Jinsi ya Kuandika Tangazo| O level na Advance

Jinsi ya Kuandika Tangazo la Gazetini

Matangazo ya gazetini huandikwa kwa lengo la kutangaza biashara. Kwa kuwa magazeti yana wasomaji lukuki, hivyo njia hii hudhaniwa kuwa miongoni mwa njia rahisi zaidi za kuwafikia watu wengi ambao hapo baadaye hugeuka wanunuzi wa bidhaa inayotangazwa.
Uandishi mzuri zaidi wa matangazo ndiyo utakaofanya bidhaa yako inunuliwe. Uandishi mbovu hugeuka kero kwa watu.

Mambo Muhimu ya Kuzingatia

1.   Kichwa cha habari. Kiandikwe kwa herufi kubwa.
2.   Taja aina ya biashara.
3.   Taja bidhaa unazouza na bei zake.
4.   Taja mahali inapopatikana bidhaa yako.
5.   Taja mawasiliano yako. Mawasiliano yanaweza kuwa ya simu, barua n.k. hata hivyo, simu ni  bora zaidi,  kwa sababu mawasiliano yake ni ya haraka.

Mfano wa Kwanza

MASOMO KWA WANAFUNZI WOTE

Kituo cha Mwalimu Makoba kinatoa huduma ya kufundisha wanafunzi wanaorudia mitihani na walio shuleni kwa masomo ya sayansi, sanaa na biashara. Gharama zetu ni shilingi 300,000/= tu kwa mwaka mzima.
Kituo hiki kinapatikana Kinondoni Manyanya mkabala na shule ya sekondari Kambangwa.
Mawasiliano:
0754 89 53 21
0653 25 05 66


Mfano wa Pill

Jifanye wewe ni afisa habari wa shirika la ndege Tanzania, andika tangazo kwa abiria kuhusu katizo la usafiri wa ndege namba TY JET 343 iliyokuwa ifanye safari yake toka Songea kwenda Zanzibar siku ya Ijumaa tarehe 25/5/2018 saa 12 asubuhi, kuwa safari hiyo itafanyika Jumapili tarehe 27/05/2018 saa nane mchana. Mabadiliko haya yanatokana na kuchafuka kwa hali ya hewaa angani. Jina la mtoa tangazo liwe kudura Riziki. 
SHIRIKA LA NDEGE TANZANIA
TANGAZO LA KATIZO LA USAFIRI WA NDEGE
Tunawatangazia abiria wetu kuwa, ndege namba TY JET 343 haitafanya safari yake siku ya tarehe 25/05/2018 saa 12 asubuhi na badala yake itafanya safari siku ya Jumapili tarehe  27/05/2018 saa nane mchana.
Mabadiliko hayo yanatokana na kuchafuka kwa hali ya hewa angani hivyo si salama kusafiri siku hiyo. Pia, tunawaomba radhi watu wote kwa usumbufu uliojitokeza ambao kusema kweli uko nje ya uwezo wetu.
Kudura Riziki

Afisa habari shirika la ndege Tanzania

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Uhakiki wa Riwaya ya Watoto wa Maman’tilie