KAULI HII YA KOREA KASKAZINI KWA MAREKANI, INAHATARISHA AMANI YA DUNIA
Korea ya Kaskazini imetoa kauli
nzito ambayo inaweza kuhatarisha amani ya dunia na kusababisha vita kubwa
kuwahi kutokea katika historia ya mwanadamu.
Balozi wa nchi hiyo, Han Tae Song
akiwa katika kikao cha Umoja wa Mataifa amesema,
“Hatua zitakazochukuliwa na Korea Kaskazini zitaisababishia Marekani
machungu makali ambayo hayajawahi kushuhudiwa katika historia yake.”
Maneno hayo yamejiri baada ya
Korea Kaskazini kuwekewa vikwazo kadhaa ikiwemo kupigwa marufuku uuzwaji wa
mafuta na bidhaa kwenda nchi hiyo.
Mapema mwezi huu, Korea Kaskazini
ilifanya jaribio la sita la kombora la nyuklia ambalo linatajwa kuwa kubwa
zaidi. Ufanyaji wa majaribio wa makombora ya Nyuklia unaifanya nchi hii iwe na
migogoro ya mara kwa mara na mataifa mengi ikiwemo Marekani.
Endapo mgogoro huu wa Marekani na
Korea Kaskazini hautatafutiwa suluhisho, huenda dunia ikashuhudia vita kubwa
zaidi kuwahi kutokea katika historia ya mwanadamu.