ROONEY KICHWA NGUMU, AVUNJA SHERIA ZA NCHI YAKE

rooney avunja sheria
Rooney ndani ya gari lake

Mshambuliaji wa Everton, Wayne Rooney, amejikuta matatani baada ya kuangukia mikononi mwa polisi. Wanausalama hao wamesema mwanasoka huyo alikamatwa siku ya Ijumaa kwa kosa la kuendesha gari akiwa amelewa jambo ambalo ni kinyume cha sheria za Uingereza.
Rooney ambaye anashikilia rekodi ya kuwa na magoli mengi katika timu yake ya zamani ya Manchester United, alikamatwa na Polisi karibu na nyumbani kwake huko Cheshire.
Huu ni mwendelezo wa makosa  ya staa huyo wa soka kwani siku chache zilizopita aliingia mikononi mwa polisi kwa kosa la kuendesha kwa mwendo mkali zaidi ya viwango vilivyowekwa.

Ukiachilia mbali kesi hizo, mwanasoka Rooney ametangaza kustaafu kuichezea timu yake ya taifa aliyoipatia mafanikio makubwa ikiwemo kuifungia magoli 53 katika michezo 119 aliyocheza.

NA: MOWASHA| NGEME

Popular posts from this blog

Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi Mwaka 2024

Jinsi ya Kuandika CV | Mfano wa CV Wasifu

Uhakiki wa Riwaya ya Watoto wa Maman’tilie