania. Kijana huyu hana mapenzi ya kweli. Anasafiri na kumuacha Dania akisubiri ndoa. Pia, Jerry anashindwa kumsaidia Dania pale anapougua ugonjwa wa ini. Anakimbia na hakuonekana tena. ii. Usaliti: Nyambuja anamsaliti mume wake Gaddi kwa kufanya mapenzi nj...