UTAFITI MPYA WA TABIA ZA NGONO WAJA NA MAJIBU YA KUSHANGAZA!
Utafiti mpya kuhusu tabia za
ngono umefanyika na kuja na majibu ya kushangaza. Utafiti huo uliofanywa nchini
Uingereza umeeleza kwamba, wanawake wana uwezo mkubwa wa kupoteza hamu ya
kufanya tendo la ngono katika ndoa ikilinganishwa na wanaume.
Chanzo kikubwa kilichoeleza
kusababisha wanawake kupoteza hamu ya tendo la ngono, ni kuishi kwa muda mrefu
na waume zao. Kwa wanaume kinachosababisha kupoteza hamu ya tendo la ndoa ni
umri mkubwa.
Jambo jingine ambalo linaweza
kuathiri hamu ya tendo la ngono kwa wapenzi wote wawili ni hali mbaya ya
kiafya.
Watafiti hao wamekuja na majibu
kuwa, tiba pekee kwa mtu mwenye matatizo hayo, siyo dawa bali ni kufanya
uchunguzi wa kina ili kuweza kulibaini tatizo.
Kwa mujibu wa utafiti huo
uliofanywa na BMJ open, wanaume wenye umri wa miaka 35 mpaka 44 hukumbwa na
tatizo la kupoteza hamu ya tendo la ndoa, huku kwa wanawake wakionekana
kukumbwa na tatizo hilo wakiwa na umri wa miaka 55 mpaka 64.